Subcribe to our RSS feeds Join Us on Facebook Follow us on Twitter Add to Circles

Jumatatu, 19 Mei 2014

UKUMUSHAJI


SWALI” Jadili dhana ya ukumushaji na sifa zake kwa kutumia mifano sahihi.

UKUMUSHAJI
Ni dhana ambayo hutoa maelezo zaidi au
Ya ziada kuhusu nomino, kivumishi, kitenzi, kielezi au kikundi cha maneno
KIKUMISHI
Ni neno , kirai au kishazi ambacho hutoa maelezo ya ziada kuhusu nomino, kivumishi, kitenzi, kielezi au kikundi cha maneno. Aidha, kikumushi huweza kuwa sentensi itoayo maelezo zaidi kuhusu sentensi nyingine.
Mfano.
Mtoto aliyekuja juzi ameondoka.
Katika sentensi hii kishazi tegemezi “ aliye kuja juzi” ni kikumushi ambacho kinatoa maelezo ya ziada kuhusu nomino “ mtoto:.
Mwanafunzi mrefu sana ameanguka.;
Neno “sana” ni kikumushi kinachotoa maelezo ya ziada kuhusu kivumishi “ mrefu”
Mifano zaidi
Gari lilikimbia kwa kasi sana
Maduhu anaimba vizuri mno
Ninapenda unavyosema.
Mwalimu aliye kwenda dukani jana amerudi.
Kimsing ukumushaji ni dhana pana zaidi ya uvumishi, kwani ukumushaji hutoa maelelezo zaidi kuliko uvumishaji. Pia kivumishi kipo katika kategoria ya kileksika lakini kikumushi kipo katika kategoria amilifu ya isimu miundo


MAZINGIRA YA UTOKEAJI WA UKUMUSHAJI
Ukumushaji unaweza kutokea baada ya nomino
Kwa mfano:
Kitabu kizuri kimepotea

Wanafunzi wapole wamefaulu mitihani yao vizuri

Askari katili ameuwa

Kijana mtiifu amezadiwa kitabu
Baada ya kiwakilsishi pia kikumishi kinaweza kutokea
Kwa mfano
Wale watundu wamefukuzwa shule

Yule msafi ameondoka chuoni
Kikumishi huweza kutokea baada ya kivumishi
Kwa mfano
Mwanafunzi mrefu kuliko wote ameanguka

Mwimbaji mashuhuri sana amekodiwa Uganda

Mwalimu mlevi kupindukia ameachishwa kazi.
Vivyo hivyo kikumishi huweza kutokea baada ya kielezi
Kwa mfano
Juma anaimba vizuri

Mbwa mkali amejeruhiwa sana

Ninapenda anavyocheza

Mwanariadha anakimbia kwa kasi
Ukumushaji vilevile huweza kutokea baada ya kielezi
Kwa mfano
Juma anaimba polepole mno

Mharifu amejitetea vizuri sana

Mwanafunzi amewasilisha kazi kwa ujasili mwingi
Ukumushaji pia huweza kutokea baada ya kihusishi
Kwa mfano
Janeth anakula wali kwa mkono

Juma amekaa juu ya meza

Maria analia kwa uchungu

SIFA ZA UKUMUSHAJI
Hutoa maelezo ya ziada kuhusu nomino, kivumishi, kitenzi au kikundi cha maneno
Mfano:
Mvulana mwembamba amepotea
Neno “ Mwembamaba” ni kikumushi kinachotoa maelezo ya ziada kuhusu nomino “ mvulana”
Kijana mnene sana anacheka.
Neno “sana” ni kikumushi kinachotoa maelezo ya ziada kuhusu “kivumishi” mnene
Ninapenda unavyocheza
Neno “ unavyocheza “ ni kikumishi kinachotoa malelezo ya ziada kuhusu “ kitenzi” “Ninapenda”.
Mwalimu aliyekuja jana asubuhi ameondoka.
Neno “aliyekuja jana asubuhi” ni kikumushi kinachotoa maelezo ya ziada kuhusu nomino “ mwalimu”
Mchungaji anahubiri vizuri sana
Neno “ sana” ni kikumushi kinachotoa maelezo ya ziada kuhusu kielezi “ vizuri”
Kikumushi kinaweza kuondolewa kwenye tungo bila kupoteza maana ya msingi ya tungo hiyo.
Mfano
Mtoto mzuri amerudi
mtoto amerudi
Ninapenda unavyokula
Ninapenda
kikumushi huweza kuundwa na neno moja au kikundi cha maneno.
Mfano
mtoto anacheza vizuri sana (neno moja)

Msichana aliyekaa mbele yangu ni msafi (kikundi cha maneno)

Kikumushi kipo katika kategoria amilifu ya isimu miundo ( mpangilio wa maneno katika tungo).
Mfano.
Msichana mrembo sana anacheka

Msichana mrembo anacheka
Kikumushi kinaweza kutokea mara moja au zaidi katika tungo
Mfano:
Ng’ombe aliyepotea jana asubuhi amepatikana leo asubuhi

Msichana anacheza vizuri sana na Baba analima vizuri sana.
Ukumushaji huweza kutokea kwenye kiima au kiarifu au pande zote kwa wakati mmoja
Mfano
Mvulana aliyetumwa kwenda kumletea mgonjwa dawa amerudi mapema mno.

Kijana aliyepotea jana ameonekana

Juma anatembea kwa madaha sana
Ukumushaji huweza kutokea katika sentensi changamano ambapo kishazi tegemezi huchukua nafasi ya kikumushi
Kwa mfano
Kijana aliyekuja jana ameondoka leo asubuhi

Mbuzi aliyezalia porini ameletwa nyumbani

Kitabu kilichoibiwa kimerudishwa

Nyimbo zilizoimbwa zinafurahisha
Kwa ujumla dhana ya ukumushaji na uvumishaji kwa jinsi tulivyojadili ni dhana ambazo zinafanana katika utendaji kazi wake lakini upekee wa ukumushaji ni kwamba huweza kutokea katika kikundi nomino pekee.
Hivyo basi ukumushaji ni mpana zaidi kuliko uvumishaji.



MAREJELEO
Matinde, S.R (2012) Dafina ya lugha, Isimu na Nadharia, Mwanza: Serengeti Educational Publishers (T) Ltd
Habwe, J na Karanja, P, (2004). Misingi ya sarufi ya Kiswahili; Nairobi- Kenya: phoenix publishers Ltd

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni