Subcribe to our RSS feeds Join Us on Facebook Follow us on Twitter Add to Circles

Jumapili, 1 Februari 2015

MICHAKATO YA KIFONOLOJIA KWA UJUMLA.

IMEANDALIWA NA MANYAMA CHARLES

A) UTANGULIZI

i) Maana ya fonolojia
ii) Maana ya michakato ya kifonolojia

B) MICHAKATO YA KIFONOLOJIA

i) Kanuni ya kudondoshaji wa fonimu
ii) Kanuni ya uyeyushaji
iii) Kanuni ya tangamano la irabu
iv) Kanuni ya mvutano wa irabu
v) Kanuni ya ukakaishaji wa fonimu
vi) Kanuni ya usigano
vii) Kanuni ya muungano wa sauti
viii) Kanuni ya usilimisho

UTANGULIZI

Kwa mujibu wa Mgullu (1999) akimrejelea Fudge (1973) anasema kwamba fonolojia ni kiwango kimojawapo cha lugha fulani kilicho na vipashio vidogo zaidi kuliko vipashio vingine vyote vya lugha. Vipashio vya kifonolojia ni fonimu na alofoni zake.


Massamba (2010) anasema kuwa fonolojia ni tawi la isimu linalojishughulisha na mfumo wa sauti (asilia) za lugha. Hii inamaana kwamba, kila lugha mahususi ina mfumo wake wa sauti ambamo maneno hujengwa. Kiukweli fonolojia hujihusisha na namna sauti zinavyotumika katika maneno ya lugha mahususi katika kuleta maana.


Massamba na wenzake (2004) wanafafanua kuwa, fonolojia ni tawi la isimu ambalo hujishughusha na uchunguzi, uchambuzi na uainishaji wa sauti pambanuzi ambazo hutumika katika mifumo mbalimbali ya sauti za lugha za binadamu.


Tuki (2004) inaeleza kuwa mchakato ni mfululizo wa shughuli unaosababisha kitu fulani kufikiwa. Hivyo katika uwanja huu wa fonolojia tunaweza kusema kuwa mchakato utakuwa unafanyika pale ambapo mofimu mbili zinapokutanishwa huweza kutokeza mabadiliko fulani katika mofimu mojawapo au kutotokea badiliko lolote.


Hivyo basi tunaweza kusema kuwa fonolojia ni tawi la isimu ambalo hujishughusha na uchunguzi, uchambuzi na uainishaji wa sauti pambanuzi ambazo hutumika katika mifumo mbalimbali ya sauti za lugha za binadamu.


MICHAKATO YA KIFONOLOJIA

Kanuni ya udondoshaji wa fonimu hii inahusu kuachwa kwa sauti Fulani katika neno /matamshi wakati mofimu mbili zinapokabiliana. Katika mazingira hayo sauti ambayo hapo awali ilikuwepo hutoweka, irabu za Kiswahili hudondoshwa wakati kuna neno la ziada la irabu. Mfano:


muchumi - mchumi


muti- mti


mutoto- mtoto


Hivyo basi “U” imedondoshwa


Umbo la nje/ umbo la ndani


Muumba /mu+umb+ a/


Muumini /mu+umini/


Muuguzi /mu+ugu+z+i/


Mtu /mu+tu/


Kanuni ya uyeyushaji, wataalamu wengine huita irabu kuwa nusu irabu Mgullu (1999) Huu ni mchakato ambapo irabu za juu /u/ na /i/ hubadlika na kuwa /w/ au / j/ katika mazingira ya kufuatiwa na irabu zisizofana nazo. Kwa kifupi ni kwamba /u/ inapofuatiwa na irabu yoyote isiyofanana nayo hubadilika kuwa [w] na /i/ ikifuatiwa na irabu yoyote isiyofanana nayo hubadilika na kuwa [j].


Na sauti hizo hubadilika katika mazingira ya /u/ hubadilika kuwa [w] inapofuatana na irabu nyingine isiyofanana nayo na / i/ inabadilika na kuwa [ϳ] pia inapofuatana na irabu isiyofanana nayo. Mfano wa /u/

umbo la ndani/ umbo la nje

/mu+aminifu/

[mwe:mbamba]

/ku+enu/

[kwe:nu]

/mu+ anafunzi/

[mwa:nafunzi]

/mu+eupe/

[mwe:upe]
/mu+embe/

[mwe:mbe]

Hivyo tunaona wazi kabisa kuwa irabu ya juu nyuma /u/ imebadilika na kuwa kiyeyusho [w] katika mazingira ya kuathiriwa na irabu isiyofanana nayo ambayo ni /a/ na /e/ kwa hapo juu lakini hata ikiwa ni /o/ huweza kubadilisha. Kanuni /u/ [w] I = u. Hivyo tunaona kuwa irabu ya mbele /i/ hubadilika na kuwa [j] inapofuatana na irabu nyingine isiyofanana nayo ambayo ni /e,a na o/. Mfano wa irabu /i/


/umbo la ndani/ [umbo la nje]

/mi+embe/

[mje:mbe]

/mi+endo/

[mje:ndo]

/mi+ezi/

[mje:zi]

/mi+anzo/

[mja:nzo]

/mi+eusi/

[mwe:usi]

/mi+oyo/

[mjo:jo]

Kanuni ya ukaakaishaji wa fonimu kwa mujibu wa Mgullu (1999) akimnukuu Les (1984), anadai kuwa ukaakaishaji wa fonimu hutokea ambapo fonimu zisizo za kaakagumu zinapobadilika na kuwa za kaakagumu. Yeye anadai kuwa katika Kiswahili sauti za kaakagumu zipo mbili tu yaani /ɟ/ na /ʧ/ ambazo ni vizuio kwamizo. Hapa tunaona kwamba kipasuo cha kaakaalaini /k/ hubadili mahali pa matamshi na kuwa kizuio kwamizi /ʧ/ cha kaakaagumu katika mazingira ya kufuatiwa na sauti /ϳ/. Kanuni yake /i/ [ ] I = kisha inabadilika kuwa /k/ [ ] /i/ kwa mfano:


umbo la ndani

umbo la nje/ umbo la nje

/ki+enu/

[kjenui]

[ enu]

/ki+eusi/

[kjeusi]

[ eusi]

/ki+ombo/

[kjombo]

[ ombo]

/ki+umba/

[kjumba]

[ umba]

/ambaki+o/

[ambakjo]

[amba o]

Kanuni ya tangamano la irabu huu ni mchakato wa kiusilimisho baina ya irabu na irabu katika kuathiriana kiasi kwamba hulazimika kufuatana. Katika mchakato huu kinachotokea ni kwamba, kama irabu ya mzizi ni /i, u au a/ basi irabu ya kiambishi cha utendea lazima kiwe ni [i ] , wakati irabu ya mzizi ikiwa ni/ e au o/ katika hali ya utendea kiambishi chake kitakuwa ni [e]. Mfano:Iwapo mzizi wa kitenzi una irabu /e/ na /o/ mnyambuliko utakuwa na irabu /e/

(Som) -som+esh+a =somesha

(chok)-chok+esh+a =chokesha

(kop)-kop+esh+a =kopesha

Iwapo mzizi wa kitenzi una irabu /a/, /i/ na /u/ mnyambuliko utakuwa na irabu /i/

(pig)-pig+ish+a= pigisha

(lim)-lim+ish+a= limisha

(andik)-andik+ish+a= andikisha


Umbo ndani/umbo la nje

/imb+a/

[Imb-i-a]

/andik+a/

[andik-i-a]

/dak+a/

[dak-i-a]

/chun+a/

[ un-i-a]

/og+a/

[og-e-a]

/ ez+a/

[ ez-e-a]

/kom+a/

[kom-e-a]

Kanuni ya muungano wa sauti hii inahusu mabadiliko mengi yanayohusu irabu lakini ambayo yanahusu kudondoshwa au kugeuka kuwa kiyeyusho, pia upo uwezekano wa irabu ya mofimu moja kukabiliana na irabu ya mofimu nyingine kisha irabu hizo mbili zikaungana na kuzaa irabu moja tu. Mfano Umbo la nje 

 umbo la ndani

Wengi / wa+ingi/

Mengi / ma+ingi/

Meno / ma+ino/

Wengi / wa+izi/

Kanuni ya usilimisho kwa mujibu wa Habwe na Karanja (2004), wanaeleza kuwa usilimisho ni kule kufanana kwa fonimu kwa kiasi au kikamilifu kutokana na kuathiriana. Hapa sauti jirani katika neno huathiriana kiasi kwamba fonimu hupokea ama kupoteza sifa za kifonetiki kwa fonimu jirani, na matokeo yakiwa kuwa fonimu hizi hukabiliana sana katika kufanana kwa hiyo kuna usilimisho pamwe wa nazali kuathiri konsonanti na konsonanti kuathiri nazali kwa kawaida sauti n humainisha umoja inapatikaribia na herufi b husilimishwa na kuwa sauti nyingine kwa mfano:


Umbo la ndani umbo la nje

Ulimi /u+limi/

Ndani /n+limi/

Urefu /u+refu/

Ndefu /n+refu/

Mbao /n+bao/

Kanuni ya mvutano wa irabu, badiliko hili la mvutano wa irabu hutokea pale ambapo irabu mbili zinapokabiliana katika maneno, hususa ni irabu ya juu na ya chini. Irabu ya juu, huvutana na irabu ya chini matokeo ni kwamba tunapata irabu ambayo si ya juu wala ya chini bali ipo katikati ya irabu hizo. Kwa mfano, irabu /a/ ambayo ni ya chini inapokabiliana na irabu /i/ ambayo ni ya juu mvutano hutokea, hali ambayo hupelekea utokeaji wa irabu. Kwa mfano:

Umbo la ndani umbo la nje

Ma+ino meno

Wa+ingi wengi

Wa+itu watu

Kanuni ya usigano ni kinyume cha usilimisho, katika usilimisho baadhi ya sauti huathiriwa na sauti fulani na kuzifanya zifanane na sauti hizo. Lakini katika usigano sauti moja huchukua sifa fulani ili kutofautiana na sauti iliyo karibu nayo. Badiliko hili mara nyingi hutokea katika lugha za kibantu. Katika lugha ya Kiswahili inapoongezwa kwa maneno yenye sauti tangulizi ambayo si ghuna kwa mfano /k/ hubadilika na kuwa /g/ ambayo ni tofauti kabisa na kifonetiki.


Kuimarika kwa fonimu hili ni badiliko ambalo linahusu fonimu ambazo hutamkwa kwa kutumia nguvu kidogo zinapobadilika zinakuwa fonimu ambazo hutamkwa kwa kutumia nguvu nyingi kwa mfano kitambaza /l/ kinapobadilika na kuwa kipasuo /b/ katika neno /ulimi/. Neno ulimi lipo katika ngeli ya U-N, linatarajiwa katika wingi wa mofu (U) ya umoja libadilike na kuwa (N), lakini badala yake tunapata neno “ndimi”.


Fonimu /l/ huhitaji nguvu kidogo katika utamkaji lakini fonimu /d/ huhitaji nguvu nyingi kwa hivyo fonimu /l/ inapobadilika na kuwa fonimu /d/ katika wingi inasemekana kuwa fonimu /l/ imeimarika. Mfano:

Umbo la nje umbo la ndani fonimu iliyoimarika

Mwana mu+ana /u/ = /w/

Mwokozi mu+okozi /u/ = /w/

Myaka mi+aka /i/ =/j/

Kwao ku+ao /u/ =/w/

Kudhoofika kwa fonimu ni badiliko ambalo hutokea pale fonimu inayotamkwa kwa kutumia nguvu nyingi inapobadilika na kuwa fonimu inayotamkwa kwa kutumia nguvu kidogo kuliko ile ya awali, katika lugha ya Kiswahili badiliko hili hutokea zaidi katika nomino zinazoundwa kutokana na vitenzi. Fonimu /d/, /g/, /k/, /b/ huhitaji nguvu nyingi katika utamkaji ikilinganishwa na fonimu /z/, /s/, na /f/. kwa hivyo kutokana na mifano hiyo hapo juu ni bayana kuwa fonimu /d/, /g/, /k/, /b/ na /p/ zimedhoofika. Kwa mfano katika vitenzi vifuatavyo:

