Subcribe to our RSS feeds Join Us on Facebook Follow us on Twitter Add to Circles

Jumanne, 9 Septemba 2014

KIDAHIZO KATIKA KAMUSI.

Swali:-    Kidahizo ndiyo msingi wa kamusi. Fafanua kauli hii ukizingatia maumbo ya maneno yanayoweza kukaa katika nafasi ya kidahizo.


    Swali litajibiwa kwa kuligawa katika sehemu tofauti ili liweze kueleweka vizuri. Ambapo  tutaangalia maana ya kidahizo, maana ya kamusi, maelezo ya kina kuhusu kidahizo na kisha tutaangalia jinsi maumbo ya maneno yanavyoweza kukaa katika nafasi ya kidahizo.
Istlahi kidahizo imefafanuliwa na wataalamu wengi miongoni mwao ni pamoja na hawa wafuatao;
TUKI (1981) wanaafasili kidahizo kama neno linaloingizwa katika kamusi kwa chapa ilyokolezwa.
BAKIZA (2010) nao wanaeleza kuwa; kidahizo; ni neno linalochapishwa kwa hati zilizokozwa na pengine kutiwa rangi kwenye kamusi ambalo taarifa zake zinafanuliwa. Tunaweza kuwaunga mkono wataalamu hawa fasili yao kwani kidahizo huwa katika wino uliokolezwa na huingizwa katika kamusi ili kutolewa maana. Lakini kwa fsili ya jumla tunaweza kusema kuwa,
Kidahihizo ni neno linaloingizwa katika kamusi ili liweze kufafanuliwa kwa kupatiwa maelezo yanayohusu taarifa za kisarufi, maana, matumizi, etimolojia semi mbalimbali za lugha na nyingine.
Oxford (2010) wanaeleza kuwa; kamusi ni kitabu ambacho huwa kinaorodha ya maneno ya lugha fulani katika mpangilio wa alfabeti na huelezwa maana ya maneno hayo. Au kamusi ni orodha ya maneno yaliyopo katika mfumo wa eletroki kwa mfano yanaweza kuhifadhiwa katika kompyuta. Faslili hii ionekena kuwa na mashiko kwani kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia si sahihi tene kufasiri kamusi kama kitabu bila kuihusisha na elektroniki katika uhidhi wake.
Kamusi hutungwa ikiwa na malengo mbalimbali kulingana na mahitaji na matumizi ya taaluma au mtumiajia fulani. Mfano zipo kamusi za uwanja husika kama sheria, isimu, falsafa na nyingine. hivyo uteuzi wa msamiati hulingana na uwanja unaotungiwa ambapo kama ni uwanja wa jumla lazima tutakuta msamiati wenye lugha sahili au lahisi. Hivyo msamiati unaokusanywa na kuwekwa katika kamusi ili kufasiliwa ndiyo huitwa kidahizo. Vidahizo hufafanuliwa kwa kupatiwa taarifa za kina ili anayetaka taarifa hizo azipate bila utata wowote.
Katika kamusi za Kiswahili vidahizo huwa na maneno ya kawaida yanayotumika katika Nyanja mbalimbali za mawasiliano miongoni mwa wazungumzaji wa Kiswahili. Msamiati unaoingizwa katika kamusi kama vidahizo hukusanywa katika sehemu tofauti  mfano machapisho mbalimbali, kama matini magazeti na vitabu mbalimbali.
Kidahizo kimegawanyika katika sehemu mbili yaani kidahizo huru na kidahizo mfuto. Hii ni kwa mujibu wa TUKI (2000). Kidahizo kikuu katika kamusi huwa ni umbo la msingi la neno. Mfano “lim.a” “li.a” wakati kidahizo mfuto, ni kinyambuo  kisichotumika sana au neno ambatani ambalo limeingizwa ndani ya maelezo ya kidahizo kikuu. Na kusoma maelezo ya maana ya kisarufi. Iwapo halitumiki sana au halijapata kutumika lakini likatumika tu kwa siku moja hupatiwa maana ya kisarufi tu. Kinyambuo cha kitenzi ambacho kina kategoria tofauti huingizwa kama kidahizo mfuto ndani ya umbo la msingi bila maelezo ya maana na kisha huingizwa tena kama kidahizo kikuu katika herufi ya alfabeti inayohusika.
Kidahizo kama msingi wa kamusi, hupangwa kwa kufuata utaratibu wa alfabeti. Kwa kila ukurasa neno la kwanza na la mwisho katika ukurasa limechapwa sehemu ya juu ya ukurasa ili kumwongoza msomaji atambue nafasi ya neno analohitaji au analotafuta, iwapo lipo katika ukurasa anaousoma au lipo nyuma au mbele ya ukurasa unaohusika maneno ya kumuongoza msomaji humwezesha kupitia kamusi na kugundua neno unalotaka kuliko kusoma ukurasa na kila kidahizo ili kupata neno unalotafuta.
Kidahizo ni msingi wa kamusi kwa kutokana nacho ndipo tunapata maana ya maana ya neno, etimolojia yake, matumizi na matamshi yake. Kwa hiyo bila kidahizo hatuwezi kuwa na kamusi. Msamiati wote unaokusanywa huwa ni kwa ajiri ya kutolewa maana katika kamusi ili kusaidia watumiajia wa lugha Fulani au wenye kuhitaji kujua msamiati wowote kutumia kamusi. Kwa hiyo naweza kusema hakuna kidahizo hakuna kamusi. Huo ndiyo umuhimu wa kidahizo katika kamusi.
Baada ya maelezo hayo mengi sasa tuone maumbo yanayoweza kutokea katika kamusi kama kidahizo.  Maumbo hayo ni kama haya yafuatayo.
Maumbo sahili; haya ni maumbo yanayoumbwa kwa neno huru yaani lisilo na utegemezi au lisiloweza kuambishwa.
                    Kwa mfano; maneno kama
                “barua”, “nyumba”, “bakuli” na “baba”.
Maneno haya ni huru. Hivyo maumbo haya huingizwa  katika kamusi kama kidahizo.
Maumbo ambatani; haya ni maumbo ya maneno ambayo huumbwa kwa kuunganisha maneno mawili tofauti, mfano nomino na kitenzi, nomino na nomino na mengine. Katka kamusi maneno haya huchukuliwa kama neno moja lenye kuwakilisha dhana fulani. Kwa mfano maumbo haya yametoka katika kamusi ya tuki (2001).
Kipeleleza-nyanbizi nm vi- [ki-vi-] asdic.
Kipazasauti nm vi- [ki-vi-] loud speaker.
Kipashamoto nm vi- [ki-vi-] chafing-dish.
Kipimahewa nm vi- [ki-vi-] barometer
Kitanguakimbanga nm vi- [ki-vi-] anticyclone
Maneno yote haya ni mwambatano lakini katika kamusi husimama kama neno moja na siyo kuwa tunaangalia maana ya neno moja moja. Hapa nisawasawa na maneno ya nahau, misemo nayo katika kamusi huchukuliwa kama neno moja lenye kuwakilisha dhana fulani. Mfano; TUKI (2001)
Kifungua kinywa,
 kick the bucket,
tia  nanga.
Maumbo changamani, ni maumbo ya maneno yanyokuwa na uchangamani. Ni maneno ambayo hayawezi   kusimama pekee katika kamusi. Maneno haya huwa na viambishi vinavyotenga mzizi wa  neno pia maneno haya hutengwa ili kuonesha uwezo wa kunyumbuliwa au kuchukua viamshi tofauti tofauti. Mfano;

M.toto 
M.tu
Nufaik.a
Nui.a
Maneno haya huweza kunyumbuliwa na kuleta maana nyingine tofauti na maneno sahili ambayo hayawezi kunyumbuliwa. Kwa mfano neno “nui.a” linaweza kunyumbuliwa na kupata maneno mengine kama, nuilia,nuilika, nuiana nuiza.
Maumbo hulutishi, haya ni maumbo ambayo kutokea kama kidahizo katika kamusi. Maneno haya huundwa kwa kuunganisha sehemu mbili za maneno tofauti na siyo kuunganisha maneno mazima. Kwa mfano;
Telephone
Mobitel
Telefax
Maumbo ya akronimia, haya ni maumbo yanayoingizwa katika kamusi kama kidahizo. Maumbo haya huwa katika ufupisho na huwakilishwa kwa herufi kubwa ambazo kila herufi hubaeba dhba Fulani. Mfano; kutoka Oxford (2006).
ISBN International Standard Book Number
ISA Industry Standard Architecture
ISDN Integrated Services Digital Network
SAD Seasonal Affective Disorders
Akronimia hizi hutokea upande wa kidahizo kuwakilisha maana  ama dhana iliyondefu kuwa katika maneno machache.
Maumbo rejerezi, katika kidahizo kuna maumbo ya maneno ya kumfanya msomajia arejelee neno jingine ili kupata ufafanuzi zaidi, maneno yanayorejelewa katika kamusi huoneshwa kwa mshale. Mshale huu ulenga kumuonesha msomaji kulitafuta neno analooneshwa. Kwa mfano;
Pally   → PAL
Pas.try  →see also CHOUX PASTRY
Pipe  → see also PIN PIPES
Mshale huu huwekwa baada ya kuwa taarifa zote kuhusu kidahizo hicho zimetolewa, na huenda kunahitajika maaelezo ya ziada kuhusu neno hilo kwa hiyo msomaji huoneshwa neno jingine kwa mshale ili aone tena maelezo hayo.
Maumbo dondoshi, haya ni maumbo ambayo huingizwa katika kamusi kama kidahizo baada ya sehemu ya neno hili kudondoshwa. Mfano wa maumbo hayo ni kama vile; kutoka katika Oxford (2006).
Phone kutokana na neno telephone
Gram kutokana na neno telegram.
Bike  kutoka na neno bicycle
Maumbo haya fupishi tunayakuta katika kidahizo cha kamusi na hubeba maana ambayo inapatikana katika neno zima ambalo halijafupishwa.
Maumbo radidi, haya ni maumbo ya neno linalojirudia rudia katika kamusi. Neno hili hubeba dhana  moja katika kamusi. Kwa mfano maneno kama,
Uramberambe nm [u-] coconut kernel
Mzengazenga nm mi-n[u-i] carrying two things by using a pole across the soulder
Mzikoziko nm mi [u-li- ] ipecacuanha.
Mnyunginyungi.
Maneno haya hubeba dhana moja inayowakilishwa na uradidi huo.
Maumbo mengine yanayoweza kuingizwa katika kamusi kama kidahizo ni maumbo ya homonimia. Maneno haya huwa na maumbo sawa na matamshi sawa lakini maana huwa tofauti. Katika kamusi huingizwa kama vidahizo vyenye maana tofauti na maana hizo hutofautishwa kwa kupewa namba.
Mfano
Kaa1.
Kaa2,
Kaa3
Panda1,
Panada2
Panda3
Vidahizo hivyo huonekana katika kamusi kama ilivyo mifano hapo juu.

Kwa kuhitimisha, tunaweza kusema kuwa uorodheshaji wa vidahizo katika kamusi hutegemea lengo la kamusi. Mfano kama kamusi ni ya kisheria huorodhesha vidahizo vyake katika  misingi ya kiseria. Maana za msingi ndizo huorodheshwa kwanza na kufuatiwa na maana zilizozuka baadaye au maana zinazohusishwa na neno hilo. Kidahizo ni cha msingi katika kamusi kwani huonesha herufi rasimi zinazopaswa kuunda neno.

Marejeo
BAKIZA (2010) Kamusi ya Kiswahili Fasaha. Kenya: Oxford University Press.
Mdee, J. S. (2010) Nadharia na Historia ya Leksokografia. Dar es Salaam: TUKI.
Oxford (2010) Oxford Advanced Learner’s Dictionary. New York: Oxford University Press.
TUKI (2001) Kamusi ya Kiswahili-Kiingereza. Dar es Salaam: TUKI.
TUKI (2004) Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Dar es Salaam: TUKI.
TUKI (2006) English-Kiswahili Dictionary. Dar es Salaam: TUKI

MATUMIZI YA MISEMO MAGAZETINI:

 
         Misemo magazetini hutumika kwa namna tofauti. Matumizi haya ya misemo hutumiwa moja kwa moja kwenye vichwa vya habari au katika maelezo. Baadhi ya vichwa vya habari hutofautiana na mada ambazo huwa zinakuwemo  ndani ya habari.Hii ina maana kuwa misemo inayotumika huwa na maana iliyotofauti kabisa na maana inayoonekana magazetini.Misemo mingine tumeionyesha kwenye kiambatisho.  Ngoja uangalie mifano ifuatayo:
a)      Nesi  Kitete ajikaanga (Mtanzania, mei, 23,2011.)
b)      Sarakakasi za Sitta Mwakyembe CCJ (Mtanzania, Mei 9, 2011).
c)      Vigogo CCM  wakaangwa (Manzania, Mei,23,2011)  .
d)     Spika, Zitto jino kwa jino, Mkulo  apigilia msumali wa mwisho(Uhulu, Juni, 14, 2011).
e)      Ujamaa wampofusha Mukama(Rai,mei 19-25,2011).
f)       Lady Jaydee kutembea uchi live(Sani,Mei, 14,2011).
g)      Akina Ukwa waja tena (Kiu, ya jibu Juni, 23,2011).
h)      Ngeleja kitanzini(Uhuru, Juni; 6, 2011).
i)        Mashabiki Yanga wafurika kushuhudia majembe yao (Bingwa, Juni, 14, 2011).
j)        Ulimwengu ndiye muuaji (Uhuru Juni 6, 2011).
k)      Morocco yafanya mauaji (Uhuru, Juni 6, 2011).
l)        Mbowe balaa Dar (Majira, juni,6, 2011) .
m)    Mganda awasili kumvaa Mwakyembe(Bingwa Mei, 20 , 2011).
n)      Lowassa amkatia Kiwete rufaa (Mwananchi, juni, 16, 2011).
o)      UPDP kuunguruma Dar kesho (Mtanzania,Mei,25,2011).
p)      CDA yakabwa koo na kamati ya bunge(Bingwa,Mei, 20,2011).
Katika mifano hii, ni dhahili kuwa maana inayoonekana katika msemo hii sivyo ilivyo katika maelezo au habari nzima. Mfano, katika (a) siyo kwamba ‘nesi alijikaanga kiaangoni’ bali alijiweka katika mazingira magumu ya kuendelea na kazi baada yahuduma  kumzalisha mama
                                                                         8.
 na mwanae kufichwa. Pia katika (f) haimaanishi Ukwa waigizaji wa Nigeria bali kuna vijana waliojifananishwa na waigizaji hao. Katika (h) ‘majembe’ haimaanishi majembe vifaa bali anamaanisha wachezaji wapya waliosajiliwa na timu ya Yanga.Mifano mingine mingi tutaitolea maana katika sehemu inayofuatwa.
                                                                     
4.1.KWA NINI MAGAZETI HUTUMIA MISEMO:
Kihole (2004) anasema kuwa ; ‘ni kwa hali hii ya kushangaza kile kinachotajwa katika mada hiyo ama hufanya baadhi ya wasomaji kukosa hata hamu ya kufikiria kununua magazeti haya au kuwachochea watu kufanya juhudi za kuyapata magazeti hayo’. Hivyo baadhi ya magazeti hutumia misemo ili kuvuta umakini wa wasomaji. Ngoja sasa tuangalie baadhi ya misemo ambayo huweza kuvuta wasomaji.
a)      Nilitema big G kwa karanga za kuonjeshwa
b)      Ray C akimbia nchi.
c)      Ngono Big Brother sasa(Kiu ya Jibu,juni,22,2011).
d)     Nilipopiga ramri kumtafuta Mungu(Kiu ya jibu,Juni,22,2011).
e)      Lady  Jay dee kutembea uchi(Ku ya jibu,Juni,22,2011).
f)       Kituo cha kuoshea nyeti za kike Dar(Sani,Mei,11-14).
g)      Mganda awasili kumvaa Mwakyembe (Bingwa Mei,20,2011).
h)      Spika Makinda mbumbumbu anasimamia asichokijua (Rai,Juni,20,2011).
i)        Freemason na ugaidi katika kanzu ya uislamu (Mtanzania,Juni,17,2011).
j)        Wanaume kumeza vidonge vya kuzuia mimba(Uhuru, Juni, 7-14,2011).
k)      Sauti ya radi awa makamu wa Rais(Ijumaa mei, 20, 2011).
l)        Waziri, changu wateta kwa nusu saa Dom(Ijuma,Julai,15,2011).
m)    90% mastaa wauza ngono bei chee(Ijumaa, Julai,15,2011).
n)      Badra aanika chachandu zake adatisha midume(Ijumaa,Julai,15,2011).
o)      Mchumba aliyevua nguo (Dimba, Juli,17,2011).
p)      Linah sina mtu sasa niko single(Sani,juni,12,2011).
q)      Mrembo anaswa akichimba dawa hadharani(Iumaa,Julai,15,2011).
                                                            9.
Kwa kuitazama  misemo hii katika vichwa vya magazeti  tunaweza kubaini kuwa inavutia wasomaji hata kununua magazeti ili kupata taarifa iliyomo ndani ya gazeti hilo. Kutokana maoni ya Kihole (2004) anaposema kuwa ni kutokana na matumizi ya misemo hiyo wasomaji huweza kukatishwa tamaa au kufanya juhudi za kuyapata magazeti hayo, tumeshuhudia magazeti mengi yakitumia misemo hiyo ili kufanikisha
nia ya wasomaji. Mfano gazeti la sani, Ijumaa na Kiu.

1.1.KUSISITIZA JAMBO:
Katika utafiti wetu tumegundua kuwa magazeti hutumia misemo, na misemo hiyo huwa inajirudiarudia katika magazeti mengi. Misemo hii hulenga kuweka msisitizo juu ya jambo lilopita, lililopo au lijalo. Mfano misemo tuliyoitumia katika utafiti wetu baadhi inasisitiza juu ya mambo yaliyokuwepo katika kipindi hicho cha utafiti ulipofanyika. Ngoja sasa tuione baadhi ya misemo hiyo.
a)      Tibaijuka ang’aka(Mtanzania,Mei,20,2011).
-Hi ilkuwa kipindi cha mchakato wa watu kurudisha ardhi walizochukua na wananchi bila kukubaliwa na serikali.
b)      Wabunge CCM wakaangwa (Mtanzania, Mei,23,2011).
Misemo hii imesikika sana kipindi cha wabunge wanahusihwa na migogoro ya chama   ilyojulikana kama (kujivua gamba).
c)      DC walimu wa shule za kata wasiitwe Voda fasta.
d)     Kujivua gamba hakutoshi.
Katika mifano hii misemo mingine huibuka kulingana na mada iliyopo na baadae misemo hiyo haisikiki tena. Hivyo ni kutokana na msisitizo huo wasomaji huweza kuwa na ufuatilizi juu ya tukio fulani kulingana na jinsi linavyotokea mara kwa mara.


                                                                 
1.2.MAANA YA MISEMO MAGAZETINI:
 Katika utafiti huu tumegundua kuwa magazeti hutumia misemo mbalimbali yenye maana tofauti. Kulingana na nadhalia iliyotumika kuchambua utafiti huu tumeona kuwa kazi ya fasihi huwa haina maana moja hivyo maana inaweza kutokana na kazi iliyopo au kulingana mukutadha uliopo. Hivyo maana ya misemo mingine hutokana na mukutadha wa kazi iliyopo. Hivyo katika maana ya misemo  hii tuliyotoa tumezingatia jinsi misemo hii ilivyotokea magazetini.  Mfano wa ,misemo hii ni kama ifuatavyo;
a)      Kalenga aipiga tafu Vodacom miss Bagamoyo(Mtanzania,Mei, 20,2011).
-‘Kupiga tafu’       kusidia .
b)      Aahidi kuanika hadharani vielelezo walivyoshiriki(Mtanzania,Mei, 20, 2011).
                -‘Kuanika’ maana yake ni kuweka wazi.
c)      Azzani asiwe mbuzi wa kafara CCM (Rai, Mei, 19-25,2011).
-‘Kuwa mbuzi wa kafara maana yake’ asiangaliwe kama mkosaji kutokana na makosa
                    yanayofanywa na wakuu wake wa kazi.   
d)     TAKUKURU inabweka lakini haing’ati(Rai, mei, 19-25, 2011)
-‘Hii ina maana kuwa takukuru inatishia lakini haitendi.

e)      Niyonzima aotambawa jangwani(Bingwa, Mei, 20,2011).
-Kuota mbawa maana yake ni kushindwa kufikia mwafaka.

f)       Nyota wa Man U walipoanika vifaa vyao kwenye ‘pati’Bingwa, (Mei,19-25,2011).
           -Kuanika vifaa maana yake walikuusanyika na nakujumuisha wake zao. Vifaa ni
wanawake.
g)      Mshindi wa Tanzania ajishebedua ‘BBA’.(Bingwa, Mei,19-25,2011).
-Kujishebedua maana yake kujifanya hutaki kitu fulani huku unakitaka.

h)      Blatter amekalia kutikavu FIFA? (Majira,23,2011).
-Kukalia kuti kavu maana yake amejiweka katika nafasi ngumu ya kazi yake.
i)        Bimman abwaga manyanga (Majira,Mei,23,2011).
-Kubwaga manyanga maana yake kuacha kazi.
                                                           11.

j)        Harambee ya Yanga yadoda (Uhuru, Mei, 3,2011).
-Kudoda maana yake kushindwa.

k)      Wadai hukumu inanuka rushwa(Majira,Mei,23,2011).
-Kunuka rushwa ina maana kuwa kuna hali ya kutoa rushwa katika hukumu hiyo.
l)        Mwakalebela aibwaga TAKUKURU.
-‘Kuibwaga’ ina maana ya alishinda kesi iliyomkabili kuhusu TAKUKURU.
Hivyo kama tulivyoeleza kabla hatujaanza kutoa mifano hii kuwa kazi ya fasihi huwa haina maana moja, nidhahili kuwa maana nyingine katika mifano hii imetolewa kulingana na muktadha wa kazi yenyewe au taarifa ilivyo kwenye magazeti.
Waandishi wa magazeti nchini Tanzania wanatumia misemo katika magazeti, kwanza ni kwa sababu ya kutaka siko la magazeti yao,hii ni kwa mujibu wa mwafunzi mmoja mwenye namba ya usajiri (2009-04-03894). Anasema kuwa waandishi hutumia misemo katika vichwa vya habari kwa kudokezea kile kitakachokuwa ndani ya habari yenyewe.Mfano ‘endelea na habari hii ndani upate uhondo’ ‘usijinyime uhondo huu’ Hivyo misemo hii imekuwa chanzo cha waandishi kuuza kazi zao. Mfano gazeti la SaniIjumaa, Kiu.
Pia kwa muuza gazeti katika kituo cha mabasi kilichoko ubungo jijini Dar es salaam namba ya simu 0713750941)  anasema kuwa amekuwa akiuza magazeti kwa muda mrefu na kusema kuwa magazeti yanayonunuliwa saana ni yale yenye maneno yanayovutia.
hivyo tukizingatia maoni na maelezo ya watu hawa tunaweza kukubaliana nao kwani tunaona maagazeti mengi yakitumia misemo mingi.   


                                                    HITIMISHO:
        Kwa kuhitimisha tunaweza kusema kuwa misemo ni kipengele ambacho ni kipana sana kwani katika utafiti wetu tumegusia tu misemo bila kangalia dhima zake, fani na maudhui yake. Hivyo ni bora zaidi kufanyike uchunguzi mwingine ili kuweza kubaini vipengele hivyo vya fani na maudhui. Vile vile misemo mingi huanza kama misimu na ikitumiwa sana huweza kuwa na mashiko na kutumika maeneo tofauti.
                                                                       

                                                          
KIAMBATISHO.
1.      Tibaijuka ang’aka.
2.      Nesi kitete ajikaanga.
3.      Kalenga aipiga tafu Vodacom miss Bagamoyo.
4.      Sarakasi za sitta Mwakyembe CCJ.
5.      Akili kuanika hadharani vielelezo walivyoshiriki.
6.      Vigogo CCM wakaangwa.
7.      Wafumania nyavu 10 kukumbukwa.
8.      UPDP kuunguruma Dar kesho.
9.      Ujamaa wampofusha Mkama.
10.  Azzan asiwe mbuzi wa kafara.
11.  Wizara ya elimu imulikwe.
12.  Takukuru inabweka lakini haing’at.i
13.  Gamba laCCM halivuliki, ibueni mafisadi.
14.  Mganda awasili kumvaa Mwakyembe.
15.  Nyota wa Man U walipoanika vifaa vyao.
16.  Mshiriki wa Tanzania BBA ajishebedua.
17.  Mbowe balaa Dar.
18.  Bimman abwaga manyanga.
19.  Wadai hukumu inanuka rushwa.
20.  CDA yakabwa koo na kamati ya bunge.
21.  Mwakalebela aibwaga TAKUKURU.
22.  Harambee ya Yanga yadoda.
23.  DC walimu wa shule za kata wasiitwe Vodafasta
24.  Ris wa zamani wa FIFA amkingia Blatter kifua
25.  Wamer amkaanga Bin Hamman
26.  Sauti ya radi awa makamu wa Rais
27.  Kujivua gamba hakutoshi
28.  Balozi wa Tanzania UK katikati ya mkutano.
29.  CCM itambue ugumu na urefu wa gamba.
30.  Mkata  tawi Gbagbo hakumsikiliza Odinga kawasikliza mijusi
31.  Basi lakanyaga kombe la Real Madrid
32.  Ulimwengu ndiye muuaji
33.  Kauli hizi za viongozi CHADEMA mauti yetu
34.  Mateja wageuza kituo cha mabasi ‘Gesti bubu’
35.  Kiburi chamuondoa duniani
36.  Spika Zitto jino kwa jino
37.  Kujivua gamba si ndoto ya mchana
                                                                      15.
38.  Tulivyozunguka kuitafuta vaselini Kampara
39.  Mashabiki wafurika kushuhudia majembe yao.
40.  Basena akunwa na beki wa Motema pembe.
41.  Wyne Rooney apandikiza nywele.
42.  Ngeleja kitanzini.
43.  Wanaume kuanza kumeza vidonge vya kuzuia mimba.
44.  Ikulu – viongozi wa dini si Malaika.
45.  Lady Jaydee kutembea uchi live.
46.  Kituo cha kuoshea nyeti za kike Dar.
47.  Wabunge wamchefua Spika Makinda awafananisha na watu wa kariakoo.
48.  CCM mnahangaika na Lowassa CHADEMA haoooo..
49.  Pinda hajui idadi ya mawaziri wanaoishi hotelini.
50.  Freemasoni na ugaidi ndani ya kanzu yabuislamu.
51.  Julio amtolea nje nyota wa Chelsea.
52.  Jenerali mchana nyavu ageuka balozi Japan.
53.  Mjadara wa posho waitikisa nchi.
54.  Dr. Slaa pakacha na chujio hayahifadhi maji.
55.  Abebwaye hukitazama kisogo cha ambebaye.
56.  Nani mwanamke shujaa ajitokeze tumuone?
57.  CCM ikiwatimua mapacha watatu tutawapokea AFP.
58.  Spika Makinda mbumbumbu asimamia asichokijua.
59.  Lowassa amkatia Kikwete rufaa.
60.  Munge arusha mpira Masijala.
61.   Mlema sijiudhulu ng’o.
62.  Bajeti iliyotolewa na Zitto haina masilahi kwa taifa.
63.  Ngono Big Brother sasa.
64.  Aliyezama baharini kusaka mwili wa osama aibukia patupu.
65.  Nilivyopiga ramli kumtafuta Mungu.
66.  Aki na Ukwa waja tena.
67.  Nilitema big ‘G’ kwa karanga za kuonjeshwa.
68.  Ray c akimbia nchi.
69.  Waziri, changu wateta kwa nusu saa Dom.
70.  Mainda, Steve Nyerere Mhhhh!.
71.  90% Mastaa wauza ngono bei cheee.
72.  Mrembo anaswa.
73.  Badra aanika chachandu zake adatisha midume.
74.  Asha Bakari vimwana Twanga pepeta ni zaidi ya miss.
75.  Mchumba aliyevua nguo shereheni.
76.  Lina sina mtu kwa sasa niko single.
                                                                              16.
77.  Belina alizwa viatu, atangaza dau.
78.  Kalala Juniour bifu za kijinga siyo ishu.
79.  Kuolewa si kila kitu dada’ngu vuta subila.
80.  Aliyemwaga radhi hadharani aachwa kwa taraka tatu.
81.  Jenifer Aniston amwenzi mbwa wake kwa totoo!
82.  Wanaomjua waanika siri zke.
83.  Mrembo anaswa akichimba dawa hadharani.
84.  Lina sina wakumpa penzi.
85.  Mbunge CHADEMA amlipua Sitta.
86.  Lowassa alizwa na kujiudhuru kwa Rostam.
87.  Mikopo ya elimu ya juu yaitafuna wizara ya elimu.
88.  Lowassa amlilia Rostam.
89.  Rostam adaiwa kumkejeli Kikwete.
90.  Ngeleja uso kwa uso na wabunge leo.
91.  Uamuzi wa Rostam kuachia ngazi watikisa nchi.




            
                                                            
                                                           MAREJEO.
Kihole, Y.M.(2004) Maswala ya kisarufi katika magazeti ya mitaani ya kiswahili: Tanzania.
              Mtandao www.ifeas-uni-mainz.de/SwaFo/SF11%20 kihore.pdf
King’ei, K.(2000) Matumizi ya Lugha kwenye vyombo vya habari. Kenya:  Mtandao
Mgazeti, Mtanzania, Kiu ya jibu, Ijumaa, Rai, Majira, Uhuru, Nipashe, Mwananchi, Bingwa,
             Mwananchi,Sani,: ya kuanzia Mei-Julai (2011).
Mulokozi .M.M.(1996)Utangulizi  wa  Fasihi. Dar  es  salaam:Taasisi  ya  Uchunguzi wa
               Kiswahili.
Wafula. R.M. na K.  Njogu (2002) Nadharia za Uhakiki wa Fasihi. Nairobi: Jomo Kenyatta
               Publishers Ltd.
Wamitila. K.W. (2006)Uhakiki wa Fasihi:Misingi na Vipengele Vyake. Nairobi:Kenya Litho
                Ltd.
  www.landmark.edu/library/citation-guides/apa.cfm Iliyosomwa Tarehe 23 juni 2011 saa
                11:41
                                                                        14