Subcribe to our RSS feeds Join Us on Facebook Follow us on Twitter Add to Circles

Jumapili, 1 Februari 2015

MAHUSIANO YA KIUTAWALA NA KIUSABIKI KUHUSIANA NA VIAMBAJENGO:-



              IMEANDALIWA NA MANYAMA CHARLES;CHUO KIKUU CHA ARUSHA.

                                                         DONDOO ZA SWALI:-

I. UTANGULIZI:-

II. KUJADILI KUHUSIANA NA DHANA ZIFUATAZO:-

A. Viambajengo Sisisi.

B. Viambajengo Viso-tamati.

C. Viambajengo Tamati.

D. Fundo Dada.

E. Fundo Binti.

F. Fundo Mama.

G. Fundo Baba.

III. HITIMISHO:-


Swali 2.

I. UTANGULIZI:-

II. KUJADILI KUHUSU MAHUSIANO YA KIUTAWALA NA KIUSABIKI KUHUSIANA NA VIAMBAJENGO:-

A. MAHUSIANO YA KIUTAWALA:-

B. MAHUSIANO YA KIUSABIKI:-

III. HITIMISHO:-

IV. MAREJEREO:-


Swali 1.

I. UTANGULIZI:-

Viambajengo ni vijenzi katika sentensi ambavyo hushirikiana na vingine ili kujenga vipashio vikubwa zaidi.viambajengo vya lugha kama fonimu, silabi na hata mkazo.

Katika Nadharia ya umilikifu,Nadharia hii ilihakikiwa na Noam Chomsky.Nadharia hii huweka masharti ya uhamishaji wa viambajengo. Kanuni katika nadharia hii ni kanuni masharti (subjacency condition). Kanuni hii inadai kwamba hatuwezi kuhamisha kiambajengo zaidi ya kifundo kimoja katika uhamishaji mmoja. Kifundo ni kikundi cha maneno yanayohusiana. Viambajengo ni maneno yanayopatikana katika sentensi Fulani.

Kwa mfano; sentensi,

a) Msichana mwerevu amepita mtihani.

Ina viambajengo vinne. Viambajengo msichana na mwerevu vinaunda kifundo kimoja ilihali viambajengo amepita na mtihani vinaunda kifundo kingine kimoja. Yaani; Msichana mwerevu amepita mtihani.

Kifundo (i) Kifundo (ii) Tunapotoa kiambajengo lazima pawe jirani na mahali kiambajengo hicho kinaelekea (landing site). Pale ambapo kiambajengo kimetoka lazima pawe wazi. Pia hatuwezi kuhamisha viambajengo viwili kwa wakati mmoja. Kwa mfano, Katika umbo ndani la sentensi; [ ameenda [mama [sokoni kununua mboga] Katika umbo nje itakuwa; Mama ameenda sokoni kununua mboga.Kutokana na mfano huu tunaweza kuhamisha kiambajengo mama kitangulie kitenzi ameenda lakini hatuwezi kuhamisha kiambajengo sokoni kwa sababu kitakuwa kimehamishwa zaidi ya kifundo kimoja katika uhamishaji mmoja.Yaani kiambajengo sokoni hakiko jirani kwa hivyo hakiwezi kuhamishwa.


II. KUJADILI KUHUSIANA NA DHANA ZIFUATAZO:-

1. Viambajengo Sisisi.

Hivi ni vijenzi au vipashio katika mchoroti ambavyo hutawaliwa kwa karibu hushirikiana na vingine ili kujenga vipashio vikubwa zaidi katika sentensi.Vilevile viambajengo hivi sisisi mtawala wake huwa ni mmoja tu na aghalabu viambajengo hivi huwa vimefuatana.


Mfano wake ni kama;


Mpira unachezwa na Juma.


S






KN KT


T KN


Juma anacheza mpira


Hivyo basi viambajengo sisisi katika mchoroti uliopo hapo juu KT ni T +KN.



2. Viambajengo Viso-tamati.


Hivi ni vijenzi au vipashio katika mchoroti ambavyo mfuatano wake unakuwa haujatimia au vinavyokuwa katikati kwenye mchoroti ambavyo uwepo wake hujenga vipashio vikubwa zaidi katika sentensi ambazo ndizo huja kuwa aina za maneno.


Mfano ni;


Mpira unachezwa na Juma.


S



KN KT


T KN


Juma anacheza mpira


Katika mchoroti huu viambajengo visotamati ni KN,KT,T na KN.Kwamantiki ya kuwa ndivyo viambajengo pekee ambavyo vimekatizwa katika mchoroti



3. Viambajengo Tamati.


Hivi ni vijenzi au vipashio katika mchoroti ambavyo mfuatano au mpangilio wake ndiyo unaokuwa chini kabisa kwenye mchoroti ambavyo uwepo wake hujenga vipashio vikubwa zaidi katika sentensi na ufahamika zaidi kama aina za maneno.


Mfano ni;


Mpira unachezwa na Juma.


S


KN KT


T KN


Juma anacheza mpira


Katika mchoroti hapo juu viambajengo tamati vyaweza bainishwa chini kabisa katika aina za maneno.



4. Fundo Dada.


Ni kile ambacho kinahusiana na kingine kwa sababu ya kuzaliwa au kumilikiwa na kifundo sawa.Fundo KN+KT au T+KN ni mafundo dada na S ndiyo huitwa fundo mama na vifundo vya chini kabisa ya mchoroti ndiyo huitwa vifundo viso-tamati.


Kwa mfano; S


KN KT


T KN


N V


5. Fundo Binti.


Ni kile ambacho kinamilikiwa kwa karibu na kifundo mama. Kwa mfano KN na KT ni vifundo binti vya S.Hivyo basi tofauti kubwa iliyopo baina ya fundo dada na fundo binti ni katika umilikifu pekee.Pia huitajika kutajwa kwa mzazi mmoja.,kama T+KN ni vifundo binti vya KT.


S


KN KT


T KN


6. Fundo Mama.


Ni kifundo ambacho kinamiliki vifundo vingine.Fundo hili ndilo mzazi halisi wa vifundo vingine kama vile fundo binti,fundo dada na hata fundo liso-tamati na fundo tamati.Mfano S ndilo fundo mama la KN+KT na T+KN


S


KN KT


T KN


7. Fundo Baba.


Wanaisimu kama Avram Noam Chomsky (1957) na mwenzake bloomfield (1965).wao kama waanzilishi wa Dhana hii ya Uambajengo,wanasdai kuwa ili kuonesha jinsi viambajengo vinavyohusiana.Wanaisimu hawa wametumia dhana au istilahi za kindugu aghalabu. kwa jinsia ya kike kwa mantiki ya kwamba ndiyo pekee yenye uwezo wa kuzaa na siyo jinsia ya kiume.Hivyo basi kifundo Baba hakiwezi kuwepo kwa madai hayo ya uwezo wa kuzaa,ndomana wakatoa mfano wa fundo mama,fundo dada na hata fundo binti.


Swali 2.


I. UTANGULIZI:-

Viambajengo ni vijenzi katika sentensi ambavyo hushirikiana na vingine ili kujenga vipashio vikubwa zaidi.
Utawala wa kiuambajengo ni hali ya kifundo cha kijenzi kimoja kukimiliki kifundo kingine.
Mahusiano ya kutangulia ni hali ya neno au kifundo kimoja kujitokeza kabla ya kingine katika ulalo. Yaani kinachokuwa kushoto kinakitangulia kilicho kulia.



II. KUJADILI KUHUSU MAHUSIANO YA KIUTAWALA NA KIUSABIKI KUHUSIANA NA VIAMBAJENGO:-


A. MAHUSIANO YA KIUTAWALA:-
Mahusiano ya Utawala wa kiuambajengo ni hali ya kifundo cha kijenzi kimoja kukimiliki kifundo kingine.Hivyo fundo lililo juu ndilo linatawala mafundo mengine yote.Mfano mzuri ni fundo mama kwa namna litawalavyo vifundo dada,fundo binti,fundo liso-tamati na fundo tamati.S inatawala KN na KT.



S

KN KT


V N T KN


Vilevile kuna aina kuu mbili za mahusiano ya kiutawala,ambayo ni utawala wa mbali na utawala wa karibu,Mfano S inatawala kwa karibu KN na KT;Pia S inatawala kwa mbali V,N,T na KN. na viambajengo vinavyotawaliwa kwa karibu ndivyo huitwa viambajengo sisisi na pia viambajengo vinavyokuwa vimetawaliwa kwa mbali ndivyo huitwa viambajengo viso-tamati na viambajengo tamati.



B. MAHUSIANO YA KIUSABIKI:-

Kutokana na Radford (1997);Mahusiano ya kutangulia ni hali ya neno au kifundo kimoja kujitokeza kabla ya kingine katika ulalo. Yaani kinachokuwa kushoto kinakitangulia kilicho kulia. aghalabu uhusiano huo wa kiuambajengo mafundo dada ndiyo haswaa hutanguliana na fundo la kushoto ndilo hutangulia fundo la kulia.Mfano


S


KN KT


V N T KN


KN inatangulia KT kwenye mahusiano ;V inatangulia N kwenye mahusiano na T inatangulia KN kwenye mahusiano.
Vilevile hata katika mahusiano ya kiusabiki kunajitokeza aina zipatazo mbili ambazo ni mahusiano ya kiutangulia kwa karibu na mahusiano ya kutangulia kwa mbali.
Mahusiano ya kutangulia kwa karibuhufuata toka katika fundo lililopo kushoto,na kutangulia kwa mbali ni pale kifundo kilichopo kushoto kutangulia vifundo vyote vilivyopo kulia. Mfano kiutoka katika mcho hapo juu ni kuwa V inatangulia kwa karibu N., na KN inatangulia kwa mbali vifundo vya KT.




MAREJEREO:-

Radford (1997) A syntax minimalist introduction..Cambrodge University Press,New York. Radford (1998) A transformational Grammar,Cambridge University Press, New York. Smith, N (199); Chomsky;Ideas and ideals,Cambridge University Press,New Yo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni