Subcribe to our RSS feeds Join Us on Facebook Follow us on Twitter Add to Circles

Jumanne, 4 Novemba 2014

KIAMBISHI TAMATI “NI”

Makala haya yatashughulikia ufupisho wa makala ya Swahili forum iliyohaririwa na rose – marie beck, Thomas gelder na wemer graefner katika uchambuzi wa kiambishi tamati cha mahali –ni, tathmini na mwisho hitimisho. Makala haya yanahusu asili na usambaaji wa kiambishi tamati cha mahali –ni. Karibu lugha zote za kibantu kuna ngeli tatu za mahali zenye viambishi pa, ku, mu, kwa mfano katika lugha ya kisangu viambishi hivi vya mahali hujitokeza pia katika maneno ya mu-khati, pa-khati, na ku-khati. Kwa upande wa lugha ya kiswahili mofimu hizi yaani pa, ku, mu hutumika kama viwakilishi vionyeshi kwa mfano hapa, huku na humu na vilevile hufanya kazi kama viwakilishi vimilikishi. Kwa mfano kwetu, kwao na mwao. Dai hili limetolewa na Beck na wenzake (1994). Swali la msingi, kama viambishi vya mahali vinavyojitokeza katika ngeli hizo, kiambishi –ni- hakipo, kiambishi hiki kimetoka wapi?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni