Subcribe to our RSS feeds Join Us on Facebook Follow us on Twitter Add to Circles

Alhamisi, 12 Juni 2014

TUJIKUMBUSHE HADITHI ZA ABUNUASI.


Abunuasi na hukumu ya kijana.

Hapo zamani za kale katika nchi moja Afrika, paliishi mama mmoja ambaye alikuwa mjane. Muda mfupi tu kabla ya mumewe kufariki walijaliwa mtoto mmoja wa kiume ambaye huyo mama alimlea kwa shida na taabu nyingi. Hata hivyo mama na mtoto wake walipendana ipasavyo. Hapo katika kijiji chao kulikuwa pia na tajiri mmoja ambaye alikuwa bahili na katili kweli. Yule kijana maskini alikwenda kwa tajiri kuomba kazi. Tajiri alimwambia kwamba alikuwa na kazi kwake na angemlipa vizuri sana.
Kijana alifurahi kusikia hivyo na akamwuliza tajiri kwa furaha.
"Kazi gani hiyo utanipa mheshimiwa? Mimi nitaifanya vizuri mpaka hata wewe utafurahia."
Tajiri akamwambia, "Ukilala katika maji baridi sana usiku mzima, nitakupa shillingi laki moja." Ulikuwa wakati wa baridi sana kwamba maji ya ziwa karibu yagandamane kuwa theluji kwa baridi.

Lo! Kijana hakufikiria angeweza kuwa na pesa nyingi hivyo katika maisha yake. Tamaa ya kutaka kumsaidia mama yake ambaye wakati huo alikuwa mgonjwa na mzee, ilikuwa kubwa sana kwa hivyo akakubali bila kufikiria. Mama aliposikia habari hizo karibu azimie kwa wasiwasi na huzuni.
"Mwanangu sitaki uhatarishe maisha yako kwa sababu ya pesa. Mungu yuko nasi na hajatuacha hata siku moja tukalala njaa. Atazidi kufanya hivyo hivyo. Je, ukifa nitabaki na nani mwanangu? Mimi mzee sasa wala sijiwezi!" Kijana alimjibu,

"Mama usiwe na wasiwasi wala woga wo wote! Nitaweza kabisa kulala kwenye maji baridi mpaka asubuhi na siwezi kufa" Mama bado alizidi kubisha, lakini kijana alisisitiza kabisa kwamba lazima afanye hiyo kazi ambayo itawaondolea shida zote za kifedha, kama alivyoona yeye.
Kwa huruma ya mama na wasiwasi juu ya mtoto wake, alikwenda karibu na ziwa pale alimotumbukizwa mtoto wake kwenye maji baridi kama barafu, Alimwona kichwa tu kimelea juu ya maji. Mama aliwasha moto mkubwa karibu na ziwa lile kwenye ufa, ili aweze kumwangazia angalao mwangaza na kumwona. Usiku kucha mama mtu hakufunguka jicho hata dakika moja. Alimlilia Mungu amtunze mwanae asife kwa baridi.
Kwa huruma ya Mwenyezi Mungu, kijana alistahimili baridi yote ile mpaka alfajiri siku ya pili.

Alikwenda kwa tajiri kupokea malipo yake lakini tajiri akamwambia.
"Hupati hata ndururu ng'o!"

"Kijana alishangaa akamwuliza, "Kwa nini mheshimiwa? Uliniahidi kunipa shillingi laki moja nikilala katika maji yabaridi usiku mzima. Usiku mzima nilikuwa ndani ya maji hayo na shahidi wako wameshuhudia na pia mama yangu."

"Ehe, hapo sasa umenena. Mamako aliyekuwashia moto ili upate joto usiku mzima. Hayo ndiyo yalikuwa maagano yetu? Sikumbuki tukiagana kwamba mama yako atakuja na kuwasha moto mkubwa wa kukupa joto kisha unidanganye umelala kwenye maji ya baridi. Unaniona mimi bwege sio? Nenda zako, sikulipi cho chote."

Kijana alikasirika kweli na akamweleza jirani yake mzee Abunuasi. Kama kuna watu Abunuasi aliowazira, ni matajiri waliopenda kuwaangamiza maskini badala ya kuwasaidia. Abunuasi akamwambia kijana asiwe na wasiwasi kwamba rafiki yake Sultan atamsaidia. Akamwambia aende kwake na kumweleza habari zote. Kijana alifuata ushauri wa Abunuasi, lakini Sultani aliposikia kisa chote kutoka pande zote mbili aliamua kwamba kijana asipate malipo kamwe. Abunuasi alishangaa na uamuzi huo wa Sultani mzima wa nchi akamwambia kijana bado asiwe na wasiwasi atapata hela zake. Kijana alimwahidi Abunuasi kumpa shillingi elfu ishirini akimsaidia.

Abunuasi aliandaa karamu kubwa na akawaalika watu wengi pamoja na Sultani na yule tajiri pia. Alichinja mbuzi akatayarisha vitu vyote, mchele, mboga zikakatwakatwa na kuwekwa kando. Moto mkubwa uliwahswa na kila kitu kikawekwa kando ya moto, nyama ya mbuzi katika sufuria pamoja na vitunguu na viungo. Mboga, mchele, zote zikawekwa kando ya moto na Abunuasi akaenda kuwakaribisha wageni wake. Wageni walingojea chakula siku kutwa hawakuona hata maji ya kunywa. Abunuasi aliwaambia kwamba chakula bado kinapikwa jikoni na wala hakijawa tayari. Itabidi wangojee. Mwisho walikasirika na kuingia wote katika jiko. Walikuta moto unawaka vizuri na kando ya huo moto chakula chote walichokuwa wakikingojea kiko kando ya moto huo mkubwa. Sultani akiwa mmoja wa wale waliokuwa na njaa alisema.
"Abunuasi wewe akili zako zinafanya kazi? Hiki chakula ulisema kinapikwa? Mbona moto uko kando na chakula kando? Hakitaiva hata baada ya miaka elfu. Wewe mwehu kweli kama watu wanavyokusema. Unatulisha njaa siku nzima?"

"Usiwe na wasiwasi Sultan, chakula kitaiva tu! Subira huvuta kheri mheshimiwa."

"Acha upuzi na ubwege. Hiki chakula hakitaiva kamwe. Hakipati hata joto la moto huo hata kama mkali kiasi gani"

"Kwa nini kisiive mheshimiwa? Wewe uliamua kesi ya kijana maskini asilipwe na huyu tajiri nduli alipomlazimisha kulala kwenye maji baridi usiku mzima. Kwa njaa na umaskini wake, alikubali. Naye mama yake kwa upendo wa mwanae, alilala kando ya ziwa akimumlikia mwanae ili apate kumwona tu kama angali hai. Wewe uliamua asilipwe kwa sababu ya huo mwangaza aliyemlikiwa na mamake. Basi na hiki chakula kutokana na uamuzi wako lazima kiive hivyo hivyo moto ukiwa kando." Sultani aliona aibu kweli mbele ya watu hao wote, na akaamuru tajiri amlipe kijana pesa zake mara moja na Sultani akampa Abunuasi zawadi kubwa kwa sababu ya ubusara wake. Baada ya hayo yote kukamilika, chakula kiliwekwa juu ya moto, kikaiva na wote wakala.


                                              Wote walimshukuru Abunuasi sana!


Abunuasi and the judgement of a youth.

Long time ago in part of Africa, there lived a widow. A short time before her husband died, they were blessed with a baby boy whom the mother brought up single handed with a lot of difficulties and hardship. Despite these, the mother and her son had a wonderful relationship. There in their big village lived also a very rich man, who was very stingy and very evil. The poor young man went to the rich man to ask for a job. The rich man said in pride that he had a very good job for him and he would pay him very well.

The boy was excited and asked, “What kind of a job will you give me your excellence? Whatever the job is I will do it well that you would be happy too.

“If you sleep in a cold see for the whole night, I will give you one hundred thousand shillings.” It was a very cold season that the water at the see was almost at a freezing point and the rich man knew it. Oh! The boy had never thought of possessing such an amount of money in his life. The great wish to help his mother at her old age was bigger, so he agreed without thinking further of his life. When the mother heard about this, she almost fainted from fear and sorrow over the life of her only son.

“My son I do not want you to endanger your life because of money. God is with us and has never abandoned us even one day that we slept hungry. He will continue to bless us as he did before. If you die, whom will I be left with in this world my child? I am an old woman now and I cannot look after myself.” The mother said in a great sorrow and in tears. “Mama have no anxiety at all. I will be able to sleep in cold water the whole night and I will not die.” The mother continued to beg the boy to change his mind, but he would not hear of it. He was convinced that he would be able to do it and earn that big amount of money which would free them from all the money problems they were having.

From the sympathy and fear over her son, the mother went to sit near the sea where her son was deepened in the cold water. She could only see his head swimming above the water. She decided to make a big fire when it became dark in order to give light for her son to encourage him that his mother was still there watching over him. The whole night the mother did not sleep. She prayed the whole night begging God to sustain her son in that big trial he was going through, and help him go through it without losing his life since he did it for the love of his mother. Through the mercy of God and through the prayers of a mother, the boy survived the terrible cold all night through. He went to the rich man to receive his money but the rich man had other arguments.

“You will not get even a penny from me!” the rich man said. The boy was surprised and asked the rich man, ”Why not your excellence? You promised to give me 100,000 shillings, if I sleep in the cold see the whole night. The whole night I spend in almost freezing water of the sea, you may ask your own witnesses. Even my own mother spend the whole night at the seaside.”

“There you are! Indeed your mother made a big fire at the seaside to warm you up. Is this what we agreed on, that your mother would make fire to warm you up and then come and claim that you spent the night in the cold water all the night? Do you think I am that stupid? Go away I will not pay you anything.

The boy was so angry, and he told his old neighbour Abunuasi about his anger. If there were people whom this old man hated were the rich ones who liked to oppress the poor instead of helping them. Abunuasi told the boy that he should not be angry and that he would get his payments alright, that Abunuasi would help him. He advised him first to take the matters to the King of their land and hear what he would say. The boy followed the advice of Abunuasi and went to the King and told him the whole incident but when the king heard of the story, and from both sides, he decided that the boy should actually not get the money since that is not what they agreed upon. The boy went back to Abunuasi and told him what the king said. Abunuasi was really shocked to hear the decision of a King. He still advised the boy not to have any fear, he would help him still to get his money. The boy promised Abunuasi to give him 20,000 if he helps him.

Abunuasi made a big party and invited many people, including the king and the rich man. All were friends of Abunuasi. He slaughtered many goats, chicken and prepared other things like rice, vegetables were cut into pieces and all the things were put near a big fire but not in the fire to cook. Meat was cut also into pieces and put in big pots. The visitors came and all waited for the big party to eat and drink but were told to wait. They waited the whole day and not even the smell of food did they smell. Hunger started making them nervous. All Abunuasi told them was “I beg your pardon, but the food has been cooking all this time but it is still not ready. We have still to wait.” In the end they were all angry and wanted to see the food which was cooking, so they stormed all in the kitchen, only to see all the food prepared but uncooked and all the pots stood near a big fire. The king being one of the people who suffered hunger asked Abunuasi. “Abunuasi are you right in your head? You have been telling us all this time that the food was cooking and why is the fire put on the side of the food? The food cannot cook even in hundred years! You are a mad man as the people say. You made us hungry the whole day.”

“Do not be angry my King, the food will be ready very soon. Patience brings blessings your excellence” Abunuasi said.

“Stop your foolishness and stupidity. This food will not cook at all. The food does not even get warmth from the fire, even though it is big.

“Why would the food not cook your excellence? You made a decision of a case of a poor youth and this evil rich man, who made the boy to sleep in a cold see the whole night. Due to his poverty and hunger he agreed. His mother due to the love and fear of her son, went to watch over her son the whole night lighting a big fire at the seaside in order to see her son’s head the whole night to make sure that he was still alive. You decided that he should not get even a penny because of the fire the mother lighted. Therefore even this food will cook like how the fire heated the sea water and made the boy warm as you ruled.

The king was so ashamed by the statement made by Abunuasi in front of all those who were invited, and he ordered the evil rich man to pay the poor boy immediately what they had agreed. Abunuasi received a big present and honour from the king due to his wisdom. Afterwards the food was prepared and served and all were happy. They all thanked Abunuasi.



HADITHI.


Maana ya neno hadith katika lugha ya kiarabu ni simulizi au taarifa za kweli au za kutunga, zinazohusiana na wakati uliopo au uliopita. Vile vile neno hili katika lugha lina maana ya mpya yaani kinyume cha kukuu. Neno hili limerithiwa katika lugha ya Kiswahili kama hadithi.

AINA YA LUGHA YA MAZUNGUMZO KWA KUZINGATIA MUKTADHA MBALIMBALI.



MAANA YA LUGHA.


Lugha ya mazugumzo ni maongezi ya watu wawili au zaidi bila kutumia maandishi. Lugha ya mazungumzo ambayo ndiyo lugha kongwe zaidi ya lugha ya maandishi ina dhima kubwa ya kufanikisha mawasiliano miongoni mwa watu au kikundi fulani. Lugha hii ya mazungumzo ilianza punde tu binadamu alipoanza kukabiliana na mazingira yake, hivyo kimsingi lugha ya mazungumzo ndiyo nguzo kuu ya kufanikisha shughuli zote za kibinadamu kutokana na nafasi yake kimatumizi.


Aina ya lugha ya mazungumzo kwa kuzingatia mazingira rasmi na yasiyo rasmi:

Mazingira rasmi: kwa mujibu Kihore (2004) haya ni yale mazingira yanayoendana na kaida za kijamii, kisheria na kiutamaduni ambazo huhusisha matumizi ya lugha iliyosanifu. Huu ni muktadha unaohusisha ushirika wa upande mmoja, kama vile msamiati wa kiufundi na adabu maalum. Mfano wa mazingira rasmi ni kama vile ofisini, mahakamani, bungeni, kanisani, msikitini na katika elimu. Katika mazingira rasmi tunapata aina mbili za lugha ya mazungumzo ambazo ni jagoni na rejesta.

Jagoni: ni aina mojawapo ya lugha inayotumika katika taaluma fulani mahususi kama vile fasihi, isimu, sheria, sayansi, uhandisi, biashara nakadhalika. Hii ina maana kwamba, lugha hii itafahamika na wale tu walioko katika taaluma husika au wenye maarifa ya taaluma hiyo. Kwa mfano wanaisimu hutumia maneno kama vimadende, vitambaza, vipasuo kwamizi nk. wakirejelea jinsi ya utamkaji wa aina fulani za sauti katika lugha.

Rejesta: Halliday (1989), anafasili rejesta kama mtindo wa lugha kutegemeana na kazi au shughuli. Vilevile fasili hii inaendana na fasili ya Habwe na Karanja (2007).

Kwa ujumla tunaweza kufasili rejesta kama mtindo wa lugha kutegemeana na kazi fulani, muktadha wa matumizi, lengo na uhusiano wa wanaowasiliana. Katika muktadha rasmi rejesta hurejelea upande mmoja kama vile, msamiati wa kiufundi, adabu maalum na matumizi ya lugha fasaha, mfano katika elimu, mahakamani nakadhalika.

Mazingira yasiyo rasmi: haya ni mazingira ambayo hayafungwi na kaida, sheria na tamaduni za kijamii. Mazingira haya hutumia msamiati ambao si rasmi yaani lugha isiyokuwa sanifu. Katika mazingira haya tunapata aina zifuatazo za lugha ya mazungumzo: misimu, agoti, rejesta na lahaja.

Misimu: Msanjila na wenzake (2009:19) wanafasili dhana ya misimu kuwa ni aina ya misemo katika lugha ambayo huzuka na kutoweka. Sifa kuu ya misimu ni kwamba haidumu muda mrefu na sio lugha sanifu, na watumiaji wa misimu huwa ni kikundi cha wazungumzaji wa lugha katika jamii ambao kimsingi huishi katika eneo moja.

Ngure (2003:147) anaonekana kukubaliana na Msanjila kwa kiasi kikubwa isipokuwa yeye anaweka mkazo zaidi hasa pale anapodai kwamba, uzukaji wa misimu ni wa ghafla na wakati fulani hufuatana na mambo au matukio maalum ya wakati au msimu huo. Anaendelea kufafanua kuwa misimu huzuka/huibuka na kutokeweka kufuatana na hali mbalimbali za kimazingira. Hata hivyo baadhi ya misimu hudumu na kuwa sehemu ya lugha. Kwa mfano neno matatu (Kenya) au daladala (Tanzania) ni neno lililotumika kurejelea nauli iliyolipwa miaka ya sitini. Hivi leo limekuwa neno linalomaanisha aina fulani ya magari ya usafiri. Katika muktadha wa mazungumzo misimu inachukuliwa kama ni aina mojawapo ya lugha ya mazungumzo itumiayo maneno yanayozuka kutokana na matukio mbalimbali ya kijamii, ambayo hiibuliwa na makundi mbalimbali katika jamii, hivyo misimu hutofautiana baina ya kundi moja na jinguine. Kwa mfano, misimu wanayotumia vijana ni tofauti na wanayotumia wazee au yanayotumia wanaume ni tofauti na wanayotumia wanawake.

Vilevile hata mazingira inamotumika misimu si mazingira rasmi kutokana na maneno yake kuzuka na kutoweka na hayatumiwi katika mazingira rasmi.

Agoti: ni lugha itumiwayo na kundi fulani la wahalifu au watu ambao wanaficha uovu wao usifahamike katika jamii wanamoishi. Mara nyingi lugha hii hutumiwa katika mazingira yasorasmi na kikundi kidogo cha watu kama vile, madereva wa magari, watumiaji wa madawa ya kulevya (mateja), majambazi, vibaka na wahuni wa mtaani. Mfano wa agoti inayotumiwa na watumiaji wa madawa ya kulevya ni kama vile, ndumu – bangi, sherehe ilikuwa na waalikwa wengi – soko la madawa ya kulevya lilikuwa na wateja wengi. Rejesta: Katika mazingira yasiyo rasmi, rejesta hutumia msamiati usio rasmi, matumizi ya misimu na ukatizaji wa maneno pamoja na udondoshaji wa baadhi ya vipashio katika maneno. Mfano, rejesta inayotumika katika mazingira yasiyorasmi kama vile mgahawani au hotelini ni kama vile nani wali ng’ombe? Ikiwa na maana kwamba nani aliyeagiza wali na nyama ya ng’ombe.

UHAKIKI WA NADHARIA YA KI-MARX KATIKA FASIHI.

Swali.
Eleza mawazo makuu yanayojitokeza katika nadharia ya Umarx kisha hakiki Tamthilia ya Kwenye Ukingo wa Thim kwa kutumia nadharia ya Ki-Marx.
DONDOO:
UTANGULIZI
  Maana ya Nadhari
  Maana ya Umarx
  Maana ya Nadharia ya Umarx
  KIINI
  Mawazo makuu yanayojitokeza katika nadharia ya Umarx.
 Sifa na udhaifu wa nadharia ya Ki-Marx
 Uhakiki wa Tamthilia ya Kwenye Ukingo wa Thim.
·        HITIMISHO
·        MAREJEO
Nadharia ni dhana iliyofafanuliwa na wataalam mbalimbali kama ifuatavyo:
Wafula na Njogu,(2007:7) Nadharia ni jumla ya maelekezo yanayomsaidia msomaji au mhakiki kuifahamu kazi ya fasihi kwa kufuata utaratibu maalumu.
Tuki, (2004:300) Nadharia ni mawazo, maelezo au muongozo uliopangwa ili kusaidia kueleza, kutatua au kutekeleza jambo fulani.
Tunakubaliana na fasili iliyotolewa na Wafula na Njogu, kutokana na kwamba fasili hii imetaja vitu muhimu kama vile, maelekezo ambayo ndiyo yanayomuongoza msomaji au mhakiki ili asivuke mipaka ya mawazo ya hiyo nadharia aitumiayo ili kufanikisha kazi kwa ufasaha.
Maana ya Umarx:
Wamitila,(2006:182) anasema, umarx ni falsafa ya kiyakinifu hasa kwa kuwa pana msisitizo mkubwa kwenye msingi wa hali za kiyakinifu za maisha kama mazingira ya kuishi kuliko mawazo katika maisha ya binadamu (ikimaanisha kwamba mawazo yake hayategemezi kwenye dhana dhahania kama urembo, ukweli au ndoto bali anayategemeza kwenye uhalisia unaoonekana.
Nadharia ya umarx ilianzishwa na Karl Marx mwaka 1818-1863 na Fredrich Engles (1820-1895).Katika nadharia hii Marx amejikita katika historia na miundo ya kijamii kwa kupitia hoja kuu zifuatazo.
Historia ya maisha ya binadamu inaweza kuelezeka katika misingi yakinifu ya kiuchumi ambayo itachunguza njia za uzalishaji mali pamoja na miundo ya kiuchumi na pia huathiri uzalishaji mali na usambazaji wa mali hizo. Hivi vyote kwa pamoja huunda misingi ambapo kwenye misingi hiyo huunda maadili, itikadi, dini na utamaduni.
Hoja nyingine ni kuamini kuwa historia ya binadamu inadhihirisha au kuakisi harakati zinazoendelea katika matabaka ya kiuchumi-jamii. Marx alisema “Historia ya maisha ya binadamu ni ya harakati za kitabaka”.
Harakati za kitabaka katika jamii. Nadharia ya ki-marx inaangalia matabaka katika ngazi mbalimbali kama vile ngazi ya familia, dini na elimu.
Ubepari kama njia ya uzalishaji mali na mara nyingi huharibiwa na tabaka la chini, hivyo ubepari hujitengenezea njia za kujiharibu wenyewe. Kutokana na unyonyaji na ukandamizaji unaoufanya kwa tabaka la chini.    
Njia ya kuondokana na ubepari huu jamii  lazima ikemee.
Mshikamano uliopo baina ya tabaka tawaliwa. Kwa mujibu wa marx ili kuondokana na mfumo wa unyonyaji na ukandamizaji, jamii lazima iungane ili kubadilisha mfumo uliopo.
Matamanio ya kitabaka yanaakisi jamii hiyo au itikadi ya jamii iliyopo. Kwa mujibu wa nadharia ya umarx tabaka la chini itikadi yao ni kupambana na tabaka la juu ili kuondokana na unyonyaji na ukandamizaji na tabaka la juu itikadi yao inaonekana kuwa ni halali kulikandamiza tabaka la chini.
Fasihi inayojitokeza inaweza kuyaakisi au kuyadhihirisha mahusiano ya nguvu katika jamii, matamanio na matakwa ya matabaka yaliyopo katika jamii yanaakisiwa katika itikadi iliyopo katika jamii.
Sifa za Uhakiki wa kimarx:
Kuna muelekeo mkubwa wa kuitazama sanaa katika nadharia hii kwa kutilia mkazo mkubwa kwenye dhamira.
Ni mkabala ambao unaingalia fasihi kwa kuhusisha na mazingira yake ya kihisitoria pamoja na shughuli zingine za kibinadamu.
Ni nadharia inayopinga au mtazamo wa kubagua au kutenga fasihi na mazingira yanayoizaa kama ilivyooneshwa kwenye nadharia nyingine kadhaa.
Kwa kuhimiza kuchunguzwa vipengele vya kijamii na kiuchumi uhakiki unaelekea kupanua uwanda wa fasihi.
Udhaifu wa nadharia hii ya Kimarx:
Uhakiki wa Ki-marx unaishia kuidunisha na kuipuuza kazi ambayo ina sifa za kiwango cha juu sana za kiujumi au kisanaa kwa kuwa ni dhaifu kiitikadi  licha ya kuwa itikadi sio kaida au kanuni ya sanaa au ubunifu. Hatuwezi kupuza kazi kwa misingi ya kiitikadi tu.
Hivyo huzichunguza sifa mbalimbali za kazi ya kifasihi pale tu zinapoingiliana na miundo ya kihistoria jamii au kiuchumi kwa kufungamana na itikadi yake.
Matokeo ya mtazamo huu wa kuyamulika zaidi masuala ya kidhamira yanaifanya nadharia hii kutoangaza vipengele vingine vidogovidogo ili kutathimini ubunifu au upekee wa kazi inayohusika.
Unaelekea kuchunguza muktadha wa kihisitoria kwa kuelemea mno kwenye vigezo vya kiuchumi.
Jamii ni kielelezo kinachoshikiliwa kama upeo wa kuendelea na kusambaratika kwa mfumo wa kibepari unaoelekea kuwa na elementi za kinjozi.
Namna ya kutumia uhakiki wa Ki-marx katika kazi za kifasihi.
Miaka ya hivi karibuni uhakiki wa kazi za kifasihi umezidi kupanuka katika kuelezea masuala ya kijamii na kisiasa. Hivyo unapotumia uhakiki wa ki-marx katika kazi za kifasihi lengo ni kuonesha tofauti za kijamii, kisiasa, kiuchumi kulingana na maelezo yalivyo katika kitabu. Hii inaonesha itikadi ya kijamii ya mwandishi na kuweka uhusiano kati ya uzoefu wa kijamii wa mwandishi na wa wahusika wake.
Katika kutekeleza itikadi za uhakiki wa ki-marx kuna hatua tano za kufuata ili kuhakiki kazi ya fasihi kwa ufanisi.
Kueleza jinsi wahusika wanavyohusiana:                                                                          Uhusiano baina ya watu, muingiliano wao utaonesha madaraja na ishara fulani zinazoendana na tofauti za matabaka ya kijamii.
Kutathimini kazi za wahusika:                                                                           
Uhusika wao umejikita katika mifumo ya kimatabaka ambapo kazi anayofanya mhusika inaashiria moja kwa moja sehemu alipo katika mfumo. Kiwango cha anasa na kiwango cha utendaji kazi navyo vinaonesha sehemu alipo katika mfumo.                                                      
Kuonesha jinsi wahusika wanavyotumia muda wao wa mapumziko.                   Nadharia ya ki-marx inaeleza kuwa mtu anauwezo wa kutumia muda wake wa mapumziko kwa namna ya uzalishaji mali au anavyopenda yeye. Huu muda wa kupumziko huashiria namna mtu anavyoishi na jamii inayomzunguka.
Kutathimini jukumu la serikali, 
kuonesha mfumo wake, vyombo vya utekelezaji na jinsi jamii inavyopokea mafanikio yake.                                                                                                 
Kurejea waandishi wengine wa ki-marx na kutafiti vipindi ambavyo kazi hiyo ya kifasihi imechapwa na kisha kuhusianisha mawazo yaliyotolewa na kipindi hicho.
Kulingana na mawazo ya ki-marx yaliyofafanuliwa hapo juu tunaweza kuhakiki tamthiliya ya “Kwenye Ukingo wa Thim” kama ifuatavyo:
Tamthiliya ya Kwenye Ukingo wa Thim iliyoandikwa na Ebrahim Hussein (1988). Hussein ni mtunzi maarufu sana ambaye ameumudu usanii wa tamthiliya za Kiswahili. Miongoni mwa Tamthiliya zake ni Kinjeketile, Mashatani, Arusi na Kwenye Ukingo wa Thim. “Kwenye Ukingo wa Thim” inaonesha migogoro iliyopo ya kitabaka baina ya mahitaji ya mila na maisha ya kisasa, utawala na utawaliwa, vilevile kuna utabaka wa kipato cha juu na cha chini, utabaka wa kielimu (waliosoma na wasiosoma). Vilevile ameonesha harakati za kuondoa matabaka hayo.
Uhakiki wa kitabu utafanyika kwa kujikita zaidi katika nadharia ya ki-marx.
Tukianza na kipengele cha maudhui dhamira zilizojitokaza ni kama ifuatavyo:
Dhuluma na unyonyaji: Mwandishi amemtumia Martha kuonesha dhamira hii. Ameonesha jinsi Umma klani ulivyomnyang’anya Martha mali zake zote baada ya kufiwa na mumewe.
Mfano; ukurasa.33 “mawe yanavunja viyoo kikundi cha watu kimeingia.Wanaimba mchaka mchaka chinja…wanachukua vitu, mapambo, glasi wanaondoka….”
Suala la dhuluma lipo katika jamii hiyo, basi kutokana na nadharia ya umarx anaonesha kuwa ili jamii iondokane na dhuluma lazima ipambane ili kuliondoa tabaka la unyonyaji.
Matabaka: mwandishi ameonesha suala hili jinsi linavyojidihirisha wazi kati ya wenyenacho na wasionacho. Mfano; familia ya Herbert, hawa ndiyo wenyenacho na wasionacho ni kama vile Stella (ukurasa.1), watawala na watawaliwa , mfano; viongozi kama DC, na watawaliwa mfanyakazi wa kwanza na mfanyakazi wa pili (19-20), wasomi na wasiosoma. Wasomi kama vile Herbert, Chris, Jean na Ben. Na ambao si wasomi ni kama vile Stella, George na Mzee. Suala hili la matabaka katika jamii ni suala la kiyakinifu ambalo limejidhihirisha dhahiri katika jamii. Hivyo kwa mtazamo wa ki-marx unatoa pendekezo kuwa ili jamii ijikomboe na matabaka lazima ifanye mapinduzi.
Ubepari: mwandishi ametumia mawazo ya mfumo wa uzalishaji mali wa kibepari kwa kuonesha tabia za mfumo huo kwa mfano; watu kumiliki majumba makubwa, magari, viwanja, makampuni nk. Mfano;
Veranda kubwa ina vitu vizuri. Vitu vyenye thamani, ina mapambo, vitu vya shaba…”(ukurasa.1)“Kazi nyingi viwanja bado havijalipiwa kodi mwaka huu,halafu Stella hana mahali pa kukaa toka zile nyumba walizokuwa wakikaa kubomolewa na kujengwa afisi mpya za kampuni mpya ya Kiamerika (ukurasa.5)”
Suala la ubepari katika jamii linajidhihirisha dhahiri, kwani kuna watu wanamiliki mali nyingi bila usawa wakati wengine hawana kabisa. Hivyo Marx anatoa pendekezo kuwa ili jamii iwe na usawa lazima kuwe na umiliki sawa wa mali katika jamii.
Uongozi mbaya: mwandishi ameonesha uongozi kama tabaka ambalo linafanya kazi kwa maslahi ya tabaka hilo. Hali hii inajidhihirisha katika sehemu za mjini ambako hukaa viongozi au watawala, huko ndiko kuna maendeleo ya kijamii na kiuchumi ambapo watu wenye kipato cha juu huishi, lakini tabaka tawaliwa ambalo wengi wao wanaishi kijijini limeoneshwa kutopewa huduma muhimu za kijamii. Mfano, miundombinu mibovu kama vile barabara na hata maji hakuna. Utaona kwamba juhudi za kujenga barabara pamoja na kisima cha maji kule kijijini ilikuwa ni kwa ajili ya kufanikisha mazishi ya Herbert kwa vile ni kiongozi lakini haikuwa nia ya kuleta maendeleo katika kijiji hicho. Mfano katika (ukurasa.19)
Mfanyakazi I: “Tumekuja kutengeneza barabara.Wapi ile daraja mbovu. Tunataka kutengenesa haraka sana”.
Mfanyakazi wa II: “Na kisima? Kisima cha kijiji kiko wapi?Tunataka tasama kama maji safi”.
Hapa katika nadharia ya umarx inasema kwamba ili jamii iondokane na uongozi mbaya unaojali tabaka tawala lazima tabaka tawaliwa lipambane ili kuondokana na uongozi mbaya katika jamii.
Dini: suala hili limeweza kijitokaza pale Herbert alipokufa, mkewe (Martha) aliponyang’anywa mali zote na Umma Klan. Tunaona kwamba Martha aliamua kupambana ili aweze kukomboa mali zake lakini Pasta alimkataza na kumuambia amuachie Mungu.
Mfano katika (ukurasa.32) Pasta:“M-a-a-r-th-a-a! Martha! Mlani shetani. Martha!”
 Martha: (Anarejesha bunduki. Pasta anaichukuwa. Anairejesha mahali pake)                                               
Kwa mujibu wa nadharia ya Umarx inasema kwamba, dini ni kama kilevi cha kuwalewesha au kuwapumbaza watu na kuwafumba fikra zao wasiendelee na harakati za kujikomboa.
Ujasiri: mwandishi ameonesha dhamira ya ujasiri kwa kumtumia Martha, dhamira hii imejidhihirisha pale ambapo shemeji yake (George) alipochukua hati ya nyumba yake. Martha alichukua bunduki na risasi na kutaka kumlenga George. Hivyo Martha aliweza kuonesha ujasiri katika kukomboa mali zake. 
Hii inajitokeza katika (ukurasa.32)
“…Martha anachukua bunduki. Anachukua risasi kwenye mtoto wa meza. AnamlengGeorge”.
Kwa mujibu wa nadharia ya Umarx katika suala la kupinga unyonyaji unahitajika ujasiri na mapambano ili kuhakikisha usawa unapatikana kwa wote, na kusiwepo na unyonyaji wala ukandamizaji.
Umoja na mshikamano: suala hili limejitokeza pale ambapo jamii ilivyoweza kupigana na kuweza kurudisha tena ardhi yao mikononi mwao. Hii inaonesha hapo awali walikuwa na ushirikiano mpaka wakaweza kurudisha ardhi yao. Na vilevile wanaitukuza kwa mila zao.
Katika (ukurasa.23) Mzee: “….Ardhi hii ni yetu.Mali yetu. Toka enzi za Ruoth. Mkuki na bunduki iliteka ardhi hii. Ni yetu. Tumeilipia kwa damu. Na tunaitukuza kwa mila zetu…”                 
Pia umoja na mshikamano umejitokeza kwa kupitia akaunti ya pamoja ya kijiji, ambapo mapato yote ya kijiji yana milikiwa na kijiji. Mfano (ukurasa.19) Muuza duka:  “nataka pesa za ndoo mbili, ufagio, chumvi; mbao”. 
Mzee:“Andika katika akaunti ya kijiji”.                                                                                                                                                                                
Nadharia ya Umarx inasema kwamba, kama jamii ikiwa na umoja na mshikamano basi matabaka ya aina yoyote hayatakuwepo na umilikaji mali utakuwa ni wa jamii nzima katika hali ya usawa.
Kutokana na nadharia ya umarx tunaweza kuchambua baadhi ya vipengele vya maudhui;
Migogoro: migogoro iliyoonekana katika tamthilia ya Kwenye Ukingo wa Thim ni pamoja na mgogoro kati ya serikali na wananchi  wa kijijini pale ambapo wanakijiji walikuwa wanapinga serikali juu ya utengenezaji wa barabara na kisima kwa ajili ya kufanikisha mazishi ya Herbert. Mfano, (ukurasa.19) Mzee:  “Barabara tunatengeneza sisi wenyewe. Ni kazi ya kijiji. Ni wajibu wetu. Wajibu wa Umma Klan”.
Vilevile kulikuwa na mgogoro kati ya Martha na Umma Klan pale ambapo Martha alinyang’anywa mali alizoachiwa na mume wake baada ya kufariki.
Kwa mujibu wa Marx migogoro hainabudi kuwepo katika jamii. Na ni lazima pawepo migogoro ndani ya jamii yoyote ya kitabaka ili kuleta maendeleo.
Falsafa: (Ni mwelekeo wa imani ya msanii juu ya kazi aliyoiandika au ni mawazo makuu ya mwandishi kuhusu maisha). Falsafa ya mwandishi ni ya kimapinduzi, yaani anaamini kuwa ili kuweza kuleta maendeleo au kuleta mabadiliko katika jamii ni lazima kuwepo na mapinduzi dhidi ya matabaka, unyonyaji, ukandamizaji na unyanyasaji. ndipo kutakuwa na usawa katika jamii. Hivyo basi moja kwa moja falsafa hii ya mwandishi inaendana na falsafa ya Ki-marx ambayo ni ya kimapinduzi.
Msimamo: (Ni itikadi anayoishikilia mwandishi ambapo hawezi kuyumbishwa juu ya mtazamo wake). Mtazamo wa mwandishi wa tamthilia hii ni wa kiyakinifu, kwani ameonesha mapambano ya kimatabaka ambayo yanaweza kuhalisika katika jamii. Vilelvile uhalisia huu unajidhihirisha katika nadharia ya Umarx.                                                    
Pia nadharia ya umarx inaweza kutumika katika kuchambua baadhi ya vipengele vya fani ambavyo ni;
Wahusika: mwandishi amewaumba wahusika kwa namna inayosadifu matabaka yao. Mfano;Herbert anawakilisha tabaka la juu, kwani ameonekana kumnyonya mafanyakazi wake wa ndani ambaye ni Stella. Katika (ukurasa.2) Stella muda wote alionekana akifanya kazi bila kupumzika.
Vilevile Stella amechorwa kama mwakilishi wa tabaka la wanyonywaji, kama anavyoonekana akitumikishwa sana, na hata hakuwa na mahali pa kuishi baada ya nyumba alimokuwa anaishi kubomolewa ili kupisha ujenzi wa kampuni mpya ya kiamerika. Rejea ukurasa.5 Hebert; “…Halafu Stella hana mahali pa kukaa…”                                                                 
Martha naye amechorwa kama mnyonywaji hasa pale aliponyang’anywa mali zote na ndugu wa mume wake hali iliyopelekea kifo chake.
Mandhari: mwandishi ametumia mandhari mbalimbali kama vile mandhari ya mjini kuwakilisha eneo linalokaliwa na watu wa tabaka la juu, wasomi na tabaka tawala. Mfano familia ya Herbert mali walizokuwa nazo kama majumba, magari, inaonekana katika ukurasa.2
Mwandishi pia ametumia mandhari ya kijijini kuwakilisha tabaka tawaliwa, watu wa kipato cha chini na wenye hali duni ya maisha. Mfano; Mzee, mfanyakazi wa kwanza na wapili pamoja na Lydia.
Matumizi ya Lugha: kwa kiasi kikubwa lugha iliyotumika ni ya kitabaka yaani lugha inayotumiwa na wasomi au watu wa tabaka la juu ni tofauti na lugha inayotumiwa na watu wa tabaka la chini. Mfano, (ukurasa. 20)
D.C:   “Nani ametoa amri ya kutengeneza barabara?” (utawala) Mfanyakazi 1:   “Ni serikali sir” D.C:   “Rudisha trekta na vyombo vyote vya kazi” P.S:   “kwa nini daraja haitengenezwi? Kwa nini darajambovu?” D.C:   “Haya anza mara moja. Tengeneza barabara.” Mfanyakazi 1 “Yes sir”.
Hivyo inaonesha wazi kwamba lugha anayoitumia D.C na P.S ni ya kiutawala huku Mfanyakazi 1 akitumia lugha ya unyenyekevu.
 Kwa kuhitimisha, nadharia ya umarx ni nadharia inayosawiri masuala ya kiuchumi-jamii kiyakinifu. Hata hivyo ina sifa na udhaifu wake kama ilivyooneshwa hapo awali.
Kuhakiki kwa kutumia nadharia hii kumejikita sana katika kipengele cha maudhui na kugusa kidogo sana au kupuuza kabisa vipengele vya fani ambavyo navyo ni muhimu sana katika kazi za fasihi. Hivyo basi katika uhakiki wa kazi za fasihi nadharia moja haijitoshelezi kuhakiki kitabu.  Hivyo ili mhakiki wa kazi za kifasihi aweze kufaulu vizuri ni lazima atumie nadharia zaidi ya moja katika kuhakiki vipengele vya fani na maudhui, kwani nadharia moja haijitoshelezi kuhakiki vipengele vyote.                             
MAREJEO:
TUKI (2004). Kamusi ya Kiswahili Sanifu.Oxford University Press East Africa Ltd. Nairobi.
Hussein, E.(1988). Kwenye Ukingo wa Thim. Oxford University Press East Africa Ltd. Nairobi.
Wamitila, K.W (2002). Uhakiki wa fasihi, Misingi na vipengele vyake. Phoenix Publishers Ltd. Mombasa.
Wafula, R. M na Njogu, K (2007). Nadharia za uhakiki wa Fasihi. Sai Industries Ltd. Nairobi.

UHAKIKI WA DIWANI ZA KISWAHILI.


UHAKIKI WA DIWANI YA WASAKATONGE


UTANGULIZI

Diwani ya Wasakatonge ni miongoni mwa diwani za hivi karibuni zinazotanabaisha matatizo mbalimbali yanayoikumba jamii katika maisha yake ya kila siku. Matatizo hayo yanaonekana kuwa kama saratani isiyo na tiba. Hata hivyo, msanii ana matumaini kwamba, iwapo wananchi wa kawaida wataungana na kuamua kupambana, ni dhahiri kwamba matatizo hayo yatatoweka kabisa. Miongoni mwa matatizo hayo yataoneshwa kwenye kipengele cha maudhui huku yakishadidiwa na fani.

MAUDHUI: ni jumla ya mambo muhimu yanayoelezwa katika kazi ya kifasihi. Maudhui yanajengwa na vipengele vidogovidogo vifuatavyo; dhamira, ujumbe, mgogoro, mtazamo na falsafa.

DHAMIRA: ni jumla ya maana anayovumbua mwandishi aandikapo kazi yake na jumla ya maana anayoipata msomaji pindi anapoisoma kazi fulani ya kifasihi. Kifasihi kuna aina mbili za dhamira yaani dhamira kuu na dhamira ndogondogo. Dhamira kuu ni lile wazo kuu la mwandishi katika kazi, wakati dhamira ndogondogo ni zile dhamira zinazojitokeza ili kuipa nguvu dhamira kuu. Dhamira zilizojitokeza katika diwani hii ni kama ifuatavyo:

UONGOZI MBAYA: ni aina ya uongozi ambao haujali maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla. Ni uongozi unaotumia mabavu na unaojali maslahi binafsi, yaani haufuati misingi ya utawala wa sharia. Katika diwani hii msanii anaonesha kuwa nchi nyingi duniani hasa zile za kiafrika zinakabiliwa na tatizo la uongozi mbaya. Viongozi walio wengi ni madikteta ambao hawataki kuachia madaraka wala kuwapa watawaliwa uhuru wa kuzungumza.

Hali hii tunaopata katika shairi la “MADIKTETA” (uk.21) ambapo msanii anasema kuwa harakati za kusaka uhuru au demokrasia kwa njia ya mtu haijawahi kuzaa matunda yanayotarajiwa. Harakati hizi zimekuwa zikizalisha viongozi “Miungu watu” au marais walio madikteta, kama ilivyokuwa kwa Mabutu Seseko-huko Zaire (kwa sasa DRC), Bokosa-huko Afrika ya Kati na Idd Amini-huko Uganda. Madikteta hawa wamekuwa na kila aina ya uovu ikiwa ni pamoja na kukumbatia ukabila, udini na uvamizi kwa nchi nyingine. Haya tunayapata katika shairi la “SADDAM HUSSEIN” (uk.26:4) anasema;

4. “Nakuafiki, Saddam, si kwa uvamizi wako,Na ujue kwamba,
Huo si uasi
Kwa wakubwa mila,
Saddam, yamesha tendeka sana!”

Viongozi wa aina hii huwanyima wananchi wao uhuru wa kusema ikiwa ni pamoja na ule wa kujiamulia mambo yao wenyewe kama katika shairi la “MARUFUKU” namba 45 (uk.36)
“Sitakiki uone,
Ingawa una macho,
Sitaki useme,
Ingawa una mdomo,
Sitaki usikie,
Ingawa una masikio,
Sitaki ufikiri,
Ingawa una akili,
Sababu utazinduka,
Utakomboka,
Uwe mtu,
Hilo sitaki,
Marufuku.”

Viongzozi wabovu (madikteta) ni wapenda dhuluma na manyanyaso. Huwadhulumu na kuwanyanyasa raia wao na raia wa nchi nyingine kama inavyojidhihirisha katika mashairi ya “KOSA” (uk.3), na “FAHARI LA DUNIA” (uk.45). Katika shairi la “KOSA”, tunaona kuwa unyanyasaji wa wananchi wa kawaida hutokea pale ambapo wanapokuwa wanadai haki zao. Mshairi anasema:
3. “Kosa letu kubwa,
Kudai haki?
Yetu miliki?
Mna hamaki,
Na huku mnatukashifu!”

Katika shairi la “FAHARI LA DUNIA” (uk.45) tunaambiwa kuwa kuna kiongozi mwenye nguvu (Marekani) ambaye mchana kutwa usiku kuchwa linanyanyasa nchi nyingi bila sababu za msingi. Msanii anasema:
5. “Fahari la Dunia,
Kwa kiburi, linatesa,
Lajigamba,
Linatamba,
Kuwa mwamba,
Linaoneya.”

Viongozi wabovu siku zote ni wanyonyaji na hushirikiana na watu wengi wenye nguvu kubeba mirija ya unyonyaji na kuanza kuwanyonya raia wa kawaida. Hali hii hujitokeza sana katika nchi za Dunia ya tatu. Haya yote tunayapata katika mashairi ya “MVUJA JASHO” (uk.12-13), “MIAMBA” (uk.29-30), “MUMIANI” (uk.34) Katika shairi la “MVUJA JASHO” msanii anaonesha kuwa raia wa kawaida wanafanya kazi kubwa na ngumu sana lakini malipo yao hayalingani na jasho wanalolitoa. Katika shairi la “MIAMBA” tunaambiwa kuwa wanyonge hawana chao, jasho lao na wao wenyewe ni chakula cha wakubwa na watawala wao. Ubeti wa 4 wa shairi hili msanii anahoji juu ya suala hili kwa kutumia taswira ya wanyama:
4. “Wanyonge,
Wamo shidani,
Digidigi na nyani,
Wamo makimbizoni,
Fisi wafurahia,
Ni sharia za mbuga?”

Katika shairi la “MUMIANI” linaonesha waziwazi unyonyaji unaofanywa na viongozi au watu wa tabaka la juu dhidi ya tabaka la chini ambao wanaishi vijijini na mijini, waendao hospitalini na wapelekwao mahakamani. Katika ubeti wa 1 tunaambiwa kuwa:-
1. “Mumiani,
Mijini,
Watembea kwa mato,
Kuzifanya kazi zao,
Kuzinyonya damu zetu,
Hawangoji,
Tulale.”

Diwani hii inaendelea kuonesha kuwa viongozi wabovu ni wasaliti na wanafiki. Viongozi hawa wanakuwa wepesi kuwaomba wananchi ili kufanikisha jambo fulani. Lakini pindi jambo hilo linapofanikishwa tu viongozi hao huwaweka wananchi pembeni (huwasaliti wananchi). Miongoni mwa mashairi yanayoonesha usaliti na unafiki wa viongozi wa dini na wa kisiasa ni “SIKULIWA SIKUZAMA” (uk.22-23), “WASO DHAMBI” (uk.1), “UASI” (uk.8), “PEPO BILA KIFO” (uk.14), vilevile shairi la “NAHODHA” (uk.41) linaonesha kuwa kuna viongozi wengi wanaoshindwa kazi lakini hawataki kuachilia madaraka. Hata hivyo msanii anaonesha kuwa viongozi wa aina hii wanaweza kuondolewa madarakani iwapo tu wananchi wote wataungana na kuwapiga vita.

KUPIGA VITA UKOLONI: Ukoloni ni hali ya kuvuka mipaka ya nchi na kwenda kuitawala nchi nyingine kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni. Kutokana na madhara yanayosababishwa na ukoloni, msanii ameona kuwa tusiukumbatie bali tuupige vita ili tuweze kuishi maisha mazuri ambayo huja baada ya kujitawala. Katika shairi la “NURU YA MATUMAINI” (uk.9-10) tunaambiwa kwamba wananchi wa kusini mwa Afrika walipiga vita ukoloni ili kuondokana na ubaguzi, dharau, ubwana na utwana na hatimaye kuishi katika mazingira ya haki na usawa.

Kwa vile ukoloni unamadhara, kama inavyooneshwa katika shairi hilo, wananchi hawanabudi kuacha tabia ya kuukaribisha tena. Katika shairi la “HATUKUBALI” (uk.30) linatuambia kuwa;
4. “Hatukubali tena,
Kutuletea usultani,
Kutuletea na ukoloni,
Kutuletea na uzayuni,
Hatukubali katu,
Ndani ya nchi yetu,
Iliyo huru.”

Mbali na kupiga vita ukoloni mkongwe bali tunajukumu la kuutokomeza ukoloni mamboleo ambao kwa kiasi kikubwa unachangia kutufanya masikini. Ukoloni mamboleo hutufanya tusiwe na kauli juu ya bidhaa tunazozalisha na hatimaye Taifa letu kuishia kwenye lindi la umasikini. Inaonesha kuwa ukoloni mamboleo hutufanya tutekeleze matakwa ya mataifa makubwa kwa lengo la kuwa nufaisha wao huku sisi tukibaki taabani. Haya tunayapata katika shairi la “HATUNA KAULI” (uk.8-9)
6. “Tumepewa yake mitaji,
Tuwe wasimamiaji,
Pia watekelezaji.”

Hali hii pia inajitokeza hata katika shairi la “WAFADHILI” (uk.38-39) ambapo tunaambiwa kuwa wafadhili hutupenda tu pale tunapokubali masharti yao na matakwa yao.


1. “Wafadhili kufurahishwa,
Ni sera zao kupitishwa,
Rais anaamrishwa,
Tekeleza!”

Hali hii hutufanya tuwe watumwa wa ukoloni mamboleo baada ya kuondokana na ukoloni mkongwe. Katika shairi la “BUNDI” (uk.43) tunaambiwa kuwa uhuru wetu tulioupata hatujaufaidi hata kidogo kutokana na kupigwa nyundo ya kichwa na ukoloni mamboleo. Ukoloni huu ambao umefanikishwa na Bundi, tunaambiwa kuwa uko nasi kila kukicha. Ukoloni mamboleo ni mfumo usio na usawa hata kidogo. Ni mfumo ambao unawafanya wanyonge waendelee kuwa masikini, wasiomithilika huku matajiri wakiendelea kuwa watu wenye mali kupindukia. Haya yote tunayapata katika shairi la “KLABU” (uk.50) juu ya ukoloni mamboleo kwa kutuasa tuchapekazi, tujenge viwanda, tuboreshe kilimo na ufugaji, tuinue elimu, kukuza uchumi na tupige vita rushwa.

UMASKINI, UJINGA NA MARADHI: Mwalimu Julius K. Nyerere aliwahi kusema kuwa, jamii yetu inakabiliwa na maadui wakuu watatu; Umasikini, Ujinga na Maradhi. Hali hii inajitokeza katika diwani hii kwani msanii anatuambia kuwa Bara la Afrika ni kama mgonjwa aliyemahututi katika shairi la “TIBA ISOTIBU” (uk.18) Hii ni kutokana na ujinga, umasikini na maradhi. Hali hii imekuwa ikisababisha njaa, vita, chuki na visasi vya kila aina na hivyo kufanya bara la Afrika lisiwe na amani kama ilivyo DRC, Sudani, Rwanda, Burundi, Tunisia nk. Mshairi anakereka sana na hali hii kwa kuhoji haya katika shairi la “AFRIKA” (uk.6-7)
1. “Lini
Afrika utakuwa,
Bustani ya amani,
Ukabila kuuzika,
Udini kuufyeka,
Ni lini?”

Kwa ujumla Bara la Afrika limejaa watu masikini ambapo umasikini wao unatokana na mambo mengi kama vile unyonyaji unaofanywa na viongozi wao kwa kushirikiana na nchi za nje. Lakini pia umasikini hutokana na ujinga yaani elimu ndogo. Hali hii pia tunaikuta katika mashairi ya “WASAKATONGE” (uk.5), “MVUJA JASHO” (uk.12-13), “WALALAHOI” (uk.36-37)

MSUGUANO WA KITABAKA NA KIITIKADI (MATABAKA): Katika diwani hii msanii anaonesha msuguano mkali wa kitabaka uliopo katika jamii na katika nchi masikini na nchi tajiri. Matabaka haya yote ni zao la maisha ya kitajiri na kimasikini katika jamii. Tunaambiwa kuwa katika msuguano huu mkali baina ya matabaka, tabaka masikini linajaribu kujifaragua ili lipate angalau tonge la ugali wakati tabaka tajiri likijaribu kunyang’anya tonge linalopiganiwa na tabaka masikini. Haya tunayapata katika shairi la “TONGE LA UGALI” (uk.20)
4. “Wanapigana
Wanaumizana,
Wanauwana,
Kwa tonge la ugali!”

Katika shairi la “WASAKATONGE” tunaambiwa kuwa wasakatonge na jua kali ni watu wa hali ya chini sana, wanaofanya kazi duni na ngumu na ndio waliowaweka madarakani viongozi wanaowanyonya na kuwanyanyasa. Wananchi hawa wana hali duni sana kutokana na kutothaminiwa na viongozi wao. Shairi la “WASAKATONGE” halinatofauti na mashairi ya “MVUJAJASHO” (uk.12) na “WALALAHOI” (uk.36-37) kwani yote yanazungumzia matatizo ya watu wa tabaka la chini yanayosababishwa na tabaka la juu. Katika shairi la “MIAMBA” (uk.29-30) na “MUMIANI” (uk.34) tunaona jinsi msongamano wa kitabaka unavyofanana na ule wa shairi la “TONGE LA UGALI.” Katika mashairi haya, wenye nguvu ndio hutawala na kuwanyonya wanyonge kama inavyojishihirisha katika shairi la “MIAMBA” ambalo limetumia taswira ya wanyama katika kuonesha matabaka hayo, kama msanii anavyosema:


1. “Miamba,
Chui na Simba,
Mbugani wanatamba,
Vinyama vinayumba,
Chakula cha wakubwa
Ni sharia za mbuga?”

Hali ilivyo katika jamii yetu haina tofauti na ile ya mataifa tajiri na mataifa masikini, tunaendelea kuambiwa kuwa, mataifa masikini hayana chao mbele ya mataifa tajiri. Kazi ya mataifa masikini ni kutengeneza mipango ya mataifa tajiri kama inavyojionesha katika shairi la “HATUNA KAULI” (uk.8-9)
4. “Maagizo tunapewa,
Mipango tunapangiwa,
Na amri tunapangiwa.”

Mashairi mengine yanayoonesha hali hii ni “WAFADHILIWA” (uk.38) na “KLABU” (uk.50-51). Pamoja na masuluhisho yanayotolewa dhidi ya hali hii kama vile tabaka masikini kuungana na kupambana na hali hii, hasa kati ya nchi lakini bado msanii anawasiwasi juu ya kuondoka kwa hali hii katika jamii yetu. Hii inatokana na maswali anayojiuliza katika mashairi ya “TONGE LA UGALI” na “WASAKATONGE” ambapo msanii anaonesha hali ya kutokuwa na jibu rahisi katika kukomesha hali hiyo.

Pia msanii huyu amedokeza kuhusu mgongano au msuguano wa kiitikadi. Katika diwani hii tunaoneshwa kuwa, hatuna itikadi ya kisiasa inayoeleweka. Tupo kama hatupo na hatuelewi kama bado sisi ni wajamaa au mabepari. Hii inajidhihirisha katika shairi la “TWENDE WAPI” (uk.20-21)


3. “Twende wapi?
Mashariki “siko”!
Magharibi “siko”!
Wapi tuendako?
Tunatapatapa!”

Kutapatapa kiitikadi kunatusababishia tufanye mambo kama vipofu na matokeo yake ni kudaka kila kitu iwe kinachotoka magharibi au mashariki na hivyo kuathiri mfumo mzima wa maisha yetu ikiwemo mmomonyoko wa kimaadili.

UNAFIKI: Katika diwani hii tunaambiwa kuwa baadhi yetu hasa wanasiasa, viongozi au wananchi ni wanafiki wakubwa. Kwani kitendo cha baadhi ya watu kujiona kuwa hawana dhambi ni cha kinafiki kwa sababu, hakuna mwanadamu asiye na dhambi kama shairi la “WASODHAMBI” (uk.1) linavyosema;


2. Wavilemba!
Wavilemba, na majoho, tasibihi,
Wajigamba, safi ni roho, ni kebehe,
Wanotenda,
Unafiki.

Pia hata katika la “MAMA NTILIYE” (uk.17) nalo linadhibitisha hilo.


2. “Majungu na makaango, jinsi unavyoyapika,
Na kibwebwe kiachiye, au utaadhirika,
Kazi hiyo isusiye, hasara sijekufika.”

Diwani hii inaendelea kuonesha unafiki wa watu wa dini kupitia shairi la “UASI” (uk.8) Watu hawa hujidai mbele za watu ni waongofu wakati ni wachafu na wadhaifu katika matendo yao. Hawa ni watu wanaokashifu dini za wenzao kwa kudai kuwa zao ndizo safi na sahihi. Shairi linasema:


“Uasi
Masheikh na masharifu,
Mapadri na maaskofu,
Kauli zao nadhifu,
Hujigamba waongofu,
Wengi wao ni wachafu,
Wenye vitendo dhaifu,
Dini wanazikashifu,
Wanafiki.”

Unafiki wa baadhi ya watu unaendelea kuoneshwa kwenye shairi la “PEPO BILA KIFO” (uk.14) ambapo baadhi yatu hupenda vitu fulani fulani bila kufuata kanuni za upatikanaji wa vitu hivyo. Kitendo cha mtu kupenda pepo bila kuonja mauti ni cha kinafiki. Vilevile kitendo cha kupenda starehe za wanawake ni cha kinafiki kwani peponi si mahali pa kufanyia umalaya bali ni mahali patakatifu. Hivyo afikiriaye mambo haya ni mnafiki kwani hajui neno la Mungu linasemaje kuhusu pepo. Katika kuonesha unafiki shairi hili linasema:


5. “Nibembee na hurulaini,
Wanawake wazuri wa shani,
Wawashindao wa duniani,
Nipumbazike.”

Unafiki mwingine unajionesha katika siasa ambapo baadhi ya viongozi hupata uongozi kwa kujipendekeza na kutoa maneno ya hapa na pale kwa wale wanawapatia hivyo vyeo. Haya tunayapata katika shairi la “WARAMBA NYAYO” (uk.46-47)


1. ‘Wajikomba,
Ili kupata vyeo,
Na uluwa.”

USALITI: Mshairi Mohammed Seif Khatibu ameonesha suala la usaliti katika diwani hii ya WASAKATONGE, kwani tunaambiwa kuwa, mara nyingi tunakuwa pamoja katika safari ya kutafuta kitu fulani lakini pindi kinapopatikana tu tunawatenga baadhi ya watafutaji wenzetu. Haya yanadhihirishwa wazi katika shairi la “SIKULIWA SIKUZAMA” (uk.22-23) ambapo msanii anabainisha kwa kusema kuwa;


1. “Nilitoswa baharini,
Ya dharuba na tufani,
Walitaka nizame,
Wao wanitazame,
Nife maji wakiona,
Waangue na vicheko,
Na kushangilia,
Ushindi wao!”

Usaliti wa aina hii unajitokeza tena katika shairi la “ASALI LIPOTOJA” (uk.37-38), Shairi hili linaweza kufananishwa na hekaheka za kupigania uhuru ambapo baada ya kupata uhuru baadhi ya watu walioshiriki katika kuutafuta uhuru huo, walitengwa kabisa. Lakini pia matunda yaliyotegemewa baada ya uhuru hayajapatikana kwa wote bali kwa watu wachache tu wenye mirija mirefu (viongozi) kama lisemavyo shairi hili:


2. “Mili ikatuvimba,
Ila hatukuyumba,
Tukabakia shambani,
Kutumaini kwamba,
Faida itawamba,
Heri itafika.”


3. “Asali lipotoja,
Wengi walikuja,
Na mirefu mirija,
Kwao kawa tafrija,
Wakapata faraja,
Sisi tukatengwa.”

Katika shairi la “VINYONGA” (uk.49) tunabaini pia usaliti wa wanasiasa kwa wananchi. Shairi hili linaonesha kuwa wanasiasa wanatenda mambo kinyume na maadili na hivyo kuwasaliti wananchi waliowaweka madarakani. Viongozi hawa hawatekelezi yale wanayoahidi kwa wananchi wao badala yake wanatumia nafasi walizo nazo katika kujitajirisha wao wenyewe. Shairi linasema;


2. “Jukwaa,
Meingiliwa,
Wanasiasa vinyonga,
Maisha ya ufahari,
Kauli zao nzuri,
Vitendo vyao hatari,
Ni kinyume na maadili,
Ni usaliti.”

Usaliti mwingine umejitokeza katika mapenzi. Mshairi anasema kuwa alikesha kwa ajili ya kumsubiri wake mahaba, ili baadaye wawe wawili. Hata hivyo mkesha wake haukuzaa matunda kwani mwenzie alimsaliti kwa kutofika katika eneo la tukio kama anavyoonesha katika shairi la “NILIKESHA” (uk.23-24)


4. “Nilikesha,
Na kulikucha sikukuona,
Nathibitisha wako uungwana,
Kosa langu kukupenda sana,
Hustahiki heshima hiyo,
Sisahau sikusamehe,
Nilikesha.”

Pia katika shairi la “SIKUJUA” (uk.28) linaonesha usaliti wa baadhi ya watu. Msanii anasema kuwa, aliyemfuga kwa mategemeo ya kumsaidia mambo mbalimbali amegeuka na kufanya kinyume na mategemeo au makubaliano. Msanii anadhihirisha hili kwa kusema;
4 “Kumbe nimefuga punda, mashuzi ndio heshima,
Ni ukaidi wa inda, mateke kurusha nyuma,
Nyama limekuwa nunda, mfugaji humuuma.”

MAPENZI/MAHABA: Miongoni mwa dhamira ambazo zimezungumziwa kwa kina katika diwani hii ni Mapenzi. Mshairi huyu anaonesha kuwa, mapenzi yana raha yake na pindi yanapokwenda mrama huleta karaha kubwa kwa mtu mmoja au wawili waliofarakana. Mshairi anasema kuwa mapenzi ni kitu muhimu sana kwake na yupo tayari kuitwa jina lolote lile kwa sababu ya kuyathamini mapenzi. Haya tunayapata kupitia shairi la “MAHABA” (uk.1-2)


4. Kama mahaba wazimu, sihitaji nitibiwe,
Bora niwe chakaramu, nipigae watu mawe,
Kuwa kwangu mahamumu, wewe isikusumbuwe,
Dawa yangu siyo ngumu, mimi nipendwe na wewe.

Kwa vile mshairi huyu anaona kuwa mapenzi ndicho kitu cha thamani kubwa kwake ayakosapo au amkosapo yule ampendaye hukonda na kudhoofika mwili kama asemavyo katika shairi la “SILI NIKASHIBA” (uk.17)


2. “Sili nikashiba, nikikukumbuka,
Hula haba, na kushikashika,
Ni chozi za huba, kweli nasumbuka.

Hali ya kupenda kwa dhati inajitokeza katika shairi la “NILIKESHA” (uk.23-24) ambapo mtu anaamua kukesha kwa kusubiri ahadi ya huba ingawa apendwaye huenda hayuko tayari kupenda. Shairi hili linasema;


1. “Nilikesha,
Si kwa ibada au shakawa,
Sio kwa ngoma ama takuwa,
Ila kwa hamu na nyingi hawa,
Ikawa hakupambazuki,
Ni mtekwa wa huba zako.”
Nilikesha.

Katika mashairi ya “USIKU WA KIZA” (uk.27-28) na “MACHOZI YA DHIKI” (uk.28) yanaendelea kuzungumzia hali hiyo ya mapenzi. Katika shairi la “USIKU WA KIZA” tunaoneshwa majonzi ya mpenzi mmoja aliyeondokewa na kipenzi chake. Kutoweka kwa mahabuba wake kunamfanya asile na kushiba kama shairi linavyosema;


2. “Meniondokeya, wangu mahabuba,
Nilikuzoweya, kwa yako mahaba,
Nnajikondeya, sili nikashiba.”

Vilevile katika Shairia la “MACHOZI YA DHIKI” (uk.28) mpenda anabubujikwa machozi kwa kuadimikiwa na wake mahabuba, yaani anateseka kutokana na kuadimika kwa mpenzi wake.

Mshairi anaendelea kutetea mapenzi ya dhati katika shairi la “PEPO TAMU” (uk.35) ambapo anasema kuwa penzi tamu ni penzi lililojaa raha na lina ladha kushinda asali. Pendo tamu hufukuza uchoyo uheka.


4 “Pendo lenye tabasamu, za dhati si za uheka,
Na nyoyo za ukarimu, uchoyo ni sumu yake,
Haliishi yake hamu, hupendi imalizike.”

Kwa kuwa mpendwa anaonesha pendo la dhati, apendwaye pia anatakiwa aoneshe pendo lake kwa kutoa kauli kuhusu kupenda au kutopenda kwake kwa yule anayemtaka. Hii ni katika shairi la “ITOE KAULI YAKO” (uk.27)


1. “Itoe yako sauti, kama, kweli wanipenda,
Niweze kujizatiti, moyo uondoke funda,
Nizidi kukudhibiti, sikuache hata nyanda.”

Shairi hilo linataka mpendwa atoe kauli yake kwani mpenda ameshatoa kauli yake ya upendo kama asemavyo katika shairi la “WEWE WAJUA” (uk.25)


1. “Nakupenda, nawe wajua,
Tusitupane,
Tupendane,
Kwa salama.”

Hali hii pia inajitokeza katika shairi la “NAKUSABILIYA” (uk.23) ambapo msanii anatoa pendo lake lote kwa yule ampendaye kama asemavyo katika ubeti wa kwanza;


1. “Nakusabiliya, pendo lote kwako,
Litaseleleya, litabaki kwako,
Sitaliachiya, kwenda kwa mwenzako.”

Kama apendwaye ataonesha pendo la dhati kwa yule ampendaye basi watalindana na kulifanya pendo lao kuwa la wawili tu kama lisemavyo shairi la “NILINDE” (uk.15)


1. Nilinde sichukuliwe, hata kwa moja shubiri,
Tubaki mimi na wewe, pendo letu linawiri,
Tuwazidishe kiwewe, wasotutakia heri.

Pia hali kama hii itasaidia kudumisha penzi lao milele na milele watabaki wawili peke yao huku wakifurahia pendo lao maridhawa. Haya tunayapata katika shairi la “TUTABAKI WAWILI” (uk.26) na “YEYE NA MIMI” (uk.39). Katika shairi la “TUTABAKI WAWILI”, tunaambiwa kuwa;


2. Hakuna wa kulizima, pendo langu kufifiya,
Litabakia daima, na kwako kuseleleya,
Hadi siku ya kiyama, pendo litaendelea,

Shairi la “YEYE NA MIMI” linadai kuwa penzi tamu na dhati huwafanya watu wawili wapendanao wakeshe katika mapenzi bila kuchoka

4. “Yeye na mimi wawili, hatuna tunobakisha,
Humsabilia mwili, hana anapobakisha,
Ana mahaba ya kweli, usiku kucha hukesha.”

Katika diwani hii tunaambiwa kuwa kama unampenda mtu asiyekupenda basi usimchukui isipokuwa muagane kwa wema pale inapobidi kama inavyojionesha katika shairi la “KWA HERI” (uk.29)


3. Ingawa menisusia kujipa kunigomeya,
Mvua hunyesha masika, masika hukesha,
Hakuna ukame,
Kwa heri.

Diwani hii inaonesha kuwa kukataliwa kimapenzi si mwisho wa dunia bali ni njia mojawapo ya kufunguliwa mlango kwa wengine hasa yule akupendaye kwa dhati. Haya yote tunayapata katika shairi la “NILICHELEWA KUPENDA” (uk.41)


1. Katika uhai wangu, nilichelewa kupendwa,
Waliowakija kwangu, wale wa kunizuzuwa,
Mwaka huu mwaka wangu, nami nimejaaliwa.

Kwa upande wa pili msanii anakemea mapenzi ya sio ya dhati (ulaghai) kutokana na kutokuwa na faida yoyote kwa mtu na kwa jamii kwa ujumla. Mapenzi ya namna hii tunayapata katika shairi la “SI WEWE” (uk.21-22) ambapo msanii anahoji na kumsuta mtu aliyempenda kwa chati. Mapenzi haya hayana faida yoyote isipokuwa mateso makali kwa mhusika au wahusika;



4. Umeshapwelewa baharini,
Wako werevu umekwisha,
Sasa unatweta,
U taabani,
Ni wewe ulo mlafi,
Si wewe?

Msanii anaendelea kusema mapenzi ya chati katika shairi la “WEWE JIKO LA SHAMBA” (uk.44) Hapa msanii anakemea tabia ya watu wanaofanya mapenzi kiholela kuwa waachane na tabia hiyo kwani haina faida isipokuwa karaha na kusutwa. Anaendelea kuwaambia kuwa;

4 Takula wako ujuvi, na mwingi uhayawani,
Upikavyo haviivi, ni vibichi sahanini,
Vitachacha hivihivi, kuozea mikononi.

Watu wa aina hii sharti wajitakase ili wakubalike katika jamii yaani “wayapangue mafiga, jiko halitaivisha” wasipofanya hivyo, hawatapata kitu chochote cha maana kwani wapenzi (wawezeshaji) wamekuwa wengi. Shairi la “BUZI LISILOCHUNIKA” (uk.45)

4 Msumeno utafute, na makali kuyaweka,
Ukwereze na uvute, na watu kukusanyika,
Na hutafika popote, buzi halitachunika.

Kwa ujumla msanii anazungumzia mapenzi ya aina mbili, mapenzi ya dhati ambayo kwake ndio ngao na mapenzi ya chati ambayo huleta karaha tupu katika maisha ya mwanadamu.




Swali.


Soma makala ya M.M.Mlokozi katika jarida la mulika (1989) namba 21 kisha jadili vigezo alivyovitumia katika kugawa tanzu na vipera vya Fasihi Simulizi.

DONDOO:

UTANGULIZI:

Maana ya Fasihi Simulizi

Maana ya tanzu

Maana ya vipera

KIINI:

Kuchambua vigezo alivyotumia Mulokozi katika kugawanya tanzu na vipera vya Fasihi Simulizi.

Kwa mujibu wa Mulokozi katika Mulika namba 21, (1989). Pamoja na kwamba Fasihi ni kongwe lakini kitaaluma bado ni changa kwa sababu ilianza kuchungunzwa hivi karibuni. Hivyo imepelekea kutokuwepo kwa nadharia, marejeo, wala istilahi zenye kutosheleza mahitaji ya taaluma hiyo. Tatizo hili linadhihirika pale tunapoangalia kazi za wataalamu mbalimbali kuhusu tanzu za Fasihi Simulizi. Kwa upande wa nadharia kitabu pekee kinachozijadili tanzu za Fasihi Simulizi kwa urefu ni kitabu cha Ruth Fennegan kinachoitwa Oral Literature in Africa (1970). Kwa upande wa Kiswahili hakuna kitabu kinachojadili uwanja wa tanzu za Fasihi Simulizi. Badala yake kunamiongozo michache kwa ajili ya shule za sekondari kama vile Balisidya, N (1975) na Taasisi ya Elimu (1987)

Mulika namba 21 ni jarida la kitaaluma linalotoa fursa kwa wataalamu, waalimu na wanafunzi katika kujadili mada mbalimbali za kiswahili. Jarida hili lililoandikwa mwaka 1989 ndani yake kuna makala ya Fasihi Simulizi inayohusu tanzu za Fasihi Simulizi na vipera vyake iliyoandikwa na M.M.Mulokozi.

Hivyo basi kutokana na kukosekana kwa nadharia zinazoongoza ugawaji wa tanzu za Fasihi Simulizi ya Kiswahili wataalamu wengi wamekuwa wakitumia vigezo mbalimbali ambavyo ni maudhui, fani, matukio, idadi ya waimbaji, vifaa vinavyotumika na namna ya uimbaji.

Fasihisi Simulizi imejadiliwa na wataalamu mbalimbali miongoni mwa waalamu hao ni M.M.Mulokozi (1996) anasema Fasihi Simulizi ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi.

TUKI (2004) Fasihi Simulizi ni kazi ya fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo kama vile; hadithi, ngoma na vitendawili.

Hivyo basi Fasihi Simulizi ni fasihi inayotokana na maneno ambayo huzungumzwa, hutolewa au kuimbwa ambapo mtungaji na mwasilishaji hutumia sanaa.

Tanzu ni istilahi inayotumiwa kuelezea au kurejelea aina ya kazi mbalimbali za kifasihi. Inawezekana utanzu mkuu kuwa na vitanzu vingine mbalimbali kwa mfano, tanzu kuu za kifasihi ni Riwaya, Tamthilia, Shahiri, Novela, Insha na Hadithi (Wamitila (2003).

Vipera ni dhana inayotumiwa kuelezea vijitanzu katika fasihi hasa fasihi simulizi. Mfano: semi methali, mafumbo, vitendawili nakadhalika. (Wamitila 2003)

M.M.Mulokozi katika makala yake ya tanzu za Fasihi Simulizi iliyo katika jarida la Muulika namba 21(1989) amezigawa tanzu na vipera vya Fasihi Simulizi kwa kutumia vigezo viwili ambavyo ni,kigezo cha kwanza ni umbile na tabia ya kazi inayohusika na kigezo cha pili ni muktadha na namna ya uwasilishaji wake kwa hadhira.

Umbile na tabia ya kazi inayohusika: katika kigezo hiki Mulokozi ameangalia vipengele vya ndani vinavyoiumba sanaa hiyo na kuipa muelekeo au mwenendo. Baadhi ya vipengele hivyo vya ndani ni namna lugha inavyotumika (kishahiri, kinathari, kimafumbo, kiwimbo na kighani), muundo wa fani hiyo na wahusika. Kwa upande wa muktadha na namna ya uwasilishaji amezingatia kuwa, Fasihi Simulizi ni tukio hivyo huambatana na muingiliano wa mambo matatu ambayo ni muktadha, watu na mahali. Mwingiliano huu ndio unaotupa muktadha na muktadha ndio unaoamua fani fulani ya Fasihi Simulizi ichukue umbo lipi, iwasilishwe vipi kwa hadhira, kwenye wakati na mahali hapo. Hivyo hadithi inaweza kugeuzwa wimbo, utendi unaweza kuwa hadithi na wimbo unaweza kugeuzwa ghani au usemi kutegemea muktadha unaohusika (Mulokozi 1989).

Kwa hiyo kwa kutumia vigezo hivi, Mulokozi amezigawa tanzu na vipera vya Fasihi Simulizi kama ifuatavyo;

Masimulizi; hii ni tanzu ya Fasihi Simulizi yenye kusimulia habari fulani. Katika kugawa utanzu huu vigezo vilivyotumika ni pamoja na kigezo cha lugha ambapo lugha inayotumika katika masimulizi ni ya kinathari. Pia kigezo kingine ni kigezo cha muundo, mara nyingi masimulizi huwa na muundo unaojitofautisha na tanzu nyingine kama vile ushairi. Katika masimulizi muundo wake mara nyingi huwa wa moja kwa moja yaani mtiririko wa visa na matukio. Vilevile kigezo kingine ni kigezo cha wahusika ambapo katika kigezo hiki huhusisha wahusika wa pande mbili ambao ni mtendaji na watendwaji. Pia kigezo kingine ni kigezo cha namna ya uwasilishaji. Katika uwasilishwaji huwasilishwa na msimuliaji mbele ya hadhira. Kigezo kingine ni kigezo cha mandhari ambayo huwa maaluma kama vile chini ya mti mkubwa na uwanjani. Masimulizi pia hufanyika katika muda maalum. Mfano, baada ya kazi.

Masimulizi yamegawanyika katika tanzu kuu mbili ambazo ni tanzu za kihadithi (za kubuni) na tanzu za kisalua (kihisitoria). Tanzu za kihadithi zina kipera kimoja ambacho ni ngano. Ngano (vigano/hurafa), hizi ni hadithi za kimapokeo zitumiazo wahusika kama wanyama, miti na watu kuelezea na kuonya kuhusu maisha. Vigezo vilivyotumika katika kugawa ngano ni kigezo cha lugha ambayo ni lugha ya kinathari, kigezo cha dhima ambacho huelezea au kuonya kuhusu maisha na kufurahisha. Kigezo kingine kilichotumika ni kigezo cha wahusika ambao ni wanyama, miti na watu. Kipera hiki cha ngano kinajumuisha vijipera vifuatavyo ambavyo ni istiara, mbazi na kisa.

Istiara; hii ni hadithi ambayo maana yake ya wazi inawakilisha maana nyingine iliyofichika. Vigezo vilivyotumika katika kugawa kipera hiki ni kigezo cha lugha ambayo ni lugha ya mafumbo.

Mbazi; hii ni hadithi fupi yenye mafunzo itolewayo kama kielelezo wakati wa maongezi au kumkanya mtu. Kigezo kilichotumika katika kugawa kipera hiki ni kigezo cha dhima.

Kisa; hii ni hadithi fupi ya kufurahisha kuhusu tukio la kweli. Kigezo kilichotumika ni kigezo cha kidhima.

Utanzu mwingine wa masimulizi ni utanzu wa kisalua. Utanzu huu umegawanyika katika vipera vifuatavyo ambavyo ni visakale, mapisi, tarihi, kumbukumbu na visasili.

Visakale; haya ni masimulizi ya mapokeo juu ya wahenga au mashujaa wa kabila au taifa yenye kuchanganya chuku na historia (kama hadithi ya Liyongo). Vigezo vilivyuotumika hapa ni kigezo cha wahusika ambao wapo katika historia yaani mashujaa fulani. Kigezo kingine ni fani ya ubunifu.

Mapisi; haya ni maelezo ya kihistoria bila kutia mambo ya kubuni. Hapa pia kigezo kilichotumika ni kigezo cha dhima ambacho huelezea mambo ya kihistoria yaliyo ya kweli.

Tarihi; haya ni maelezo au jedwali la matukio muhimu na tarehe zake. Kigezo kilichotumika hapa ni kigezo cha kidhima ambacho ni kuelezea matukio muhimu na tarehe zake. Pia kigezo kingine ni namna ya uwasilishaji ambapo huwasilishwa kwa kutumia jedwali na lugha yake huwa katika maandishi.

Kumbukumbu; haya ni maelezo ya matukio muhimu yanayomuhusu mtu binafsi au jamii ya watu. Hapa kimetumika kigezo cha fani, ambayo ni fani za wasifu na tawasifu. Pia kigezo kingine ni kigezo cha wahusika ambao ni watu.

Visasili; hiki ni kipera kinachofungamana na imani za dini na mizungu ya kajamii pia hizi ni hadithi za kale zenye kuwakilisha imani na mtazamo wa jamii inayohusika kuhusu asili ya ulimwengu na maisha yao. Kigezo kilichotumika ni kigezo cha kidhima ambacho huelezea shabaha ya maisha.

Utanzu mwingine wa Fasihi Simulizi ni utanzu wa Semi. Semi ni tungo au kauli fupi fupi za kisanaa zenye kubeba maana au mafunzo. Kigezo kilichotumika katika kugawa utanzu huu ni kigezo cha lugha ambayo ni lugha ya mkato. Kigezo kingine ni kigezo cha kidhima ambacho ni kufunza.

Utanzu huu umegawanyika katika vipera vifuatavyo ambavyo ni methali, vitendawili, misimu, mafumbo na lakabu.

Methali ni semi fupi fupi zenye kueleza kwa mukhtasari fikra au mafunzo mazito yaliyotokana na uzoefu wa kijamii. Vigezo vilivyotumika katika kipera hiki ni kigezo cha lugha ambayo ni lugha ya mafumbo. Vilevile kimetumika kigezo cha muundo ambapo methali huundwa na muundo wa pande mbili ambazo hutegemeana.

Vitendawili; huu ni usemi uliofumbwa ambao hutolewa kwa hadhira ili ufumbuliwe. Vigezo vilivyotumika ni kigezo cha lugha. Hapa lugha inayotumika ni lugha ya kimafumbo.

Misimu; ni semi za muda na mahali maalum ambazo huzuka na kutoweka kutegemea mazingira maalum. Hivyo vigezo vilivyotumika katika kugawa kipera hiki ni kigezo cha muktadha yaani hutokea wakati maalum na mazingira maalum.

Mafumbo; ni semi za maonyo au mawaidha ambazo maana zake za ndani zimefichika. Kigezo kilichotumika ni kigezo cha kidhima ambacho ni kuonya pamoja na kigezo cha lugha ambayo ni lugha ya mafumbo.

Lakabu; haya ni majina ya kupanga ambayo baadhi ya watu hupewa au hujipatia kutokana na sifa zao za kimwili, kinasaba, kitabia au kimatendo. Kigezo kilicho tumika katika kipera hiki ni kigezo cha lugha ambayo lugha iliyotumika ni lugha kificho yaani maana yake hufichwa.

Utanzu mwingine wa Fasihi Simulizi ni ushairi. Huu ni utanzu wa fasihi simulizi unaowasilishwa kwa hadhira kwa njia ya uimbaji au ughani badala ya usemaji wa kawaida. Vigezo vilivyotumika katika kugawa utanzu huu ni kigezo cha lugha ambayo ni lugha ya kishairi. Pia kimetumika kigezo cha fani ambapo fani inayotumika ni wizani, lugha ya mkato, lugha ya mafumbo na uimbaji au ughani.

Katika utanzu huu kuna vipera viwili ambavyo ni nyimbo na maghani;

Nyimbo ni kila kinachoimbwa. Vigezo vilivyotumika katika kipera hiki cha ushairi ni kigezo cha fani ambapo huangalia muziki wa sauti ya muimbaji au waimbaji, muziki wa ala (kama ipo), matini au maneno yanayoimbwa. Pia kuna kigezo cha muktadha ambacho huzingatia hadhira inayoimbiwa na muktadha unaofungamana na wimbo huo, kwa mfano sherehe, ibada, kilio nakadhalika. Kwa vigezo hivi utanzu wa nyimbo umegawanyika katika vijipera vifuatavyo ambavyo ni, tumbuizo, bembea, kongozi, nyimbo za dini, wawe, tenzi, tendi, mbolezi, kimai, nyiso, nyimbo za vita, nyimbo za uwindaji, nyimbo za taifa, nyimbo za watoto na nyimbo za kazi.

Tumbuizo; hizi ni nyimbo za furaha ziimbwazo kuwafurahisha watu kwenye matukio mbalimbali kama vile ngomani au harusini. Vigezo vilivyotumika hapa ni kigezo cha kidhima ambacho hulenga kuwafurahisha watu, pia kigezo kingine ni kigezo cha kimuktadha ambapo huwasilishwa katika matukio yanayoendana na dhima ya kufurahisha.

Bembea; hizi ni nyimbo za kubembeleza watoto. Kigezo kilichotumika hapa ni kigezo cha kidhima ambapo hulenga kubembeleza watoto.

Kongozi; hizi ni nyimbo za kuaga mwaka. Vigezo vilivyotumika hapa ni kigezo cha kidhima ambapo dhima yake ni kuaga mwaka na kigezo cha kimuktadha ambapo muktadha wake ni muktadha maalum yaani huimbwa mwishoni mwa mwaka.

Nyimbo za dini; hizi ni nyimbo zinazoimbwa kwa lengo la kumsifu Mungu au miungu. Vigezo vilivyotumika ni kigezo cha kidhima ambapo dhima yake ni kumsifu Mungu au miungu, pia kimetumika kigezo cha kimuktadha ambapo huimbwa katika muktadha wa kidini.

Wawe; hizi ni nyimbo za kilimo. Vigezo vilivyotumika ni kigezo cha kimuktadha ambapo huuimbwa wakati wa kulima, pia kigezo cha kidhima kimetumika ambapo dhima yake ni kuchapusha kazi.

Tenzi; hizi ni nyimbo ndefu za kimasimulizi au mawaidha. Kigezo kilichotumika ni kigezo cha kifani ambapo fani yake ni masimulizi au mawaidha.

Tendi; hizi ni nyimbo ndefu za masimulizi juu ya matendo ya mashujaa. Vigezo vilivyotumika hapa ni kigezo cha kifani ambapo wahusika wa tendi ni watu wenye historia za matendo ya kishujaa, pia kigezo cha lugha kimetumika ambapo lugha yake ni ya kinathari.

Mbolezi; hizi ni nyimbo za kilio au maombolezo. Vigezo vilivyotumika katika kugawa kipera hiki ni kigezo cha kimuktadha ambapo huwasilishwa katika muktadha wa maombolezo au kilioni/msibani, pia kimetumika kigezo cha kidhima ambapo dhima yake ni kuomboleza.

Kimai; hizi ni nyimbo zihusuzo shughuli za baharini. Vigezo vilivyotumika hapa ni kigezo cha kidhima ambapo dhima yake ni kuchapusha kazi. Vilevile katika kigezo cha kimuktadha kimai huwasilishwa katika mazingira ya baharini.

Nyiso; hizi ni nyimbo za jandoni. Vigezo vilivyotumika ni kigezo cha kidhima ambapo dhima yake ni kutoa mafunzo kwa vijana kuhusu maisha ya utu uzima. Kigezo kingine ni kigezo cha kimuktadha ambapo nyiso huwasilishwa katika mazingira maalumu, kama vile porini nakadhalika.

Nyimbo za vita; hizi ni nyimbo ziimbwazo na askari wakati wa vita. Vigezo vilivyotumika katika kugawa kipera hiki ni kigezo cha kimuktadha ambapo muktadha wake huwa ni wakati wa vita, na kigezo kingine ni kigezo cha wahusika au waimbaji ambapo waimbaji wake huwa ni maaskari.

Nyimbo za watoto, hizi ni nyimbo waimbazo watoto wakati wa michezo yao. Vigezo vilivyotumika ni pamoja na kigezo cha kimuktadha ambapo huwasilishwa wakati wa michezo ya watoto. Kigezo kingine ni kigezo cha wahusika au waimbaji ambapo waimbaji wake huwa ni watoto.

Nyimbo za uwindaji; hizi ni nyimbo ambazo huimbwa na makundi ya wawindaji wakati wa shughuli au sherehe zao. Vigezo vilivyotumika hapa ni kigezo cha wahusika au waimbaji ambapo huimbwa na wawindaji na kigezo kingine ni kigezo cha kimuktadha ambapo huwasilishwa wakati wa shughuli au sherehe za uwindaji.

Nyimbo za Taifa; hizi ni nyimbo za kisifia Taifa au kabila. Kigezo kilichotumika hapa ni kigezo cha kidhima ambapo dhima yake ni kusifia Taifa au kabila.

Nyimbo za kazi; hizi ni nyimbo zinazoimbwa katika shughuli mbalimbali kama vile, kulima, kutwanga, kusuka, uvuvi, uashi, useremala na kadhalika. Vigezo vilivyotumika hapa ni kigezo cha muktadha wa uwasilishaji ambapo huwasilishwa kulingana na shughali maalumu. Pia kigezo kingine ni kigezo cha kidhima ambapo dhima ya nyimbo za kazi ni kuchapusha kazi.

Maghani; hiki ni kipera cha ushairi kinachotolewa kwa kalima badala ya kuimbwa. Kwa mujibu wa Wamitila (2003) maghani ni istilahi inayotumiwa kuelezea aina ya ushairi ambao hutolewa kwa kalima au maneno badala ya kuimbwa. Vigezo vilivyotumika katika kugawa utanzu huu ni lugha ambayo ni lugha ya kishairi. Pia ametumia kigezo cha wahusika ambapo wahusika wakuu ni binadamu. Hivyo vigezo hivi ndivyo vilivyopelekea utanzu huu kuwekwa kwenye utanzu wa ushairi.

Kipera hiki kina vijipera vitatu ambavyo ni maghani ya kawaida, sifo na maghani masimulizi. Maghani ya kawaida ni kundi ambalo tunaweza kuingiza fani mbalimbali za ushahiri simulizi kama vile ushairi wa mapenzi, siasa, maombolezo, kazi, dini ilimradi unaghanwa katika namna ya uwasilishwaji wake.

Sifo; hizi ni tungo za kusifu ambazo husifu watu, wanyama na mimea. Baadhi ya sifo huwa zinakashifu au kukejeli. Vigezo vilivyotumika katika kugawa kipera hiki ni kigezo cha wahusika, wahusika wake wakuu ni binadamu wanyama au mimea. Kigezo kingine ni muktadha ambao huelezea matukio yaliyopita au yaliyopo. Sifo huwa na tanzu muhimu kama vile vivugo (majigambo), pembezi na tondozi.

Kivugo; hili ni ghani la kujisifia, hutungwa na kughanwa na muhusika mwenyewe. Vigezo vilivyotumika katika kugawa kijipera hiki cha sifo ni lugha, katika lugha zimetumika mbinu kama vile sitiari, mkato, vidokezo, ishara, takriri na vina. Kigezo kingine ni kigezo cha wahusika ambapo wahusika wake wakuu ni binadamu pia kimetumika kigezo cha muktadha ambapo muktadha wake hufungamana na tukio maalum katika maisha ya muhusika, mfano vitani. Vilevile katika kigezo cha uwasilishaji huweza kuwa na masimulizi ndani yake. Muundo wake hutegemea shabaha za mtunzi na jadi ya utunzi anayoiwakilisha hakiandikwi na kutungwa papo kwa papo.

Tondozi; hizi ni tungo za kusifu watu, wanyama au vitu. (Pembezi pia ni aina ya tondozi ambayo imekusudiwa watu wa aina fulani tu). Vigezo vilivyotumika katika kugawa kipera hiki ni kigezo cha wahusika ambao ni wanyama na mimea. Mfano wa wanyama ni kama vile Simba. Kigezo kingine ni lugha ambayo ni lugha ya kishairi.

Ghani masimulizi: hizi ni ghani ambazo hutambwa ili kusimulia hadithi, historia au tukio fulani. Vigezo vilivyotumika kugawa kipera hiki ni pamoja na kigezo cha lugha, lugha inayotumika katika kijipera hiki ni lugha ya kishairi na fani iliyotumika ni kusimulia hadithi/tukio kwa kirefu. Vile vile kuna kigezo cha namna ya uwasilishaji huambatana na ala za muziki mfano zeze na marimba.

Ghani masimulizi ina vipera vinne ambavyo ni rara, ngano, sifo na tendi.

Rara ni hadithi fupi nyepesi ya kishairi yenye visa vya kusisimua, vigezo vilivyotumika katika kugawa kipera hiki ni pamoja na lugha inayotumika, lugha inayotumika katika kipera hiki ni lugha ya kishairi, fani iliyotumika ni fani ya kihadithi ambayo ni hadithi fupi, nyepesi na inavisa vya kusisimua na kigezo kingine ni muktadha wa uwasilishaji ambapo huimbwa au kughanwa ikiambatana na ala za muziki.

Ngano; hizi ni hadithi za mapokeo zitumiazo wahusika kama wanyama, miti na watu katika kuelezea au kuonya kuhusu maisha. Katika kipera hiki kigezo kilichotumika ni muktadha wa uwasilishaji, kwamba huwasilishwa pamoja na ala ya muziki. Ngano huwa ghani masimulizi inapowasilishwa pamoja na ala ya muziki.

Sifo; hizi ni tungo za kusifu, kigezo kilichotumika ni muktadha wa uwasilishaji: sifo huwa ghani masimulizi inapoingiza muziki katika utondozi wake, lugha iliyotumika ni lugha ya kishairi.

Tendi; hizi ni ghani ndefu za masimulizi juu ya matendo ya mashujaa yenye uzito kijamii au kitaifa. Vigezo vilivyotumika katika kugawa kipera hiki ni fani ambayo ni huhusu matukio muhimu ya kihisitoria au ya kijamii. Kigezo kingine ni muktadha wa uwasilishaji, hutungwa na kuwasilishwa papo kwa papo.

Utanzu mwingine wa Fasihi Simulizi ni utanzu wa mazungumzo. Mazungumzo ni maongozi au maelezo ya mdomo katika lugha ya kawaida juu ya jambo lolote lile. Si kila mazungumzo ni fasihi ili mazungumzo yaitwe fasihi lazima yawe na usanii wa aina fulani. Vigezo vilivyotumika katika kugawa utanzu huu ni kigezo cha lugha ambapo lugha iliyotumika ni lugha ya kifasihi. Kigezo kingine ni kigezo cha kimuundo ambapo muundo wake huwa wa kidayalojia.

Utanzu huu wa mazungumzo una vipera vifuatavyo ambavyo ni hotuba, malumbano ya watani, soga, mawaidha na ulumbi.

Hotuba; haya ni mazungumzo ambayo huwasilishwa kwenye vikao rasmi vya kimila, kisiasa au kidini. Vigezo vilivyotumika katika kugawa kipera hiki ni kigezo cha lugha ambapo lugha yake huwa rasmi, sanifu na ya kisanaa. Kigezo kingine ni kigezo cha kimuktadha ambapo hotuba huwasilishwa katika mazingira maalumu kwa mfano katika vikao rasmi au mikutano.

Malumbano ya watani; haya ni mazungumzo yanayozingatia masharti yanayotawala uhusiano wao wa kiutani. Huweza kuwa utani wa kikabila, utani wa mababu au mabibi na wajukuu. Vigezo vilivyotumika katika ugawaji wa kipera hiki ni kigezo cha lugha ambapo lugha huwa ni ya kimafumbo. Kigezo kingine ni kigezo cha wahusika ambapo wahusika huwa na uhusiano wa karibu.

Soga; haya ni mazungumzo ya kupitisha wakati ili kusubiri kitu fulani. Vigezo vilivyotumika katika kugawa kipera hiki ni kigezo cha kidhima ambapo dhima yake ni kupitisha wakati. Kigezo kingine ni kigezo cha lugha ambapo lugha inayotumika siyo rasmi. Vilele kuna kigezo cha muktadha ambapo muktadha wake huwa ni mahali popote.

Mawaidha; haya ni maneno ya maonyo au mafunzo aghalabu huwa ya kidini na yenye muongozo. Kigezo kilichotumika katika kugawa kipera hiki ni kigezo cha kidhima ambapo dhima yake ni kuonya au kutoa muongozo.

Ulumbi; huu ni uhodari wa kuzungumza ambao huwa ni wa kiufasaha na madoido. Vigezo vilivyotumika katika kugawa kipera hiki ni kigezo cha kifani ambapo lugha iliyotumika ni lugha ya kimadoido na kifasaha.

Utanzu mwingine katika Fasihi Simulizi ni utanzu wa maigizo. Maigizo ni michezo ambayo hutumia watendaji wa kuiga tabia na matendo ya watu au viumbe wengine ili kuburudisha na kutoa ujumbe fulani kwa hadhira. Vigezo vilivyotumika katika kutenga utanzu huu ni kigezo cha namna ya uwasilishaji ambapo huwasilishwa kwa kuiga matendo ya watu au wanyama. Kigezo cha kidhima ambapo dhima yake ni kuburudisha, kuelimisha au kuonya. Pia kimetumika kigezo cha mandhari ambapo maigizo huambatana na matukio maalumu kama vile kwenye maadhimisho ya sherehe fulani na katika matukio ya kijamii.

Utanzu mwingine wa Fasihi Simulizi ni utanzu wa ngomezi. Ngomezi ni ile hali ya kupeleka ujumbe kwa kutumia mdundo wa ngoma. Vigezo vilivyotumika katika utanzu huu ni kigezo cha kifaa cha uwasilishaji ambacho ni ngoma. Pia kigezo kingine ni kigezo cha kidhima ambapo dhima yake ni kupeleka taarifa fulani kwa jamii. Mfano taarifa hiyo yaweza kuwa ya msiba, mkutano na kadhalika.

Pamoja na ugawaji huu wa tanzu na vipera vya Fasihi Simulizi uliofanywa na Mulokozi kwa kuzingatia vigezo vyake alivyovitumia, bado ugawaji huu unaudhaifu mkubwa tu. Udhaifu au changamoto za vigezo alivyovitumia Mulokozi ni kama ifuatavyo:-

Vigezo vyote hivi vinaweza kuingiliana; mfano kigezo cha kidhima, kama vile kuonya au kuelimisha huweza kuonekana katika tanzu zaidi ya moja au hata katika vipera mbalimbali.

Pia kigezo cha namna ya uwasilishaji huweza kuingiliana kutoka utanzu mmoja hadi mwingine. Mfano, katika utanzu wa masimulizi na mazungumzo.

Vilevile kigezo cha wahusika; kigezo hiki huweza kuingiliana katika utanzu mmoja na mwingine. Mfano, unaweza kuwa na hadithi yenye wanyama, binadamu, mizimu na kadhalika. Hivyo inakuwa si jambo rahisi kuona tofauti zilizopo.

Kwa kuhitimisha, tunaweza kusema kwamba ni vigumu kuainisha tanzu na vipera vya Fasihi Simulizi kutokana na kwamba, Fasihi Simulizi hubadilika badilika kifani, kimaumbo na hata kimaudhui kwa kutegemea muktadha na namna ya uwasilishaji wake. Kwa mfano ngano iliyopo katika masimulizi ni tofauti na ngano iliyopo katika maghani. Hivyo basi tatizo hili linaweza kutatuliwa kwa kutumia istilahi tofauti katika vipera au tanzu zinazoingiliana.

MAREJEO:

Mulokozi, M. M. (1989). Tanzu za Fasihi Simulizi: Katika Mulika 21. TUKI. Dar es Salaam.

Mulokozi, M.M. (1996). Utangulizi wa Fasihi Simulizi ya Kiswahili. TUKI. Dar es Salaam.

Wamitila, K.W. (2003). Kamusi ya Fasihi, Istilahi na Nadharia. Focus Publications Ltd. Nairobi.

TUKI, (2004). Kamusi ya Kiswahili Sanifu. (Toleo la Pili). East Africa: Oxford University Press na Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI).