Subcribe to our RSS feeds Join Us on Facebook Follow us on Twitter Add to Circles

Jumanne, 4 Novemba 2014

FONOLOJIA YA KISWAHILI





UTANGULIZI USULI WA TAALUMA YA FONOLOJIA 
Neno fonolojia linatokana na maneno mawili ya Kigiriki phone-sauti za kusemwa na logos- taaluma/mtalaa. Masimulizi yanadai kuwa taaluma hii ilianza zamani sana kati ya mwaka 460 kabla ya Masihia huko India ya kale, ambapo mtu aliyeitwa Panini, na ambaye huaminika kuwa ni baba wa isimu aliandika kuhusu fonolojia ya Kisansikriti katika matini aliyoiita Shiva Sutras. Ni katika andiko hili ndipo alipobainisha kuwepo kwa dhana ambazo leo hii hujulikana kama fonimu, mofimu na mzizi. Baada ya andiko hilo, habari za taaluma ya fonolojia ni kama zilipotea kabisa katika uwanja wa isimu hadi ilipofika karne ya 19 ambapo wanaisimu wengine waliibuka na kuzungumzia upya masuala ya fonolojia. Miongoni mwa wanaisimu wa mwanzo wanaotajwa kujihusisha na fonolojia ni Mpolandi "Jan Baudouin de Courtenay" , (pamoja na mwanafunzi wake wa zamani "Mikołaj Kruszewski" alipobuni neno fonimu mnamo mwaka 1876, na kazi yake, ijapokuwa hairejelewi sana, inachukuliwa kuwa ni mwanzo wa fonolojia mamboleo. Mwanaisimu huyu si tu alishughulikia nadharia ya fonimu, bali pia vighairi vya kifonetiki (ambavyo leo huitwa alofoni na mofofonolojia). Maandishi ya Panini (Sarufi ya Kisanskriti) pamoja na Jan Baudouin de Courtenay yalikuja kuwa na athari kubwa kwa anayeaminika kuwa baba wa nadharia ya Umuundo Mamboleo, Ferdinand de Saussure, ambaye pia alikuwa ni profesa wa Sansikriti. Wanaisimu wote hawa walikuwa wanajaribu kulinganisha sauti za lugha za Asia Mashariki na za Ulaya, lengo lao likiwa ni kujua mizizi ya lugha zilizoitwa India-Ulaya. Kutokana na mkabala huo, katika kipindi hicho isimu ilikuwa Isimu-linganishi tu. Kutokana na tafiti zao hizo waliweza kupata maneno yenye sauti na maana zilizolingana, kufanana au kukaribiana. Utafiti huo uliweza kugundua jamii mbili za lugha ambazo ni jamii ya lugha za Kirumi na jamii ya lugha za Kijerumani. Baadhi ya wanaisimu mahususi kabisa wanaokumbukwa kuchangia katika maendeleo ya fonolojia ni pamoja na: (i) Jan Baudouin de Courtenay (1845-1929) Kama ilivyoelezwa hapo awali, huyu ni mwanaisimu aliyebuni dhana za foni na fonimu. Katika nadharia yake, alidai kuwa sauti za mwanadamu ni za aina mbili—foni na fonimu.  Alisema kuwa foni ni sauti za kutamkwa tu lakini fonimu ni sauti za lugha. Hata hivyo, de Courtenay hakutumia istilahi za foni na fonimu (kama zinavyotajwa sasa) bali alitumia istilahi za anthrophonics—foni na psychophonics—fonimu. Yeye alidai kuwa foni zipo karibu sana na taaluma ya kumuelewa binadamu pamoja na alasauti zake ambazo kwa hakika hutofautiana sana na za wanyama wengine. Na kuhusu fonimu, alidai kuwa zinahusu kumwelewa binadamu pamoja na akili zake na namna anavyofikiri katika akili yake. Alidai kuwa, mara nyingi, binadamu hupokea kinachotamkwa na kufasiliwa. (ii) Ferdinand de Saussure (1887-1913) Ni mwanaisimu wa Kiswisi anayejulikana kama baba wa isimu kutokana na mchango wake alioutoa katika taaluma hii. Yeye anakumbukwa zaidi kutokana na uwezo wake wa kutofautisha dhana alizoziita langue—mfumo wa lugha mahsusi na parole—matamshi ya mzungumzaji wa lugha husika. Langage hufafanuliwa kuwa ni uwezo alionao mzungumzaji wa lugha mahususi wa kuzungumza na kuelewa matamshi ya mzungumzaji mwingine wa lugha hiyohiyo. Ni sehemu ya lugha inayowakilisha maarifa kati ya sauti na alama. Ni mfumo wa alama kwa maana ya kiufundi tu. Dai lake la msingi ni kuwa alama inategemea vitu viwili—kitaja na kitajwa—hivyo ili mawasiliano yafanyike, mfumo wa ishara lazima ufahamike na ukubaliwe na wanajamii wote. Kwa upande wa parole, anadai kuwa ni matendo uneni. Ni namna lugha inavyotamkwa katika hali halisi na mtu mmoja mmoja. Dhana ya parole inalingana na dhana ya performance (utendi) ya Noam Chomsky. Katika lugha, parole ni matamshi tofauti ya sauti moja—alofoni. Wanaisimu wanaonekana kukubaliana na madai ya Saussure kwakuwa inaelekea kuthibitika kuwa hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya kitaja na kitajwa [alama (lugha) na kinachowakilishwa (masilugha)], bali makubaliano baina ya wazungumzaji wa lugha moja husika ndiyo hutawala. (iii) Nikolai Trubetzkoy (1890-1939) Ni miongoni mwa waanzilishi wa taaluma ya fonolojia akichota mizizi ya taaluma ya isimu kutoka katika Skuli ya Prague. Mwanaisimu huyu aliandika misingi ya fonolojia kwa kutumia maarifa yaliyoibuliwa na Ferdinand de Saussure. Ni mtaalamu wa kwanza kufasili dhana ya fonimu. Aliandika vitabu vingi kwa lugha ya Kijerumani, miongoni mwake ni Grundzüge der Phonologie (Principles of Phonology, 1939), ambapo ni katika kitabu hicho ndimo alimotoa fasili ya fonimu pamoja na kubainisha tofauti baina ya fonetiki na fonolojia. (iv) Noam Chomsky (1928-) Huyu ni mwanaisimu wa Kimarekani anayevuma sana kwa mchango wake katika taaluma ya isimu kwa ujumla. Dhana za competence (umilisi) na perfomance (utendi) zimemfanya awe maarufu ulimwenguni. Dhana hizi zinaelezea tofauti baina ya maarifa na udhihirishaji wa maarifa hayo ya mtumiaji wa lugha. Katika fonolojia, Chomsky anakumbukwa kwa ufafanuzi wake wa dhana ya fonimu kwa mtazamo wa kisaikolojia. Anapochunguza dhana hii, hudai kuwa fonimu ni tukio la kisaikolojia, hivyo fonimu zimo kichwani mwa mzungumzaji wa lugha. (v) Daniel Jones (1881-1967) Ni mwanafonetiki kinara na maarufu kabisa katika nusu ya kwanza ya karne ya ishirini. Ni Mwingereza msomi ambaye alikuwa na shahada ya kwanza ya hisabati na shahada ya mahiri ya sheria, shahada ambazo hata hivyo, hakuwahi kuzitumia. Baadae, alisomea lugha na kuhitimu shahada ya uzamivu. Daniel Jones alifunzwa fonetiki na maprofesa mbalimbali, japokuwa aliathiriwa zaidi na Paul Passy na Henry Sweet. Hamu yake kuu ilikua kwenye nadharia ya fonetiki. Anafahamika zaidi kwa ufafanuzi wa dhana ya fonimu kwa mtazamo wa kifonetiki (ufafanuzi wake tutauchunguza katika sehemu ya mitazamo ya dhana ya fonimu).       FONETIKI NA FONOLOJIA Fasili ya taaluma ya fonolojia haiwezi kukamilika, na pengine kueleweka, iwapo hakuna linalosemwa kuhusiana na taaluma ya fonetiki. Hali hii inatokana na ukweli kuwa kuna uhusiano wa kinasaba kati ya fonolojia na fonetiki. Massamba na wenzake (2004:5) wananeneleza ukweli huu kwamba: …fonetiki na fonolojia ni matawi mawili tofauti ya isimu lakini yenye kuhusiana sana. Uhusiano wa matawi haya unatokana na ukweli kwamba yote mawili yanajihusisha na uchunguzi na uchambuzi unaohusu sauti za lugha za binadamu. Kutokana na ukweli huu, jitihada za kufasili dhana ya fonolojia inaelekea kuwa nyepesi, dhana hizi mbili zinapofasiliwa kwa mlinganyo. Tuanze na fonetiki: FONETIKI NI NINI? Fonetiki ni tawi la isimu linalochunguza sauti za kutamkwa na binadamu ambazo huweza kutumika katika lugha asilia. Massamba na wenzake (kama hapo juu) wanafasili fonetiki kuwa ni tawi la isimu linalohusika na uchunguzi na uchambuzi wa taratibu za utoaji, utamkaji, usafirishaji, usikiaji, na ufasili wa sauti za lugha za binadamu kwa ujumla. Wanasisitiza kwamba, kinachochunguzwa katika fonetiki ni [maumbo] mbalimbali ya sauti zinazoweza kutolewa na alasuti za binadamu (yaani sauti za binadamu zinazotamkwa tu). Kipashio cha msingi cha uchambuzi wa kifonetiki ni foni. Foni ni sauti yoyote inayotamkwa na binadamu na inayoweza kutumika katika lugha fulani. Hivyo basi, foni ni nyingi sana na hazina maana yoyote. Wanafonetiki hudai kuwa foni zimo katika bohari la sauti (dhana dhahania) ambalo kila lugha huchota sauti chache tu ambazo hutumika katika lugha mahususi. Sauti chache zinazoteuliwa na lugha mahususi kutoka katika bohari la sauti huitwa fonimu. Matawi ya Fonetiki: Kuna mitazamo miwili tofauti kuhusiana na matawi ya fonetiki. Mtazamo wa kwanza ni unaodai kuwepo matawi matatu; na mtazamo wa pili ni unaodai kuwepo matawi manne. Mtazamo wa kuwepo matawi matatu unataja fonetiki matamshi, fonetiki akustika, na fonetiki masikizi. Mtazamo wa kuwepo matawi manne (kama Massamba na wenzake (kama hapo juu), pamoja na matawi tuliyokwisha yataja, wanongezea tawi fonetiki tibamatamshi. Fonetiki matamshi huchunguza jinsi sauti za lugha zinavyotamkwa kwa kutumia alasauti. Hususani, huchunguza namna na mahali pa kutamkia sauti husika. Fonetiki akustika huchunguza jinsi mawimbi ya sauti yanavyosafiri kutoka katika kinywa cha mtamkaji hadi kufika katika sikio la msikilizaji. Fonetiki masikizi hujihusisha na mchakato wa ufasili wa sauti za lugha, hususani uhusiano uliopo baina ya neva za sikio na za ubongo. Na fonetiki tibamatamshi ni tawi jipya lililozuka mwanzoni mwa karne hii, ambalo huchunguza matatizo ya utamkaji ambayo binadamu huweza kuzaliwa nayo au kuyapata baada ya kuzaliwa. Ni tawi linalojaribu kutumia mbinu za kitabibu kuchunguza matatizo na kutafuta namna ya kuyatatua. FONOLOJIA NI NINI? Fonolojia ni taaluma ya isimu inayochunguza mifumo ya sauti za kutamkwa zinazotumika katika lugha asilia mahususi za binadamu. Inapolinganishwa na fonetiki, inasisitizwa kuwa fonolojia ni tawi la isimu linalochunguza mifumo ya sauti za lugha mahususi tu, kama vile sauti za Kiswahili, Kiingereza, Kigogo, n.k. Hata hivyo, wapo wanaisimu wanaoelekea kukubaliana kuwa kuna fonetiki ya lugha mahususi pia, na kuna fonolojia ya jumla, na fonetiki ya lugha mahususi. Mathalani, Massamba (1996) licha ya kufasili fonolojia kuwa ni taaluma ya isimu inayochunguza mfumo wa sauti za lugha mahususi, anaenda mbele zaidi na kudai kuwa fonolojia inaweza kuchunguza sauti kwa ujumla wake bila kuzihusisha na lugha mahususi. Akmajian na wenzake (2001), nao wanadokeza msimamo kama wa Massamba wanapodai kwamba fonolojia inaweza kuchunguzwa kwa mitazamo miwili tofauti. Kwanza, fonolojia kama tawi dogo la isimu linalochunguza mfumo na ruwaza za sauti za lugha mahususi ya binadamu; na pili, fonolojia kama sehemu ya nadharia ya jumla ya lugha ya binadamu inayohusika na tabia za jumla za mfumo wa sauti za lugha asilia za binadamu. Katika mhadhara huu, hata hivyo, tutakuwa wafuasi wa mtazamo unaoona kuwa fonolojia ni tawi la isimu linaloshughulikia mfumo wa sauti za lugha mahususi, hivyo tuna, kwa mfano, fonolojia ya Kiswahili, fonolojia ya Kiingereza, fonolojia ya Kiha, fonolojia ya Kihehe, na fonolojia ya Kibena. Kipashio cha msingi cha fonolojia ni fonimu. FONIMU Ni kipashio kidogo kabisa cha kifonolojia kinachoweza kubadili maana ya neno. Hivyo basi, fonimu ina maana, kwakuwa inaweza kubadili maana ya neno inapobadilishwa nafasi katika neno husika. Foni chache zilizoteuliwa kutoka katika bohari la sauti ili zitumike kwenye mfumo wa sauti za lugha mahususi ndiyo fonimu. Hivyo, fonimu ni chache ikilinganishwa na foni. Idadi ya fonimu za lugha hutofautiana kati ya lugha moja na nyingine. Mathalani, Kiarabu kina fonimu ishirini na nane (28), Kiswahili kina fonimu thelathini (30), Kifaransa kina fonimu thelathini na tatu (33), na Kiingereza kina fonimu arobaini na nne (44). Sauti ambayo huweza kubadilishwa nafasi yake katika neno lakini maana ikabaki ileile huitwa alofoni. Alofoni ni kipashio cha kifonolojia kinachotaja hali ambapo fonimu moja hutamkwa na kuandikwa tofautitofauti bila kubadili maana ya neno. Mfano: Fedha na feza Sasa na thatha Heri na kheri Kwa kifupi, alofoni ni matamshi tofautitofauti ya fonimu (sauti) moja. MITAZAMO YA DHANA YA FONIMU Juhudi za kufasili dhana ya fonimu zilizofanywa na wanaisimu mbalimbali zimezua mitazamo mbalimbali ya namna ya kuchambua dhana hii. Hadi sasa, mitazamo mitatu ifuatayo ndiyo hujulikana zaidi. Fonimu ni Tukio la Kisaikolojia Huu ni mtazamo uliokuzwa na kutetewa na wanasarufi geuzi-zalishi, mwanzilishi wake akiwa ni Noam Chomksy. Kwa mujibu wa mtazamo huu, fonimu ni dhana iliyo katika akili ya mzungumzaji wa lugha. Mtazamo huu unadai kuwa kila mzungumzaji wa lugha ana maarifa bubu ya idadi na jinsi ya kutamka fonimu za lugha yake. Chomsky anayaita maarifa haya kuwa ni umilisi (competence). Anadai kuwa maarifa haya ya fonimu hufanana kwa kiasi kikubwa miongoni mwa wazungumzaji wa lugha moja husika. Kinachotofautiana ni jinsi ya kudhihirisha (kutamka)  fonimu hizo, yaani utendi (perfomance). Chomsky anabainisha kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kuhitilafiana baina ya umilisi na utendi kutokana na matatizo mbalimbali ambayo mzungumzaji hukabiliana nayo. Matatizo hayo ni kama vile uchovu, ulemavu wa viungo vya matamshi (alasauti za lugha), athari za mazingira, ulevi, na maradhi. Hivyo, kutokana na hali hii, fonimu hubaki kuwa tukio la kiakili, yaani kisaikolojia tu. Fonimu ni Tukio la Kifonetiki Wafuasi wa mtazamo huu wanaongozwa na Daniel Jones. Daniel Jones anaiona fonimu kuwa ni [umbo] halisi. ..........................Inaendelea

MOFOFONEMIKI YA KISWAHILI


Katika mada hii tumeangalia fasili ya mofofonemiki kwa mujibu wa wataalam mbalimbali, kisha tukaangalia kwa ufupi historia ya nadharia ya mofofonemiki na katika kiini cha mada tumejadili sababu zilizopelekea kuibuka kwa nadharia ya mofofonemiki. Kwa kuanza na fasili ya mofofonemiki  kwa mujibu wa mtandao wa Wikipedia wanafafanua mofofonemiki kuwa ni tawi la isimu linalojishughulisha na mwingiliano wa michakato ya kimofolojia na kifonolojia au kifonetiki. Pia hujishughulisha na mabadiliko ya sauti yanayotokea katika mofimu wakati zinapoungana kuunda maneno. (Tafsiri yetu). fasili hii ina mapungufu fulani kwani, mofofonemiki haijishughulishi na michakato yote ya kifonolojia na kimofolojia bali ni baadhi tu ya michakato hiyo ambayo ilishindwa kufafanuliwa kwa kutumia data za kifonolojia au kifonetiki peke yake. The New Oxford American Dictionary inafafanua kwamba, mofofonolojia/mofofonemiki ni tawi la isimu linalojishughulisha na uwakilishi wa kifonolojia wa mofimu. Hivyo basi tunaweza kusema kuwa, mofofonemiki ni tawi la isimu linaloshughulikia matumizi ya kimofolojia katika kueleza baadhi ya tofauti za kifonolojia ambazo isingewezekana kuzielezea kwa kutumia data za kifonetiki au kifonolojia peke yake. Baada ya kuangalia fasili ya neno mofofonemiki ifuatayo ni historia fupi ya nadharia ya mofofonemiki. Kwa mujibu wa Massamba (2010:82) akimrejelea Martnet (1965) anafafanua kwamba, istilahi hii mofofonemiki/mofofonolojia ilipendekezwa kwa mara ya kwanza na N.S. Trubetzkoy (1929). Trubetzkoy alitumia istilahi hii kwa maana ya tawi la isimu ilinaloshughulikia matumizi ya mafolojia katika kuelezea baadhi ya tofauti za kifonolojia ambazo isingewezekana kuzielezea kwa kutumia data za kifonolojia au kifonetiki peke yake. Baada ya kuangalia historia fupi ya mofofonemiki yafuatayo ni mambo yaliyosababisha kuibuka kwa nadharia ya mofofonemiki. Kuchunguza ubadilikaji wa sauti ambao usingeweza kuelezwa kwa kutumia data za kifonolojia peke yake. Baadhi yao wakapendekeza kuwapo kwa kiwango cha kimofofonemiki pamoja na kipashio umbo kiini kama kiwakilishi cha mofimu, kwa hiyo walipendekeza hivyo baada ya kushindwa kujua ipi ni alofoni ya fonimu ipi kwa kutumia kigezo cha kifonetiki pekee  Kwa mfano;  walishindwa kujua /k/ ni alofoni ya /c/ au /c/ ni alofoni ya /k/ Kwa mfano hata katika lugha ya kurusi –                                             ruka = “mkono”                                             ručnoj = “a mkono”                                              Mzizi ni – ruk na ruč Wanamofofonemiki walichunguza wakagundua kuwa katika mazingira fulani /k/ hubadilika kuwa /č/ baada ya kufuatiwa na “noj”. Hivyo wakapendekeza umbo kiini la maneno haya ni ruKa au ruČnoj umbo kiini lake lilitambulika kama {K} au {Č} Katika lugha ya Kiswahili kuna mabadiliko ya sauti yanayotokea katika baadhi ya maneno baada ya sauti fulani kufuatiwa na kiambishi cha unominishaji (i) kwa mfano katika maneno yafuatayo;                    Fuata – fuasi                    Penda – Penzi                    Cheka – Cheshi                    Pika – Pishi Pia wanamofofonemiki walichunguza ubadilishanaji huu wa sauti kwani walishindwa kujua ipi ni alofoni ya fonimu ipi. Ndipo wakagundua kuwa katika mazingira fulani /t/ hubadilika kuwa /s/ baada ya kufuatwa na mofimu ya unominishaji “i” pia sauti /d/ hubadilika na kuwa /z/ baada ya kufuatwa na mofimu ya unominishaji “i” Baada ya kupendekeza umbo kiini maneno haya yakaandikwa kama ifuatavyo: kwa mfano neno {fuaTa} umbo {T} likawa umbo kiini ambalo linawakilisha sauti zote mbili yaani /t/ na /s/, pia neno {piKa} umbo kiini lake ni {K} ambalo linawakilisha sauti /k/ na /ʃ/ Kuchunguza mabadiliko ya sauti yanayotokea mofimu zinapoungana. Kwa mfano; katika lugha ya Kiswahili,             U + ima         –       wima             I + etu            –       yetu             Mu + alimu    –      Mwalimu             U + imbo      –       wimbo             Vi + ake        –      vyake Wanamofofonemiki wakagundua kuwa sauti fulani huweza kuungana na kuunda sauti moja na kubadili umbo la neno. Chunguza muundo wa kifonolojia wa mofimu katika lugha. Kwa mfano katika lugha ya Kiswahili;             Mu + huni – Mhuni             Mu + gonjwa – Mgonjwa             Mu + guu – Mguu             Mu + uguzi – Muuguzi             Mu + tu – Mtu Wanamofofonemiki wakagundua kwamba mofimu fulani huweza kuungana na mofimu nyingine na kuunda umbo la neno. Kuchunguza ubadilishanaji wa sauti ambao una una uamilifu wa kimofolojia lakini husababisha mabadiliko fulani ya kifonetiki. Kwa mfano katika lugha ya kiingereza;             Play + s – [pleiz]             Dog + s – [dogz]             Since – [sins]             Else – [els]             Place – [pleis] Wanamofofonemiki wakachunguza kinachosababisha kuwepo na maumbo tofauti tofauti ya mofimu ya wingi. Kwa mfano; /s/, /iz/, /z/ Wakagundua kuwa kuna mchakato zaidi ya ule wa kifonolojia ambao ni wa kimofolojia unaosababisha umbo ‘s’ kutamkwa /z/ au /iz/ au /s/

                                        MAREJEO:
 The New Oxford American Dictionary. (2005), (2ndEdit), Oxford University Press. New York.


KANUNI ZA UUNDAJI WA HOJAJI




Makala haya yanahusu kanuni za uandaaji wa hojaji. Katika kujadili mada hii tumegawa kazi hii katika sehemu tatu muhimu, sehemu ya kwanza fasili ya hojaji kulingana na wataalam mbalimbali, sehemu ya pili ni kiini cha swali ambapo inaelezea kanuni muhimu za uundaji wa hojaji, hatimaye hitimisho. Kwa mujibu wa Kothari C.R, (2004), uk 100, anafasili neno hojaji kuwa ni maswali yanayoandikwa katika karatasi ili yaulizwe kwa mtafitiwa kwa lengo la kupata taarifa za tatizo la utafiti. Nayo Kamusi ya Kiswahili sanifu (2004) TUKI uk 116, inasema kwamba hojaji ni karatasi yenye maswali ya uchunguzi. Ni seti ya maswali mengi apewayo mtu/watu kwa lengo la kupata taarifa juu ya jambo fulani (Macmillan Dictionary) [1] Kutokana na fasili hizo hapo juu tunaweza kusema kuwa, hojaji ni maswali yanayoandaliwa na mtafiti kwa lengo la kukusanya data kutoka kwa watafitiwa. Hojaji hizo mtafiti anaweza kupeleka mwenyewe kwa mtafitiwa kwa njia ya mkono au kwa njia ya posta ikiwa na kimbatanisho cha kumwomba mtafitiwa asome na kuelewa maswali kisha ajibu maswali katika nafasi zilizoachwa wazi kwa matumizi tu ya hojaji kisha kuyarudisha kwa mtafiti. Hojaji zinazopelekwa kwa njia ya mkono husambazwa kwa haraka zaidi, na huwafikia watu wengi hususani wale wanaomzunguka mtafiti. Faida yake ni rahisi kukusanya, pia zinachukua muda mfupi, vilevile gharama zake ni ndogo, Faida ya kutumia njia ya posta ni pamoja na kutumia gharama ndogo na husambazwa katika eneo kubwa kwa muda mfupi. Pia mtafitiwa ana muda wa kutosha wa kuweza kutoa majibu kadri maswali yalivyoulizwa. Pia mtafitiwa ambaye hawezi kuingiliwa kwa urahisi hii inaweza kuwa njia nzuri ya kutumia. Licha ya njia hizo kuwa na faida pia zina hasara kama zifuatazo; kwanza mara nyingi hojaji zinazorudi zikiwa zimejazwa ni chache. Hii ni kutokana na mtafitiwa kutokuona umuhimu wa hojaji au kusongwa na majukumu au maswali kutokueleweka. Pili inabagua maana inahitaji watu wanaojua kusoma na kuandika, hojaji zinaweza kupotea zinapokuwa zinatumwa au kurudishwa. Ni vigumu kuelewa kama majibu yatolewayo ni ya kwa kweli au ya uongo. Hata hivyo njia hii ni ya taratibu mno kuliko njia zingine katika ukusanyaji wa data. Hojaji zimegawanyika katika makundi makubwa mawili; kwanza hojaji funge na hojaji za wazi (zisizo funge). Hojaji funge maswali yake yako wazi na yanaeleweka kwa watafitiwa. Maswali yanayoulizwa yanakuwa sawa kwa watafitiwa wote, yanalenga kutoa jibu moja tu. Mfano ndiyo au hapana, au ya kuchagua a,b,c,d…. hayaruhusu mtafitiwa kuweka hisia zake. Muundo wa maswali waweza kuwa funge. Kwa mfano; ANDIKA “N” KAMA JIBU NI NDIYO NA “H” KAMA JIBU NI HAPANA. AU CHAGUA HERUFI YA JIBU SAHII TU. Hojaji isiyo funge ni hojaji ambayo inamruhusu mtafitiwa kutoa maelezo/kujieleza/au kutoa maoni ya ziada (kutoa ufanuzi zaidi kadri ya uelewa wake kulingana na jinsi alivyoulizwa) Hojaji kama njia ya ukusanyaji data ina kanuni muhimu za kuzingatiwa wakati wa kuiandaaa. Mtafiti hana budi kuzingatia mambo yafuatayo; kwanza; ajue TATIZO LA UTAFITI. Mtafiti akishajua tatizo la utafiti itamsaidia kuandaa hojaji yake katika muundo unaotakiwa. Kwa mfano; atajua ni eneo gani ataenda kufanyia utafiti wake, umri wa watafitiwa, jinsia na kiwango chao cha elimu. Tatu izingatie usuli wa watafitiwa kama vile jina, umri jinsia, kabila na kiwango cha elimu. Hii inasaidia mtatifi katika uchambuzi wa data kujua amehoji watu wa umri gani na amehoji watu wa kiwango gani cha elimu. Pili ni mtiririko mzuri wa maswali; ili kutengeneza/kuandaa hojaji nzuri na kupata majiu sahihi mtafiti lazima azingatie mtiririko mzuri wa uaandaaji wa maswali. Mtiririko mzuri unaondoa uvulivuli/ukakasi kwa mtafitiwa, hivyo basi maswali lazima yawe katika mtiririko ufuatao; Kuanzia maswali mepesi kwenda maswali magumu, hii itampa moyo mtafitiwa au kumvutia na kuonesha ushirikiano lakini pia yatamvutia na kumpa moyo hivyo ataonesha ushirikiano au kupata hamasa ya kutaka kutoa majibu zaidi. Maswali hayo yawe na uhusiano/ muwala. Maswali yafuatayo hayana budi kuekwa; maswali yanayomtaka mtafitiwa kufikiri sana maswali yanayomhusu mtafitiwa, mfano una watoto wangapi, mkewe yuko wapi, kwa nini huna mtoto? Maswali yanayohusiana na mali za mtafitiwa, mfano je una magari mangapi? Au unalipwa kiasi gani kwa siku? Maswali yanayofuata baada ya maswali ambayo hayana budi kuepukwa ni maswali yanayohusiana na mada ya utafiti. Ambayo yanamtaka mtafitiwa kufikiri kiundani ili kuweza kutoa majibu sahihi. Mfano, nafasi ya uchaguzi wa lugha ya Kiswahili kama lugha ya kufundishia elimu ya juu. Maswali yalenge nini kinapelekea Kiswahili kuteuliwa kuwa lugha ya kufundishia elimu ya juu. Au tatizo la utafiti ni watoto wa mtaani. Kwa hiyo maswali yalenge sababu za kuwepo watoto wa mitaani. Maswali magumu yaulizwe mwishoni. Hii ina faida kwa sababu, hata kama mtafitiwa atashindwa kujibu kutokana na sababu mbalimbali maswali yale ya awali yatakuwa yanatosha kutoa taarifa muhimu zinazohusu tatizo la utafiti. Pia mtiririko wa maswali lazima uanze na maswali ya jumla kwenda maswali mahususi. Mtafitiwa hana budi kuelewa kuwa majibu yaliyotolewa ni kwa ajili ya utafiti huo. jinsi/namna ya utungaji wa maswali hayo; kutunga maswali katika mtiririko mzuri kwa kuanza na maswali rahisi kwenda magumu lakini pia kwa kuzingatia maswali ya jumla kwenda maswali mahususi. Maswali magumu yanaulizwa mwishoni. Maswali yanayotungwa yawe wazi, yasiwe na upendeleo wa kijinsia au kisiasa au kidini. Maswali yazingatie vigezo vifuatavyo; Maswali, yawe mafupi, yenye wazo moja, pia yawepo maswali ya majibu mafupi ya ndiyo au hapana, ya kuchagua na yawepo maswali ya kutoa maelezo. maswali yaeleweke/yawe sanifu maswali yaendane na uwezo wa kufikiri wa mtafitiwa, mfano unasuka kwa mwaka mara ngapi? Swali hilo ni gumu kwa maana hiyo lingeweza kuulizwa kuwa, kwa wiki unasuka mara ngapi? Hii itasaidia kufikiria kwa haraka. Kanuni ya pili hojaji isiwe ndefu sana, na kila hojaji iwe na lengo moja tu. Matokeo ya hojaji kuwa ndefu itamchosha mtafitiwa. Muhimu maswali yasidokeze majiu. Kwa mfano Hivi wewe ndo Honest? Hapa hospitali nasikia hakuna huduma nzuri ni kweli? Tatu izingatie usuli wa watafitiwa kama vile jina, umri jinsia, kabila na kiwango cha elimu. Hii inasaidia mtatifi katika uchambuzi wa data kujua amehoji watu wa umri gani na amehoji watu wa kiwango gani cha elimu. ***namna/jinsi ya kutunga maswali, mtafiti lazima atambue kwamba kila swali lazima liwe wazi vinginevyo mtafitiwa hataelewa swali linataka nini. Vilevile maswali yasiwe na upendeleo wa kijinsia kwa mfano*** 4. Maswali yazingatie vigezo vifuatavyo; yawe rahisi, na yenye wazo moja la msingi. Maswali yaeleweke kirahisi. Maswali yaendane na uwezo wa kufikiri wa mtafitiwa mfano unasuka kwa mwaka mara ngapi? Swali hilo ni gumu kwa maana hiyo lingeweza kuulizwa kuwa kwa wiki unasuka mara ngapi? Hii itasaidia kufikiria kwa haraka. Pamoja na hayo kuna miundo ya aina mbili ya utungaji wa maswali; maswali yenye majibu ya kuchagua (funge) maswali yanayomruhusu mtafitiwa kujieleza (si funge) FAIDA YA MASWALI FUNGE Kwanza ni rahisi kujibu, yanaeleweka kwa urahisi, mtafitiwa ana uwezo wa kutofautisha swali moja na jingine HASARA Kwanza maswali hayo yanatoa majibu kwa mtafitiwa. Mfano Wahehe wanakula mbwa? Andika ndiyo au hapana, pia huzuia nafasi ya mtafitiwa kujieleza zaidi kwa jambo analolijua, pia hayako sahihi hasa pale ambapo yanakuwa magumu na hasa mtafiti anahitaji majibu sahihi. Kutokana na udhaifu wa maswali funde, ndipo maswali ya wazi yanapohitajika. Maswali ya wazi yanatungwa kwatika mazingira ambayo yanatoa nafasi kwa mtafitiwa kutoa maelezo zaidi kwa kutumia maneno/maelezo yake binafsi. FAIDA YA MASWALI HURU Huruhusu mtafitiwa kutoa maelezo mengi tena kwa maneno yake binafsi, mtafitiwa huwa huru katika kujieleza,. HASARA Ni vigumu kukabiliana nayo, kwa maana kwamba inaibua ugumu wa kubaini majibu sahihi ya swali lililoulizwa hii ni kwa sababu maelezo yanakuwa mengi. Pia mtafitiwa anaweza akawa na mtizamo hasi kwa hiyo akajibu ndivyo sivyo. Kwa hakika hojaji nzuri haina budi kutumia njia zote mbili yaani njia ya maswali funge na njia ya maswali ya wazi. Kwani kwa kufanya hivyo unaweza kupata majibu ya ndiyo au hapana kadri ya maswali yaliyoulizwa, lakini pia utapata maoni mbalimbali na picha halisi kulingana na mtizamo wa mtafitiwa. Mtafiti lazima awe makini katika maneno anayotumia katika kuaandaa maswali, maneno yawe na maana. Pia mtafiti lazima atumie sentensi rahisi. Maneno ambayo ni magumu ambayo hayaeleweke, istilahi za kitaalumaau na yenye maana zaidi ya moja lazima yaepukwe. Pia maneno ambayo hayaendani na utamaduni wa jamii husika lazima yaepukwe Kimsingi utunzi wa maswali na utumiaji wa maneno ni sanaa ambayo inahitaji mtu kujifunza.

MJENGO WA FASIHI SIMULIZI NA FASIHI ANDISHI MJENGO WA FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI. MJENGO WA FASIHI ANDISHI YA KISWAHILI

MJENGO WA FASIHI SIMULIZI NA FASIHI ANDISHI MJENGO WA FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI. MJENGO WA FASIHI ANDISHI YA KISWAHILI


SINTAKSIA HAIWEZI KUTENGANISHWA NA VITENGO VINGINE VYA LUGHA.




Katika kujadili mada hii, kwanza tutatoa fasili ya sintaksia kwa mujibu wa wataalam mbalimbali, fasili ya lugha, tutafafanua uhusiano uliopo kati ya sintaksia na vitengo vingine vya lugha na mwisho tutatoa hitimisho juu ya mjadala wetu. Kwa mujibu wa Massamba na wenzake (1999) Sintaksia ni utanzu wa sarufi unaojihusishana uchunguzi wa mpangilio wa maneno katika sentensi na uhusiano wa vipashio vyake. Wanaendelea kusema, utanzu huu huchunguza sheria au kanuni zinazofuatwa katika kuyapanga maneno ili yalete maana inayokubalika na kueleweka katika lugha husika. Pia Habwe na Karanja (2004) wanasema Sintaksia ni utanzu wa isimu unaoshughulikia muundo wa sentensi na elementi nyingine zinazounda sentensi kama vile kategoria za maneno, vikundi na vishazi. Kutokana na fasili hizi inaonekana kuwa Massamaba na wenzake wamefafanua zaidi kwa kuonesha kuwa licha ya kuzingatia kanuni na sheria za kupanga maneno lakini pia ni lazima maneno hayo yawe na uhusiano. Kwa upande mwingine Habwe na Karanja wameshindwa kuelezea suala hili, wao wanaona sintaksia inashughulika na muundo wa sentensi na vipashio vyake. Kwa mantiki hii tunakubaliana na fasili ilyotolewa na Massamaba na wenzake kuwa Sintaksia ni utanzu wa sarufi unaojihusisha na uchunguzi wa mpangilio wa maneno katika sentensi na uhusiano wa vipashio vyake, kwa kuzingatia sheria na kanuni za lugha husika ili kuleta mawasiliano. Katika fasili ya lugha, wataalam wengi wanakubaliana kuwa lugha ni mfumo wa sauti nasibu ambazo hutumiwa na jamii kwa madhumuni ya mawasiliano kati yao. Baadhi ya wataalam wanao kubaliana na fasili hii ni Massamba na wenzake (Wameshatajwa). “Kitengo” kwa mujibu wa TUKI (2004) ni mahali pateule palipotengwa kwa shughuli maalum. Tunaporejea katika muktadha wa lugha tunaweza kusema kuwa vitengo vya lugha ni vipengele muhimu vinavyounda maarifa ya lugha kwa ujumla. Kwa fasili hii, vipengele vinavyounda maarifa ya lugha ni fonolojia, mofolojia, sintaksia na semantiki. Kwa hiyo kutokana na kwamba sintaksi pia ni kitengo mojawapo kinachounda maarifa ya lugha, tunakubali kwamba, sintaksia haiwezi kutenganishwa na vitengo vingine vya lugha kutokana na uhusiano mkubwa uliopo baina ya vitengo hivi. Vitengo hivi hutegemena na kuathiriana. Hivyo basi tunaweza kuonesha jinsi sintaksia isivyoweza kutenganishwa na vitengo vingine vya lugha yaani fonolojia, mofolojia na semantiki kama ifuatavyo: Uhusiano baina ya fonolojia na sintaksia. Massamba na wenzake (Wameshatajwa) wanafasili fonolojia kuwa ni uchambuzi wa mfumo wa sauti katika lugha mahususi. Wanaendelea kusema ni jinsi ambavyo vitamkwa au sauti za lugha zinavyoungana ili kujenga maneno yanayokubalika katika lugha. Kwa hiyo tunaweza kusema kuwa kuungana kwa vitamkwa ili kujenga maneno yanayokubalika katika lugha fulani hutegemea mpangilio sahihi wa vitamkwa. Na kwa kuwa neno ni kiwango cha msingi cha uchambuzi katika sintaksia basi fonolojia ina uhusiano wa moja kwa moja na sintaksia. Mifano ifuatayo huthibitisha hoja hii: Mfano 1.“Anapika”. Hili ni neno lakini pia ni sentensi, hivyo huweza kuchanganuliwa kifonolojia kama ifuatavyo: a|n|a|p|i|k|a|, mpangilio wa sauti umeunda neno “anapika”. Mfano 2.a. baba. Limeundwa na (KIKI). b. abab. Limeundwa na (IKIK). Katika mfano 2a tunaona neno “baba” lina maana na limefuata kanuni na mpangilio unaokubalika wakati mfano 2b neno “abab” halina maana katika lugha ya Kiswahili kwa sababu halina mpangilio mzuri wa fonimu. Kwa mifano hii tunaona kwamba hatuwezi kuwa na miundo mikubwa katika sentensi bila kuwa na mpangilio sahihi wa sauti katika lugha. Kwa hiyo sintaksia haiwezi kukamilika bila fonolojia. Uhusiano baina ya mofolojia na sintaksia. Mofolojia ni kitengo kingine cha lugha ambacho kwa mujibu wa Rubanza (1996) ni taaluma inayoshughulikia vipashio vya lugha katika kuunda maneno. Kutokana na fasili hii, kipashio cha msingi katika uchambuzi wa kimofolojia ni neno ambalo ndilo hutumika kuunda darajia ya sintaksia. Vilevile maumbo ya kimofolojia huathiri vipengele vingine vya kisintaksia, kwa mfano, sentensi zifuatazo hufafanua zaidi: 1. Mtoto anacheza. 2. Watoto wanacheza. Katika mifano hii tunaona kwamba mofimu m- na wa- katika upande wa kiima zimeathiri utokeaji wa mofimu a- na wa- katika upande wa kiarifu. Pia kanuni za mfuatano na mpangilio wa mofimu au viambishi zikifuatwa huunda maneno katika miundoya kisintaksia. Mfano: 1. Alicheza = a-li-chez-a 2. Anaimba = a-na-imb-a Kwa ujumla kipengele cha umoja na wingi katika maumbo ya kimofolojia ndicho kinachoathiri umbo linalofuata jina na kuathiri muundo wa sentensi nzima. Mfano: 1. Mwalimu alikuwa anafundisha. 2. Walimu walikuwa wanafundisha. Tunaona katika mifano hii maumbo ya umoja na wingi ya maneno Mwalimu na Walimu yameathiri mpangilio mzima wa sentensi. Uhusiano baina ya semantiki na sintaksia. Habwe na Karanja wakimnukuu Richard na Wenzake (1985) wanasema Semantiki ni stadi ya maana. Semantiki ni utanzu unaochunguza maana katika lugha ya mwandamu. Wanaendelea kusema semantiki hutafiti maana za fonimu, mofimu, maneno na tungo. Kwa hiyo kutokana na fasili hii maana hushughulikiwa katika vitengo au viwango vyote vya lugha ambavyo ni fonolojia, mofolojia na sintaksia. Mfano: a) Paka mweusi amepotea. b) Mweusi paka amepotea. c)Amepotea mweusi paka. Katika mifano hii tunaona kwamba sentensi a) ina maana kutokana na kwamba imefuata mpangilio sahihi wa maneno katika tungo na sentesi zilizobaki hazina maana kutokana na sababu kwamba hazijafuata mpangilio ulio sahihi. Kwa mantiki hii, kwa kuwa semantiki hushughulikia viwango vyote vya lugha, basi hushughulikia pia kiwango cha sintaksia ambapo huangalia maana za tungo. Tungo yoyote ni lazima ilete maana inayokubalika na wazungumzaji au watumiaji wa lugha husika, kama itakuwa kinyume basi haitakuwa tungo bali ni orodha ya maneno tu. Mfano: Mtoto anacheza mpira uwanjani. Mtoto uwanjani mpira anacheza. Tukiangalia mifano hii tutagundua kwamba katika sentensi ya kwanza mpangilio wake wa vipashio unaleta maana lakini sentensi ya pili haina maana kutokana na kuwa na mpangilio mbaya wa maneno. Kwa hiyo tunaweza kuhitimisha kwa kusema kuwa sintaksia haiwezi kutenganishwa na vitengo vingine vya lugha kwa kuwa kuna uhusiano wa moja kwa moja baina ya vipengele hivi vya lugha na kwa hiyo hutegemeana kati ya kipengele kimoja na kingine. Kwa mfano, huwezi kupata mofolojia (neno) bila kupitia ngazi ya fonolojia na pia huwezi kuwa na ngazi ya sintaksia (sentensi/tungo) bila kupitia ngazi ya fonolojia na mofolojia lakini vitengo vyote hivi hutawaliwa na kitengo cha semantika ili kuleta mawasiliano miongoni mwa wazungumzaji. 

                                                                         MAREJEO 
Habwe, J na P. Karanja (2007). Misingi ya Sarufi ya Kiswahili. Nairobi: Phoenix Publishers Ltd. Massamba, D.P.B na wenzake (1999). Sarufi Miundo ya Kiswahili Sanifu: Sekondari na Vyuo. Dar essalaam: TUKI. Rubanza, Y.I (1996). Mofolojia ya Kiswahili. Dar es salaam: Chuo Kikuu Huria cha Tanzania. TUKI (2004).Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Dar es salaam: TUKI.

KIAMBISHI TAMATI “NI”

Makala haya yatashughulikia ufupisho wa makala ya Swahili forum iliyohaririwa na rose – marie beck, Thomas gelder na wemer graefner katika uchambuzi wa kiambishi tamati cha mahali –ni, tathmini na mwisho hitimisho. Makala haya yanahusu asili na usambaaji wa kiambishi tamati cha mahali –ni. Karibu lugha zote za kibantu kuna ngeli tatu za mahali zenye viambishi pa, ku, mu, kwa mfano katika lugha ya kisangu viambishi hivi vya mahali hujitokeza pia katika maneno ya mu-khati, pa-khati, na ku-khati. Kwa upande wa lugha ya kiswahili mofimu hizi yaani pa, ku, mu hutumika kama viwakilishi vionyeshi kwa mfano hapa, huku na humu na vilevile hufanya kazi kama viwakilishi vimilikishi. Kwa mfano kwetu, kwao na mwao. Dai hili limetolewa na Beck na wenzake (1994). Swali la msingi, kama viambishi vya mahali vinavyojitokeza katika ngeli hizo, kiambishi –ni- hakipo, kiambishi hiki kimetoka wapi?

NADHARIA YA UDENGUZI NADHARIA YA UDENGUZI KATIKA UJITOKEZAJI WA WAHUSIKA WA TAMTHILIYA ZA KISWAHILI.

 Wahusika ni kitu muhimu katika kazi yoyote ya kifasihi, kwani ndio wanaosukuma mbele kazi ya kifasihi. Wataalamu mbalimbali wamezungumzia kwa namna tofauti maana na ujitokezaji wa wahusika wa kazi ya fasihi. Hii ni taka enzi za Ugiriki ya kale hadi katika fasihi ya kiswahili. Mulokozi (1996) anasema hadithi ya tamthilia husonga mbele kwa njia ya vitendo na mazungumzo ya wahusika. Hivyo anaonesha bila wahusika hata mazungumzo hayatakuwepo. Brecht (1898-1956) aliibua kanuni ya ukengeushi ambayo aliitumia kukengeuka kanuni za Kiaristotle. Moja kati ya ukengeushi wake ulikuwa ni katika kipengele cha wahusika. Ambapo kwa Aristotle mhusika mkuu katika Tanzia alikuwa ni lazima atoke tabaka la juu, lakini kwa Brecht haikuwa lazima kwa mhusika kutoka tabaka la juu. Lengo la Brecht lilikuwa kuonesha kuwa hata tabaka la chini linaweza kuleta mabadiliko katika jamii. Kanuni/dhana hii ya Brecht inalandana na nadharia ya udenguzi/ujenguzi. Udenguzi ni nadharia ya kihakiki iliyoanzishwa na mwanafalsafa wa Kifaransa Jacques Darrida (1973), ambapo anasema ujuzi na maarifa si vitu vinavyoweza kueleweka moja kwa moja, katika matini yoyote ile ujuzi hutumika katika kuunda matini hiyo, kwa kuwa ujuzi si kitu kinachoweza kueleweka moja kwa moja hupelekea kuonekana kwamba ujuzi na maarifa kuwa ni kitu kisichoshikika yaani chenye utelezi. Hivyo hata tafsiri ya matini kwa wahakiki haiwezi kuelezwa kwa namna moja, kila mtu ataieleza kwa namna yake hii ina maana kwamba, maana zinaweza zikaendana au zikapingana. Miller (1976) anasema udenguzi ni juhudi ya kufikia nguvu na uwezo wa matini kama chombo kinachoweza kujifafanua. Rorty (1995) anasema udenguzi ni ukiushi wa kaida wa matini, ukiushi huu utokeapo kwa amara ya kwanza huonekana kama ni usaliti, lakini utokeaji wa ukiushi si ajali bali hukusudia kufikisha ujumbe uliokusudiwa. Maelezo hayo ya Rorty yanatupa picha halisi ya mabadiliko yanayoweza kutokea katika uundaji wa matini. Mfano uundaji wa mashairi ya Kiswahili hapo mwanzo ulikuwa ukifuata urari wa vina na mizani lakini baadaye yakaibuka mashairi ya kisasa ambapo wanajadi waliona kuwa ni usaliti wa ushairi wa Kiswahili. Vilevile maelezo hayo yanatupa mwanga wa kuelewa kuwa katika matini udenguzi utokeapo unakuwa na lengo la kujifafanua zaidi. Kutokana na maelezo hayo ndipo Wafula na Njogu (2007) waliposema kwamba kutokana na udenguzi hakuna toleo la mwisho la kazi ya fasihi. Hii ndio inayofanya wahakiki kutoa fasili tofauti tofauti za jambo moja fasili hizo zaweza kufanana au kutofautiana. Kwa hiyo udenguzi unaweza kuboresha matini au kuumba upya kwa lengo la kukidhi upya mahitaji ya jamii kama ilivyokuwa kwa nadharia ya ukengeushi ya Brecht. Nadharia hii tutaitumia kuhakiki ujiotokezaji wa wahusika katika tamthiliya za Kiswahili. Semzaba (1997) anasema Wahusika ni tabia zinazopambanua mhusika mmoja na mwingine. Wahusika ndio nyenzo muhimu inayosababisha mtiririko wa matukio. Mhusika huonyeshwa na mwandishi kwa maneno pamoja na matendo. Kwa kuwa tamthilia ni utungo ulioandikwa wahusika hutofautiana kwa mambo manne; kwa mujibu wa Semzaba. (i) Maumbile kama vile jinsia, umri, tambo, rangi nk. Pia hutofautiana dini, kiuchumi nk. (ii) Wahusika wasiobadilika (bapa) wanaobadilika (duara) (iii) Wahusika ishara (iv) Wahusika wafaili: Hujenga wahusika wakuu. Mulokozi (1996) Ametaja aina za wahusika wa tamthilia; kuna wahusika wakuu (i) Mbabe /nguli (ii) Mkinzani (iii) Muwi (muovi) Wahusika wadogo (i) Mfoili (ii) Msimamizi (iii) Chizi Wahusika hawa walioorodheshwa ni kutokana na uanishaji wa tamthilia za kimagharibi. Tamthilia kwa upande wa fasihi ya Kiswahili zilifuata baadae, hivyo ujitokezaji wa wahusika ukawa tofauti hasa baada ya kuingiza Uafrika (upya) katika sanaa hizi. Hata kama aina ya mhusika ni ile ya Kimagharibi (Mfano msimulizi wa chizi) lakini ujitokezaji wake ukaanza kuwa wa Kiafrika zaidi hapa ndipo tukaona udenguzi unatokea, udenguzi huu hautokei kama ajali bali umelenga kuboresha na kuhifanya tamthilia iendane na mazingira halisi ya fasihi ya Kiswahili, Katika tamthilia ya Mkutano wa Pili wa Ndege ujitokezaji wa wahusika kiudenguzi ni katika matumizi ya wahusika wa kifasihi simulizi. Mwandishi ametumia wahusika wa kifasihi simulizi ambao ni ndege na wanyama, katika tamthilia. Mfano katika (uk.14–15) mwandishi anasema: Tausi: enyi wa mashariki Poleeni Ogeleeni Chiriku: ko ko likoo! ooooh! Magharibi sisahau Wahusika hawa (ndege na wanyama) hutumiwa sana katika fasihi simulizi, hivyo mwandishi amedengua ujitokezaji wa wahusika si binadamu pekee katika tamthilia za Kiswahili kuna wahusika wasio binadamu. Pia katika tamthilia ya Jogoo Kijijini na Ngano ya Jadi ujitokezaji wa wahusika kiudenguzi ni katika matumizi ya wahusika wa kifasihi simulizi. Mwandishi amemtumia mhusika Joka akaliita sesota, kiishara kuwakilisha ukoloni na jinsi ukoloni huu ulivyokomaa, akalipa joka hilo vichwa sabini, kuonyesha kiasi gani unavyoziathiri nchi za Kiafrika. Mfano: Katika (uk.21) mwandishi anasema Kwani Likuwa tabia makini Killa mwaka ukibaini Joka hushuka kijijini Kuchukua mali na binti mwema mmoja. Matumizi ya joka ni udenguzi. Pia katika tamthilia ya Nguzo Mama, ujitokezaji wa wahusika kiudenguzi ni kupitia mhusika Chizi. Chizi kama inavyoaminika katika jamii ni mtu asiyeweza kuongea neno la maana, lakini katika tamthilia hii mwandishi amemtumia mhusika huyu na kumwonyesha akieleza kitu cha msingi na muhimu. Mwandishi anasema: Chizi: Nani anapendeza? Waoneni watu hawa Hawapendi demokrasia Nikisema yote mie Wananiita mie chizi Chizi mie au nyie (uk. 29 – 31) Pia katika tamthilia hiyo hiyo ya Nguzo Mama ujitokezaji wa wahusika kiudenguzi ni katika majina ya wahusika. Mwandishi amewapa wahusika wake majina kwa kuanzia na Bi Moja – Bi Nane. nk. Majina hayo yote huashiria uhusika na kifasihi simulizi, kwa kuwa katika hadithi nyingi za Kifasihi simulizi, huanza hivi. ”Hapa zamani za kale, palikuwa na baba mmoja na mama mmoja.” Hivyo mwandishi huyu ametumia majina ya kiidadi au kinamba ambayo ni majina pia ya wahusika wa kifasihi simulizi katika tamthiliya ya Heshima Yangu ujitokezaji wa wahusika kiudenguzi umejitokeza kupitia mhusika Mzee Issa. Mhusika huyo anadai heshima ambayo yeye mwenyewe hajailinda heshima hiyo kwa kuzaa nje ya ndoa na kuificha siri hiyo ya kuwa na mtoto nje ya ndoa yake. Mzee Issa alimkataa Salum toka akiwa tumboni mwa mama yake, na kisa kutomjua baba yake hadi ukubwani alipotaka kumuoa Rukia, ndipo anapoambiwa kuwa ni dada yake. Mwandishi anaonyesha kuwa kuheshimiwa si kwa vile una umri mkubwa tu bali pia matendo yako yanaweza kukuvunjia heshima hata kama una umri mkubwa. Mwandishi anasema: Rukia (anasogea mbali na nyumba, anawaza kwa huzuni). “Heshima yangu, heshima yangu” (Kimya kwa muda) Ni heshima gani ipatikanayo katika kumkatalia Salum kijana mzuri, mwenye tabia nzuri na moyo wa imani, eti kwa sababu ni mwana haramu? Ni kosa.....(uk. 10)” Pia katika tamthiliya ya Mashetani ujitokezaji wa wahusika kiudenguzi unajitokeza kupitia wahusika wake Juma na Kitaru. Mwandishi katika tamthilia hii amedengua ujitokezaji wao kutoka kufikia hali ya kuwa na majina yao ya Juma na Kitaru hadi kwenye uhusika wa kishetani na kibinadamu. Mwandishi ameonesha udenguzi wa wahusika kwani si hali ya kawaida kwa wahusika kuchorwa hivyo, Mfano:- Muhusika katika tamthilia akichorwa kama baba, basi atakuwa baba hadi mwisho wa tamthilia hiyo. Pia katika tamthiliya ya Kivuli Kinaishi ujitokezaji wa uhusika kiudenguzi unajitokeza kupitia mhusika Bi Kirembwe, ambaye ni mhusika mwanamke lakini amechorwa kitofauti na wahusika wengine wanawake wanavyochorwa katika baadhi ya kazi za Fasihi. Mhusika huyu amechorwa kama mtawala na mwenye amri na sauti yakuwatisha hadi wanaume. Hii ni tofauti kwa uchoraji wa wahusika wa kike katika tamthilia nyingi, ambazo huwachora katika daraja la chini, duni na kukandamizwa. Mfano Martha katika tamthiliya ya Kwenye Ukingo wa Thim, amechorwa ni mwanamke anayekwenda na wakati lakini anakandamizwa na mfumo mzima wa jamii yake kwa kuonyeshwa akipokonywa mali zote baada ya mume wake kufariki. Pia katika tamthiliya ya Aliyeonja Pepo ujitokezaji wa uhusika kiudenguzi ni katika matumizi ya wahusika wakifikirika au wa kiimani, ijapokuwa suala hili limejitokeza pia katika riwaya za Kusadikika na Kufikirika lakini katika tamthilia hizi mwandishi amekwenda mbali zaidi kwa kutumia usawiri wa pepo na uhusika wa kiimani zaidi kuwakilisha mambo yaliyopo au yanayotendeka duniani na si nchi ya kidhahania kama alivyofanya Shaaban Robert katika riwaya zake za Kufikirika na Kusadikika. Mwandishi wa aliyeonja pepo ametumia wahusika kama malaika Ziraili, Sirafili, Jaburili na wengine ambao huamini ni malaika au pepo kuwakilisha mambo mbalimbali yanayotendeka duniani. Mfano: Mwandishi anasema: Ziraili: Wapi? Jiburili: Huko ambako wewe bado hajajishughulisha nako Huko...........(uk.3). Katika tamthiliya ya Lina Ubani ujitokezaji wa wahusika kiudenguzi ni kupitia mhusika Bibi ambaye anajitokeza mwanzo kabisa mwa tamthilia kwa kuimba. Jambo ambalo ni udenguzi wa kimuundo wa ujenzi wa tamthilia kwa kufuata misingi ya Kiaristotle, ambao kimuundo anasisitiza wimbo katika tamthilia uwe mwishoni na si mwanzoni mwa tamthilia kama alivyofanya mwandishi Penina Mhando katika tamthilia hii katika ukurasa wa kwanza, mwandishi anatuonesha mhusika Bibi amekaa analia kwa kuimba na kuombeleza. Bibi: Ing’oma ili sikuidaha doo ae Woidoo ae ya Nime mwitunda dya mele do Pia katika tamthiliya hiyo hiyo ya Lina Ubani ujitokezaji wa uhusika kiudenguzi unajitokeza kupitia mhusika Mwanahego. Mwandishi amemchora mhusika huyo kama mlevi lakini anaongea na kubishana na sauti mambo yenye maana, tofauti na walevi walivyozoeleka katika jamii, kwamba ni watu wasioweza kuchangia au kuongea mambo ya msingi katika jamii. Mwandishi anasema; Mwanahego: Umoja na mke wamo mnajifunika wote shuka moja Mwanahego na wewe tutakutana wapi ndipo tuwe na umoja....... wewe juu ya kilima, mimi bondeni.....(Uk.46). Pia katika tamthiliya ya Morani ujitokezaji wa wahusika kiudenguzi umejitokeza kupitia mhusika Jalia ambao ni mhusika wa kike ambaye mwandishi amedengua kwa kuonyesha asishiriki bega kwa bega na katika kampeni za kuwakamata wahujumu uchumi Jalia anashirikiana na mwenzake katika kampeni hiyo na kuonyesha msimamo wa hali ya juu, na ushupavu wa wanawake katika ukurasa wa 17 mwandishi anasema: Jalia: Na njia ya kuuzima moto ni kuwasha moto; moto mkali zaidi. Hivyo ndiyo hatua kamili. Kwa kuhitimisha nadharia ya Udenguzi na mawazo ya Brecht katika kuwachora wahusika yanalenga katika kuleta upya wa fikra kwa watazamaji na wasomaji wa tamthilia.