Umbo la ndani umbo la nje fonimu inayodhoofika

Mpendi mpenzi /d/ =/z/

Mnjengi mjenzi /g/ =/z/

Mpiki mpishi /k/ =/ʧ/

Mwibi mwizi /b/ =/z/

Ogopya ogofya /p/ =/f/

Unazalishaji wa irabu kwa mujibu wa Massamba (2011) anadai kuwa unazalishaji wa irabu ni aina ya usilimisho ambao irabu hupata sifa ya unazali kutokana na irabu yenyewe kutangamana na konsonanti ambayo ni nazali. Hivyo irabu nyingi hupewa sifa za unazali kutokana na ama kufuatiwa kwa nazali ama kutanguliwa na nazali. Na alama inayowakilisha unazalishaji ni alama ya kiwimbi [ ̴ ], hivyo sauti zote zilizowekewa alama ya kiwimbi ( ̴ ) zina unazali kwa sababu zimefuatana na nazali na hivyo zimefanywa kuwa unazali. Zaidi tuangalie mifano ifuatayo.Mifano


umbo la ndani umbo la nje

/nondo/

[nondo]

/penya/

[penya]

/mama/

[mama]

/ngambo/

[ ambo]

/nyumba/

[ umba]

/muwa/

[muwa]


HITIMISHO

Kwa hiyo tunaweza kusema kwamba mifanyiko ya kifonolojia huhusu mabadiliko ambayo hutokea pale ambapo fonimu mbili huambatana katika kuunda vipashio vikubwa kuliko fonimu (yaani silabi, mofu na maneno ). Mabadiliko hayo hutokea kwa sababu ya sauti moja kuathiri nyingine au sauti mbili kuathiriana katika mazingira maalum ya utokeaji, Kutokana na kuathiriana kwa fonimu za lugha na mabadiliko yanayojitokeza.


kuna kanuni ambazo zimeundwa na wanaisimu ijapo mabadiliko hayo huathiri mofu na maneno hujikita zaidi katika sifa za kifonolojia ambazo ni kama vile udondoshaji wa fonimu, mvutano wa irabu, tangamano la irabu, ukakaihsaji wa fonimu, uyeyushaji, kuimarika na kudhoofika kwa fonimu, usilimisho pamwe wa nazali na mengine mengi ambayo hatukuyasema katika uchambuzi watu wa michakato ya kifonolojia.


MAREJEO

Habwe, J. na Peter, K (2004) MISINGI YA SARUFI YA KISWAHILI. Phoenix Publisher. Nairobi.

Hyman, L.M. (1975) PHONOLOGY: THEORY AND ANALYSIS. New York HRW Press

Massamba, D.P.B. na wenzake (2004) FONOLOJIA YA KISWAHILI SANIFU (FOKISA): Sekondari na vyuo. Dar es salaam. TUKI

Massamba, D.P.B. (2010) PHONOLOGICAL THEORY: HISTORY AND DEVELOPMENT. Dar es Salaam. TUKI.

Mgullu, R.S. (1999) MTALAA WA ISIMU: FONETIKI, FONOLOJIA NA MOFOLOJIA YA KISWAHILI. Longhorn Publishers Ltd. Nairobi.

Matinde, S.R. (2012) DAFINA YA LUGHA ISIMU NA NADHARIA. Sekondari na vyuo vya kati na vyuo vikuu. Serengeti Educational Publishers Ltd.

TUKI, (2004) KAMUSI YA KISWAHILI SANIFU. Oxford University Press: Nairobi.
















Hakuna maoni:

Chapisha Maoni