Subcribe to our RSS feeds Join Us on Facebook Follow us on Twitter Add to Circles

Jumanne, 9 Septemba 2014

MAANA IBUKIZI KWA WAZUNGUMZAJI WA KISWAHILI ZAMA ZA UTANDAWAZI (MAANA YA KINGONOSHI).



                    Wazungumzaji wa Kiswahili wanaweza kuibua maana mbalimbali kulingana na wanavyotumia maneno. Maana hii huibuliwa mara nyingi na msikilizaji. Wakati msemaji akimaanisha maana fulani msikilizaji huweza kuibua maana ya ziada ambayo msemaji hajamaanisha. mtaalamu mmoja aliyaita maneno hayo ibukizi maneno ya kiungonoshaji. yaani nanafungamana na fikra za kingono. Ashakumu si matusi, maneno yatakayotumika ni makali zaidi kwani tumeyachukua jinsi yalivyo kutoka kwa wazungunzaji wa lugha.
      Yafuatayo ni baadhi ya maneno ya Kiswahili ambayo yakitumika kati ya wazungumzaji na wasikilizaji huweza kuibua maana ya ziada. Maneno haya  tutayaainisha kwa kuyatungia sentensi  na kufafanua utata wa maana zake.Kwa uhakika maneno haya hutumika katika mazingira ya kawaida lakini haijulikani ni kitu gani humsukuma msikilizaji kuibua maana ya ziada bada la ya maana ya msingi. Endelea
(i) Sentensi hizo ni kama ifuatavyo;
1.      Juma amemkata Asha jana.
Maana ya msingi; Juma ametumia kifaa chenye ncha kali kama vile sindano, kisu, panga na vinginevyo kumuweka jeraha mwilini mwa Asha.
Maana ibukizi; Juma amefanya mapenzi na Asha.
2.      Yeye alimwambia rose “naomba tigo
Maana ya msingi; Alimuomba Rose ampatie aidha vocha ya mtandao au kampuni ya mawasiliano ya tigo au laini ya tigo
Maana ibukizi; Yeye alimuomba Rose afanye naye mapenzi kinyume cha maumbile.
3. Nilipokuwa nasafiri kwa daladala kwenda mbagala nilisikia mama mmoja akimwambia kondakta wa daladala “nitakupa ikisimama”.
Maana ya msingi: Alimwambia atatoa nauli endapo gari litakuwa limesimama kituoni.
Maana inambukizi; ana kwamba watafanya nae mapenzi endapo uume utakuwa imesimama.
4.      Rafiki yangu aliniambia “atanipa mbele”.
Maana ya msingi; Rafiki yangu atanipa kitu fulani tulichoaidiana mbele ya safari tunapoelekea.
Maana ibukizi; Rafiki yangu atanipa sehemu ya mbele yaani uke au uume wakati tukifanya mapenzi.
5.      Naomba usinitie hapa tafadhali.
Maana ya msingi; Anaomba usimhusishe au usimjumuishe au kumuhusisha na tendo au tukio lolote.
Maana ibukizi; Anaomba usifanye naye mapenzi katika eneo hilo labda kwa sababu lipo wazi sana au halifai.
6.      Raheli alimwambia Kanyamaishwa kuwa  “ndizi yake” ni kubwa kuliko ya Jabiri.
Maana ya msingi; Tunda aina ya  ndizi alilokuwa nalo Kanyamaishwa lilikuwa ni kubwa kuliko la  Jabiri.
Maana ibukizi; Kanyamaishwa ana uume mkubwa kuliko wa Jabiri.
7.      Jamila ana shimo kubwa sana
Maana ya msiingi; Jamila ana sehemu  kubwa aliyoichimba kwenda chini kwa ajili ya kuweka vitu kama vile takataka.
Maana ibukizi; Jamila ana uke mkubwa sana (mpana)
8.      Amina alimwambia Jabiri kuwa “watafanya”.
Maana ya msingi; Wakikutana watatekeleza mambo fulani ya msingi waliyokuwa wameahidiana.
Maana ibukizi; Watakapo kutana hawatafanya mapenzi.
9.      Pita amemchoma Meri
Maana ya msingi; Pita ametumia kitu chenye ncha kali kwa kumjeruhi meri kama vile sindano.
Maana ibukizi; Pita amefanya mapenzi na Meri hadi akaridhika.
10.  Asha alimwambia Deo “leo umenifikisha kileleni”.
Maana ya msingi; Asha ailmwambia Deo kuwa leo amekwea naye hadi mwishoni mwa  kikomo au tamati ya mlima.
Maana ibukizi; Asha alimwambia Deo kuwa leo amefanya nae mapenzi akaridhika.
11.  Juma alimwambia Asha apanue aingize vizuri.
Maana ya msingi; Juma alimwambia  Asha afungue vizuri kitu kama mfuko au gunia ili aweke kitu fulani kwa uangalifu.
Maana ibukizi; Juma alimwambia Asha atanue vizuri miguu ili sehemu zake za siri yaani uke uonekane vizuri ili aingeze uume vizuri.
12.  Jana shangazi alimwambia mjomba achomoe taratibu.
Maana ya msingi; Shangazi alimwambia mjomba atoe kitu fulani kilichokuwa kimeingizwa mahali fulana kama vile msumari ukutani taratibu.
Maana ibukizi;  Shangazi alimwambia mjomba utoe uume wake taratibu kwenye uke wa shangazi.
13.  Daaa!!!! Rafiki yangu anamtambo mkubwa sana.
Maana ya msingi; Rafiki nyangu ana mashine kubwa sana ya kurahisishia kazi kama vile jenereta na n.k.
Mmana ibukizi; Rafiki yangu ana uume mkubwa.
14.  Jabiri amelala na Asha.
Maana ya msingi; Jabiri alipumzika pamoja na Asha kitandani au chini.
Maana ibukizi;  Jabiri alifanya mapenzi na Asha.
15.  Dada alimwambia kondakta “nikikaa vizuri nitakupa”.
Maana ya msingi; Dada atamwambia kondakta atampa nauli aliwa amekaa vizuri.
Maana ibukizi; Dada atampa konda uke akikaa vizuri.
16.  Siku hizi bakari anatembea na dada yangu.
Maana ya msingi; Bakari anaongozana na dada yangu katika matembezi yao.
Maana ibukizi; Bakari anamahusiano ya kimapenzi na dada yangu.
17.  Musa ameacha kusimamisha siku hizi.
Maana ya msingi; Musa ameacha tabia yake ya kuzuia kitu fulani kama vile gari, pikipiki au baisikeli visiendelee na safari.   
Maana ibukizi; Musa, uume wake haufanyi kazi kama mwanaume kamili.
18.  Yeye amemwagia Dada mbegu kichwani.
Maana ya msingi; Ina maana yeye alimmwagia nafaka kama vile mahindi, maharage na kadhalika kichwani.
Maana ibukizi; Yeye alimmwagia manii/ shahawa kichwani.
19.  Alinitaka sana mara ya kwanza nikakataa lakini mara ya pili nilikuballi.
Maana ya msingi; Kunihitaji tushirikiane naye sana katika kufanikisha jambo au mabo fulani aliyokuwa nayo mfano kazi.
Maana ibukizi; Kumwomba awe na uhusiano wa kimapenzi naye.
20.  Jana nilikunwa vizuri sana kuliko siku zote.
Maaana ya msingi; Jana alinikwangua kwangua au kunisugua sugua kwa kutumia kitu kama kucha au kijiti kuliko siku zote.
Maana ibukizi; Jana alinidhisha kimapenzi kuliko siku zote.
21.  Halima hatamwacha Munisi kwa sababu alimsugua vizuri.
Maana ya msingi; Munisi alimkuna / alimsugua vizuri alipokuwa anawashwa.
Maana ibukizi;  Halima alifanya naye mapenzi hadi aridhike
22.  Hapo mwanzo alitulia sana siku hizi anagawa sana.
Maana ya msingi; Alikuwa hatoi vitu kama vile msaada kwa watu.
Maaana ibukizi; Alikuwa hajihusishi na masuala ya mapenzi lakini kipindi hiki anafanya sana mapenzi kwa kila mtu.
23.  Pale nimepita lakini sijafurahi kabisa.
Maana ya msingi; Kuendelea na safari kwa kupitia njia ile ile lakini hufurahii safari.
Maana ibukizi; Kufanya mapenzi na mtu fulani bila kupata raha yoyote.
24.  Juma ndie aliyewabandua wale wasichana wawili.
Maana ya msingi; Kutoa mabango au vipeperushi vya wasichana wawili vilivyokuwa vimewekwa sehemu fulani kama kwenye mbao za matangazo.
Maana ibukizi; Juma ndiye aliyewatoa bikira wasichana wale wawili.
25.  Alipotoka pale alikuwa tayari kaloana.
Maana ya msingi; Nguo alizokuwa amevaa zilikuwa na majimaji.
Maana ibukizi; Alipotoka pale nguo zake zilikuwa zimeloa shahawa.
26.  Juma hajui kulenga mpaka aongozwe.
Maana ya msingi; Hana shabaha hadi aongozwe .
Maana ibukizi; Juma hawezi kuingiza uume wake kwenye uke hadi aongozwe.
27.  Ingawa ya kwangu ni nyembamba lakini ya kwake ni nene zaidi.
Maana ya msingi;  Maneno “ya kwake” na “ya kwangu” yanarejelea nomino yoyote iliyomo katiaka ngeli ya mofolojia ya nomino. Kwa mfano simu, nyumba, chupa na n.k.
Maana ibukizi; Maneno “ya kwangu” na “ya kwake” huweza kurejelea na kumaanisha sehemu za siri za mwanamke au mwnaume. (uke na uume)
28.  Leo nina hamu sana kwasababu nimemkosa siku nyingi.
Maana ya msingi; Nina shauku ya kumuona kwa sababu sijamuona siku nyingi.
Maaana ibukizi; Nina nyege naye za kufanya naye mapenzi kwa sababu sijafanya naye siku nyingi.
29.  Joni hupenda sana kuzama chumvini.
Maana ya msingi; Joni anapenda kuingia sehemu yenye majimaji yenye asili ya chumvi.
Maana ibukizi; Joni anapenda sana kunyonya au kulamba sehemu za siri za mwanamke yaani uke.
30.  Ingawa alinishughulikia vizuri sikuridhika.
Maana ya msingi; Ingaw alifanya haraka katika kufanikisha jambo fulani / kujitahidi kufanikisha jambo fulani.
Maana ibukizi; Ingawa alinipa mapenzi vizuri lakini sikiridhika
31.  Ingawa anamtaimbo mkubwa hawezi kuutumia
Maana ya msingi; Ingawa ana fimbo kubwa ya chuma ya kuvunjia miamba hawezi kuitumia.
Maana ibukizi; Ana uume mkubwa lakini hawezi kuutumia.
32.  Japokuwa amenichokonoa hakufanikiwa.
Maana ya msingi; Japokuwa alinidadisi kwa kuniuliza maswali lakini hakifanikiwakupata majibu aliyoyahitaji.
Maana ibukizi; Aliingiza uume au kidole kwenye uke bila kutimiza haja ya mwanamke.
33.  Jana alinikaza kuliko siku zote.
Maana ya msingi;  Jana alinifanyia uimara kuliko siku zote
Maana ibukizi;  Alinifanyia mapenzi mazuri kuliko siko zote
34.  Ingawa alimpa kidogo ila alikojoa sana.
Maana ya msingi;  Ingawa alipata kinywaji kidogo alienda haja ndogo mara nyingi.
Maana ibukizi;  Alitumia sehemu za siri (uke au uume) kidogo lakini alitoa shahawa nyingi.
35.  Aise! Siku hizi huoni mtu anayefyeka ovyo ovyo.
Maana ya msingi; Siku hizi huoni mtu anayejua kukata miti au  majani ili yawe mafupi ovyo ovyo.
Maana ibukizi; Siku hizi huwezi kuona mtu akifanya mapenzi na kila msichana bila kuchagua.
36.  Yeye ananimegea vizuri kuliko wewe.
Maana ya msingi; Yeye ananivunjia kitu au kunikatia kitu kinacholiwa vizuri kuliko wewe.
Maana ibukizi; Yeye alinipa mapenzi mazuri yasiyokuwa na choyo kuliko wewe.
37.  Kutokana na tundu lako dogo nilishindwa kutimiza haja yangu.
Maana ya msingi; Kutokana na uwazi mdogo mfano tundu la choo nilishindwa kutimiza haja yangu.
Maana bukizi; Kutokana na uke wako mdogo nilishindwa kufanya mapenzi vizuri nikatimiza haja yangu.
38.  Juma hupenda kunyonya maziwa kila siku kabla hajalala.
Maana ya msingi; Juma hupenda kunywa maziwa yaliyosindikwa katika pakiti au mifuko.
Maana ibukizi; Juma hupenda kunyonya matiti kila siku usiku.
39.  Jana yeye alimtafuna kutwa nzima.
Maana ya msingi; Jana alisaga kwa meno kitu fulani kutwa nzima.
Maana bukizi; Jana alifanya nae mapenzi siku nzima.
40.  Juma alipochomoa nilihisi maumivu makali.
Maana ya msingi; Juma alipotoa kitu kama sindano matakoni mwangu nilipata maumivu makali.
Maana bukizi; Juma alipochomoa uume kwenye uke nilihisi maumivu.
41.  Mama alimwambia dada kuwa “usafi unaanzia chini”.
Maana ya  msingi; Mama alimwambia dada usafi huanzia sehemu ya kawaida kabisa tenga katika ngazi ya chini.
Maana ibukizi; Mama alimwambia dada kuwa usafi unaanzia sehemu za siri yaani uke au uume.
42.  Ikiingia huwa ninasinzia.
Maana ya msingi; Ikipenya kuingia ndani kitu kama sindano ya usingizi huwa ninasinzia.
Maana ibukizi; Kila uume uingiapo ndani ya uke wangu huwa ninasinzia
43.  Alipoiweka ilizama yote.
Maana ya msingi; Baada ya kuingia au kuzama ndani ya kitu kama vile  kimiminika ilizama yote.
Maana ibukizi; Uume ulipoingia ndani ya uke ilizama yote.
44.  Kila nikifikia katikati huwa nndio ninapata utamu.
Maana ya msingi; Kila nikifika katikati ndio nanogawa kwa kitu au jambo.
Maana bukizi; Kila nikiingiza kwenye uke (katikati) ndio napata utamu.
45.  Wewe unapenda nyeti.
Maana ya msingi; Wewe unapenda kudeka
Maana bukizi. Wewe unapenda sehemu za siri ( uke au uume)
46.  Mchi wake unatwanga vizuri.
Maaana ya msingi. Kifaa chake cha  kutwangia vitu kama nafaka na madawa kwenye kinu unatwanga vizuri.
Maana ibukizi; Uume wake unaweza kufanya mapenzi vizuri.
47.  Akina mama huko mbele mtanipa. (aliuliza mgombea). Na akina baba je huko nyuma mtanipa.     
Maana ya msingi; Akina mama mliokaa mbele na akina baba mliokaa nyuma mtanipia kura.
Maana ibukizi;   Neno “mbele” na “nyuma” yana maana sehemu za  siri yaana “mbele” ni “uke” na “nyuma” ni “mkundu”.
48.   Sina hamu kabisa na yule kaka maana kitendo alichonifanyia huko nyuma sitakisahau kabisa.
Maana ya msingi: Sina hamu kabisa na yule kaka, kwani  kuni  jambo alilonifanyi hapo zamani sitalisahau kabisa.
Maana ibukizi: Sina hamu kabisa na yule kaka maana kitendo alichonifanyia kwenye matako/ mkundu sitakisahau.

49.  Jamaa wa lori alilazimishia mpaka akafanikisha  kumchomekea kwa mbele yule dada aliyekuwa anaendesha gari aina ya  Prado.
Maana ya msingi: Jamaa wa lori alilazimisha mpaka akafanikisha kutanguliza gari lake aina ya lori  katika nafasi ya mbele ya gari la yule dada  mwenye Prado.
Maana ibukizi: Jamaa wa lori alilazimisha mpaka akafanikisha  kuingiza uume wake katika uke wa dada yule mwenye  Prado.
50.  Dada  mwenye pikipiki  alimwambia yule kijana yule pale sheli, “ingiza vizuri pipe yako usije ukamwaga nje”.

Maana ya msingi: Dada mwenye pikipiki alimwambia yule kijana pale sheli, “weka mpaka ndani bomba la mafuta  usije ukamwaga mafuta nje.

Maana ibukizi: Dada mwenye pikipiki alimwambia yule kijana pale sheli,
“ingiza uume wako mpaka ndani usije akamwaga shahawa nje”.
 
(ii) Kutokana na data ya kwanya kategoria zinazongonoishwa zaidi ni pamoja na;
·         Vitenzi. Kwa  mfano choma, liwa , ingiza, chomoa ,liwa, tia, tiwa.
·         Nomino. Kwa mfano shimo, tundu, mtaimbo, mchi.
·         Vivumishi. Kwa mfano, yake nene, pana.
·         Vihusishi. Kwa mfano, ya kwake, ya Asha
Kategoria zinazongonoishwa zaidi ni vitenzi kwa sababu ndio msingi na muhimili wa sentensi. Vile vile ndio msingi unaobeba utendaji katika tungo.
Kategoria ambazo haziwezi kungonoshwa ni viunganishi na vielezi.
(iii) Wazungumzaji wa Kiswahili hupenda sana kuibua maneno kwa sababu hufikiria zaidi ya maana ya msingi ya neno husika kutokana na maendeleo ya sayansi na tekinolojia na kusababisha dhana ya ngono kukaa akilini mwa watu hasa vijana.
(iv) Kati ya msemaji na msikilizaji anayengonosha maneno yanayosemwa ni msikilizaji kwani yeye ndiye mlengwa na mfasiri wa dhana inayosemwa. Yeye ndiye anayetafuta maana ya lile lisemwalo.
(v) Hakuna ruwaza maalumu na dhabiti ya ungonoishaji.
(vi)  Kundi la watu wanaongonoisha zaidi ni kundi la vijana kwa misingi ya rika kwa sababu rika hili huwa na mawazo yalivofungamana zaidi na mambo ya ngono.
(vii) Anayeelewa maana ngonoshi za maneno ya Kiswahili ni wazungumzaji na watu waliofungamana na maana hizo za ngono. Wasioelewa maana ya ngonoshi ni wale ambao wapo nje ya muktadha  na rika hilo la vijana. Mfano baadhi ya wazee.
(viii) Katika taaluma ya isimu ungonoshi una mchango kama ufuatao;
·         Huonyesha uhusiano wa maana za maneno. Kwa mfano unaweza kujua ni neno lipi lina maana ya msingi na lipi lina maana ngonoshi.
·         Husidia katika kuonyesha ukubalifu wa maana za maneno kulingana na matumizi. Yaani neno linapata maana kutokana na jinsi linavyotumika, watumiaji wenyewe katika mzingira fulani.
·         Hutusaidia kupata maana za ziada. Kwa mfano neno “mbele” inaweza kuwa na maana ya “kutangulia” na maana ya ziada  ikawa  ni “sehemu za siri” yaani uke au uume.
Athari za maana ibukizi / ungonoishaji ni pamoja na;
·         Kwanza athari ni kupotosha maana ya msingi. Kwa mfano msemaji alikusudia kuomba kura kwa kusema “kina mama hapo mbele mtanipa” kama kuwauliza wanaompiga kura lakini wao wakapata maana potofu ya kuwaomba sehemu za siri yaani uke
·         Pili ni kuongeza uziada dufu katika lugha. Ungonoishaji huaongeza maana ya ziada katika neno. Maana isiyo ya msingi katika neno.
·         Tatu ni kuleta utata katika tungo. Kwa mfano “ikiingia huwa nafumba macho”. Mtu anaweza kujiuliza nini inayoingia.
·         Pia huibua mgogoro katika jamii. Kwa mfano msemajia anapomwambia msikilizaji (kwa mfano wa kike) ambaye hana mzoea naye utungo kama “unashimo kubwa”, kauli hii yaweza kuleta malumbano baina ya msemaji na msikilizaji.
·         Hupelekea uzalilishaji wa kijinsia.
(ix) Ungonoishaji wa maneno ya Kiswahili ni jambo jipya lililoibuka ingawa maneno yanayotumika yalikuwepo. Kimsingi maneno haya yalizingatia maana za msingi za maneno husika. lakini kutokana na maendeleo ya sayansi na tekinolojia pamoja na utandawazi maneno haya yameanza kupewa maana ya ziada inayofungamana na ngono yaani ungonoishaji. Na hii hutokana na mawazo ya watumiaji kufungamana na ngono.
(x) Suala la ungonoishaji ni suala la kukemewa na kubezwa kwani linapotosha maadili na uwezo wa kukamilisha mawasiliano na lengo lililokusudiwa. Kwa mfano kama mtu anafundisha anaweza kujikuta anachekwa baada ya kutumia neno liloibua dhana ya ungonoishi kwa wanafunzi au wasikilizaji. Hivyo suala hili likiendelezwa mwisho wake maana ya msingi imefifizwa na wanatumia maana ungongoshi tu.



Marejeo.
TUKI,  (2004), Kamusi ya Kiswahi Sanifu. Oxford University Press: Nairobi





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni