Subcribe to our RSS feeds Join Us on Facebook Follow us on Twitter Add to Circles

Jumapili, 18 Mei 2014

MOFOLOJIA YA KISWAHILI.



Mofolojia ya Kiswahili


Mofolojia ya kiswahili


· Malengo ya somo hili • Kueleza na kufafanua maana ya mofolojia • Kutambua na kufafanua zaidi mofolojia na vipashio vyake.


· Kunihusu mimi • STEPHEN MANYAMA CHARLES • MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA ARUSHA,NI MWALIMU-MWANAFUNZI WA SOMO LA KISWAHILI KWA VYUO NA SEKONDARI,Karibuni kwa Mchango na Mawazo na hata kwa kujifunza pia.

· Utangulizi • Maana ya mofolojia


· Maana ya mofolojia • Mofolojia ni tafsiri ya neon la kiingereza “Morphology”. Neno hili nalo linatokana na neon la kiyunani “Morphe” lenye maana ya muundo au umbo ( Aurbach et al 1971; 106). • Mofolojia ni neno linalotumiwa kumaanisha utanzu wa isimu unaoshughulikia muundo wa maneno ( Habwe na Karanja 2004).


· Maana.......... • Hartman (1972). Mofolojia ni tawi la sarufi ambalo hushughulika na uchunguzi na uchambuzi wa maumbo, fani na aina za maneno yalivyo sasa pamoja na historia zake


· Maana......... • Kwa ujumla mofolojia ni taaluma inayoshughulikia lugha pamoja na mpangilio wake katika uundaji wa maneno. Vipashio hivyo vya lugha huitwa mofimu


· Uhusiano uliopo kati ya mofolojia na matawi mengine ya sarufi • Mofolojia na fonolojia • Kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya mofolojia na fonolojia:i. Vipashio vya kifonolojia ndivyo hutumika katika kuunda vipashio vya kimofolojia mfano


· Mofolojia na fonolojia • Vipashio vya mofolojia ni fonimu, mfuatano wa fonimu ndio huuna vipashio vya kimofolojia ambavyo ni mofimu Mfano • Fonimu: i, p, t, a, huunda • mofimu: Pit-a • Hivyo basi neno pita limeundwa na mofimu mbili na fonimu nne


· Mofolojia na fonolojia ii) Uhusiano mwingine kati ya fonolojia na mofolojia ni kwamba, kanuni za kifonolojia hutumika kueleza maumbo ya kimofolojia ambayo yanaathiriana. Mfano Katika neno mu-ana mwu-alimu


· Mofolojia na fonolojia • Kipashio [mu] katika mifano hapo juu kinajitokeza kama [mw-] inapofuatwa na irabu ambayo. Mu mw-/-I


· Neno hutumika kuundia sentensiØMofolojia na sintaksia i. Vipashio vya msingi vya kimofolojia ndivyo hutumika katika kuundia daraja hili la sintaksia.·


Mwisho kwa asante usomaji Mawasiliano: charlesmanyama@rocketmail.com,0768326604 ©2014

· Maswali na majibu • Kwa maswali au mchango wowote kuhusuiana na kiswahili nifuate kwenye email yangu ya charlesmanyama@rocketmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni