Subcribe to our RSS feeds Join Us on Facebook Follow us on Twitter Add to Circles

Jumatano, 7 Januari 2015

KATEGORIA ZA KISARUFI KULINGANA NA MTIZAMO WA WANAMAMBOLEO NA MTAZAMO WA WANAMAPOKEO:- :-

        I.            KATEGORIA ZA KISARUFI KULINGANA NA MTIZAMO WA WANAMAMBOLEO:-
Kategoria ya Sarufi ya kimamboleoInaoongozwa na wanasosiolojia ambao unahusisha sarufi mbalimbali kama vile :- Sarufi msonge , Sarufi miundo virai na Sarufi geuza maumbo zalishi iv. Sarufi husiano Katika kategoria hii huu ndipo tunapata kuona  sarufi kama tafiti na uchambuzi wa miundo inavyooneka kwenye lugha.
a)      Kategoria ya Muundo wa Kirai;
Kirai ni fungu la maneno yanayohusiana kimuundo lisilokuwa na muundo wa kiima kiarifu. Maneno katika kirai humilikiwa na neno moja ambalo ndilo neno kuu. Kirai hubainishwa na kategoria ya neno kuu. Kwa mfano: KN, KT, KV, KE KH n.k.
Virai huundwa na viambajengo. Kiambajengo ni kikundi cha maneno au hata neno moja pia inayofanya kazi kama kitu kimoja. Kirai, kishazi au sentensi ni mkusanyiko wa viambajengo kadha.
Kirai ni mkusanyiko wa viambajengo vilivyojengwa kuzunguka neno kuu. Kwa mfano, KN huundwa na nomino na vivumishi vyake, kwa hivyo muundo wa kirai ni maneno yanayokiunda yakiwakilishwa na alama za kategoria za maneno hayo.
Kwa mfano: a) ‘Mtoto mdogo’.    Hiki ni Kirai Nomino (KN) kilichoundwa na N (nomino) na V (kivumishi).  Kwa hivyo KN  N+V       b) ‘analima shamba’.
Hiki ni kirai kitenzi (KT) chenye kuundwa na kitenzi (T) na kirai nomino (KN). Kwa hivyo KT  T+KN.

b)      Kategoria ya Muundo wa Vishazi na Sentensi
Kishazi ni kikundi cha maneno kilicho ndani ya sentensi chenye muundo wa kiima na kiarifu. Kishazi kina muundo sawa na sentensi.
Sentensi ni kikundi cha maneno chenye maana iliyo kamili. Sentensi ndicho kipashio lugha cha kimuundo ambacho ni kikubwa kuliko vipashio vingine. Vipashio vya lugha ni pamoja na: mofimu, neno, kirai, kishazi na sentensi yenyewe. Sentensi na kishazi huundwa na virai vikuu viwili: KN na KT. KT yaweza kuundwa na kitenzi na nomino, kitenzi na kielezi .
Kwa hivyo S- KN + KT
c)      Kategoria ya Sarufi geuza umbo zalishi;
Kategoria ya  geuza umbo zalishi huonyesha ujuzi alionao mzungumzaji ambao humwezesha kutunga sentensi sahihi na zisizo na kikomo. Uwezo wa mzungumzaji kutunga sentensi zisizo na ukomo unatokana na kufahamu kanuni za kutunga sentensi sahihi ambazo mzawa wa lugha anazijua kutokana na kuwa na umilisi na lugha yake. Kanuni za kutunga sentensi sahihi hubainisha sentensi sahihi na zisizo sahihi.
Kwa mujibu wa kategoria hii, sentensi ina umbo la nje ambalo ndilo linalojitokeza katika usemaji na hata inapoandikwa, na umbo la ndani ambalo huwa limefichika na hujidhihirisha katika umbo jingine wakati wa kuongea (maana).
Kategoria hii imeweza kuonyesha uhusiano wa tungo ambazo japo zilikuwa na umbo la nje tofauti, zina umbo la ndani sawa.
Kwa mfano:
Juma  anacheza  mpira
KN       KT           KN

Mpira  unachezwa na  Juma
               KN    KT           KU   KN
Mfanano wa tungo hizi umekitwa katika maana. Japokuwa sentensi a) inaanza na Juma, na ile b) inaanza na Mpira, mtenda na mtendwa katika sentensi zote ni yule yule.
d)      Kategoria ya Sarufi miundo virai zalishi;
Katika  kategoria ya sarufi miundo virai zalishi muundo wa sentensi huelezwa kwa kuchanganua vijenzi vyake ambavyo ni viambajengo. Viambajengo hivi huchanganuliwa hadi kufikia neno moja ambalo hubainishwa kwa kategoria yake ya kisarufi. Uchanganuzi huu wa sentensi huelezwa kwa kanuni ambazo huwezesha kutunga sentensi nyingi zaidi.
Kanuni za muundo virai.    KN  N --- mtoto
Hii ina maana kuwa KN ina N (yaani Kirai Nomino kina kiambajengo kimoja tu ambacho ni nomino). Hii yaweza pia kuelezwa hivi:
KN  N     Mtoto
Hii ina maana kuwa kirai hiki ni neno moja. ‘mtoto’Kirai chenye viambajengo zaidi kimoja, yaani chenye maneno zaidi ya moja  huelezwa kwa kanuni:
KN N V au KN N V      Mtoto mzuri Hii ina maana kuwa KN kinaundwa na maneno mawili, yaani ‘mtoto mzuri’Vivyo hivyo kwa Kirai kitenzi (KT).


KATEGORIA ZA KISARUFI KULINGANA NA MTAZAMO  WA WANAMAPOKEO:-
Kama ilivyoelezwa hapo mwanzoni kuwa kategoria za kisarufi zinahusu sifa zinazoambatanishwa katika aina za maneno nazo ni kama ifuatavyo:-
Kategoria za nafsi, ni sifa ama ni kipashio kinachodhihirisha muhusika katika usemaji nazo zipo za aina tatu ambazo nafsi ya I, II, na  III ambapo huwakilishwa na ni-tu, u-m na a-wa.viwakilishi katika ngazi hii ni tegemezi kwani haviwezi kusimama peke yake na kuleta maana iliyokusudiwa.kwa mfano
Nafsi ya I ninaimba- tunaimba
Nafsi II  unaimba- mnaimba
Nafsi III anaimba – wanaimba
Kategoria za njeo/wakati, ni viambishi vinavyoambikwa katika mashina ya vitenzi vikionesha au kutoa taarifa ya tendo lililtendeka, linatendeka au litatendeka muda gani.viambishi hivi ni vingi lakini vimewekwa katika katika hali ya uyakinishi na viambishi vya tendo katika hali ya ukanushi, njeo hiyo iliyopo, iliyopita, na ijayo katika hali ya uyakinishi na ukanushi kwa mfano. Njeo iliyopita   Alicheza -   hakucheza
                         Walicheza – hawakucheza
Njeo iliyopo     ninasoma -  sisomi
                          Tunasoma – hatusomi
Njeo ijayo          utalima – hautalima
                         Mtalima- hamtalima
Kategoria za hali,ni viwakilishi ni viwakilishi vinavyopachikwa katika mashina ya vitenzi ambavyo huangalia utendekaji wa lile tendo. Kategoria hizi huwa viko karibu sana na kategoria za njeo.japo zina utofauti kuna aina zaidi ya tatu za hali kwa mfano hali ya mazoea huwakilishwa na (hu-) hali ya kuendelea huwakilishwa na kiambishi (na-), hali ya masharti huwakilshwa na kimbishi (-ki-/-nge-/-ngali-/-ngeli-) na hali timilifu inayowakilishwa na kiambishi (-me-). Katika hali ya kutokea viambishi hivi havitokei katika shina moja la kitenzi ilavinaweza vikatokea katika sentensi moja katika mashina tofauti ya vitenzi.kwa mfano mwalimu alikuwa anafundisha /amefundisha . katika sentensi hii -li- inaonesha njeo na -na- /-me- inaonesha hali
Kategoria za idadi, hivi ni viambishi vinavyoambikwa katika aina mbalimbali za maneno vikionesha umoja na wingi ambapo katika Kiswahili hudhihirika kupitia viambishi ngeli vya upatanisho wa kisarufi . kwa mfano mwalimu analima, walimu wanalima (a-wa) huonesha umoja na wingi hivyo hudokeza idadi.
        

Kategoria za kauli, ambalo ni umbo ni umbo la kitenzi ambalo linadhihirisha uhusiano baina ya kiima na yambwa mfano kauli ya kutenda na kutendwa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni