Subcribe to our RSS feeds Join Us on Facebook Follow us on Twitter Add to Circles

Alhamisi, 22 Mei 2014

FASIHI KWA UJUMLA.


Fasihi Simulizi

Fasihi Simulizi ni utanzu wa fasihi ambao unawakilisha sanaa ya lugha inayopitishwa kutoka kwa kizazi hadi kizazi kwa njia ya maneno/masimulizi ya mdomo.

Sifa za Fasihi Simulizi

  1. Hupitishwa kwa njia ya mdomo
  2. Ufanisi wa sanaa katika fasihi simulizi hutegemea uwezo wa msimulizi, au wahusika
  3. Masimulizi yake yanaweza kuathiriwa na mazingira, hisia na hali
  4. Ni mali ya jamii. Hakuna mtu fulani anayemiliki sanaa katika fasihi simulizi.
  5. Inaweza kubadilika kutoka kizazi hadi kizazi, au mazingira mbalimbali kwa sababu hutegemea kumbukumbu ya msimulizi.
  6. Aghalabu huwa na funzo fulani

Umuhimu wa Fasihi Simulizi

  1. Kuburudisha - Hufurahisha na kuchangamsha hadhira
  2. Kunasihi- kutolea mawaidha na kuonyesha mwelekeo unaotarajiwa katika jamii
  3. Kuelimisha watu kuhusu vitu mbalimbali hasa mazingira yao
  4. Kutambulisha jamii - jamii mbalimbali husifika kutokana na sanaa zao katika fasihi simulizi kama vile nyimbo
  5. Kuhifadhi na kudumisha utamaduni wa jamii
  6. Kuunganisha watu - huleta watu pamoja
  7. Kukuza lugha - fasihi huimarisha lugha kwa kuwa hutumia mbinu mbalimbali za lugha.
  8. Kuliwaza - hutoa huzuni na kuleta matumaini.
  9. Kupitisha muda - wakati mwingine fasihi simulizi hutumika kupitisha muda.

Fasihi Andishi



Fasihi Andishi ni aina ya sanaa ambayo hutumia maneno yaliyoandikwa kupitisha ujumbe. Ni sanaa inayopitishwa kwa njia ya maandishi

Tanzu za Fasihi Andishi

Kuna tanzu nne kuu za Fasihi Simulizi:
  1. Hadithi Fupi - kazi andishi ya fasihi isiyokuwa ndefu sana
  2. Riwaya - kazi andishi ya fasihi ambayo huwa ndefu kuliko hadithi fupi
  3. Tamthilia- kazi andishi ya fasihi inayowasilisha mchezo wa kuigiza
  4. Mashairi - mashairi yaliyochapishwa huwa chini ya fasihi andishi.

Sifa za Fasihi Andishi

  1. Hupitishwa kwa njia ya maandishi
  2. Ni mali ya mtu binafsi
  3. Haiwezi kubadilishwa
  4. Hutumia mbinu za lugha na mbinu za sanaa

Umuhimu wa Fasihi Andishi

  1. Kuhifadhi kazi ya sanaa katika maandishi
  2. Kukuza lugha
  3. Kuburudisha
  4. Kuelimisha
  5. Kukashifu tabia zisizoandamana na maadili ya jamii
  6. Kuonya, kuelekeza, kunasihi

Uchambuzi wa Fasihi Andishi

Unapochambua kazi ya fasihi andishi zingatia:

Aina ya Kazi Andishi

  • Tambua aina au kipera cha kazi andishi ikiwa ni riwaya, hadithi fupi au tamthilia

Wahusika

  • Tambua wahusika katika kazi hiyo ya fasihi
  • Fafanua sifa za kila mhusika kwa kutumia vivumishi au virai vivumishi vinavyolingana na hulka za mhusika huyo.
  • Aidha, unapaswa kuyakinisha sifa hizo kwa kutolea mifano kutoka kwenye hadithi
  • Taja aina ya wahusika

Maudhui na Dhamira

  • Maudhui - ni nini kinachofanyika?
  • Dhamira - lengo/kusudi la kazi hiyo ni nini?

Mandhari

  • Hadithi inafanyika katika mazingira gani?
  • Mazingira hayo yanachangia vipi katika kisa hicho au sifa za wahusika?
  • Msanii ameunda hali gani? (hisia, n.k)

Mbinu za Lugha

  • Taja kwa kutolea mifano, fani za lugha zilizotumika ili kuifanya lugha iwe ya kuvutia zaidi
  • Fafanua mbinu za sanaa zilizotumika na utaje mifano mwafaka




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni