Subcribe to our RSS feeds Join Us on Facebook Follow us on Twitter Add to Circles

Jumanne, 4 Novemba 2014

HADITHI YA WAVULANA WAWILI NA MACHUNGWA

"Hadithi" by David E. Diva
Annotated by: Manyama charles

WAVULANA WAWILI NA MACHUNGWA

Palikuwa na wavulana wawili, mmoja akiitwa Kasu na wa pili Ambari. Walikuwa wakikaa katika kijiji kimoja na kusoma katika skuli moja; walikuwa marafiki wakubwa sana

Siku moja jioni, walikuwa wakitoka skuli na kurudi kijijini kwao. Walipokuwa wanapita katika shamba moja la michungwa, Kasu akamwambia Ambari, "Tazama machungwa hayo, yameiva vizuri sana. Je waonaje, hatuchumi machache tule, na mengine tuyachukue nyumbani?"

Ambari akamjibu, "La, michungwa hii si mali yetu wala ya jamaa zetu; kwa nini tuyachume? Huo ni wizi, haifai!"

Kasu akamwambia, "Ah lakini ipo njiani, na watu wengi hupita hapa; ni mali ya mtu ye yote.

Ambari akasema, "La, maana machungwa yenyewe yapo juu ya miti ya watu, hayapo njiani; huko ni mbali kabisa na kuokota kwa kawaida."

Walipokuwa wanajadiliana hivi, mtu mmoja akatokeza kichwa dirishani katika nyumba moja iyokuwapo karibu. Mtu yule aliitwa Hamisi, naye ndiye aliyekuwa mwenye shamba lile la michungwa, lakini wao hawa kumwona.

Ambari akasema, "Wakumbuka, Kasu, ya kuwa jana ulikuwa karibu na kupigana na Musa kwa sababu alichukua kalamu yako? Kwa nini, basi, wataka tuchukue machungwa ya watu?"

Kasu akasema, "Ah sijui, lakini mimi naona ya kuwa yapo kando ya njia. Kila mtu ana haki ya kuyachuma na kuyachukua."

Mara Hamisi, mwenye shamba, akacheka dirishani. Wavulana wale waliogopa sana. Kasu akakimbia, lakini Ambari alisimama pale pale alipokuwapo. Hamisi akachukua kikapu, akakijaza machungwa, akampa Ambari, akamwambia, "Chukua machungwa haya, na nusu yake kampe yule rafiki yako aliyekimbia. Nina hakika ya kuwa akiendelea na tabia yake mbaya ya kutokuwa na uaminifu atapotea; afadhali usishirikiane naye."

Ambari akamwambia Hamisi, "Asante sana, bwana, kwa machungwa haya na pia kwa maonyo yako."

Basi Ambari akayachukua machungwa yale, akampa Kasu, rafiki yake, nusu. Kasu alisikitikam sana kwa nia mbovu aliyokuwa nayo, na tangu siku ile akabadili mwenendo wake na kuwa mtoto mwema katika kila jambo.
xxxxxx MWISHO xxxxxxx

HADITHI YA MTOTO WA MFALME NA LULU-JIVUNIEKISWAHILI






Hapo zamani za kale, katika kijiji cha Mgombezi, palikuwa na mfalme aliyekuwa anajulikana kwa jina la Mbezi. Watuwake walikuwa hodari sana katika kilimo cha katani pamoja na zao la chakula la mpunga na uchimbaji wa madini ya dhahabu.
Mfalme Mbezi alikuwa pia hodari sana katika kutafuta soko la zao la katani katika nchi za jirani ili kukuza uchumi wa nchi yake. Kutokana na bidii aliyokuwa nayo aliweza kuwa msambazaji mkubwa wa zao la katani katika nchi za Lewa, Manundu, Zavuza nahata Kilole na Kwamatuku. Nchi yake ilikuwa haraka sana kiuchumi na wakaziwake walikuwa wanajiweza vyema kiuchumi. Mfalme Mbezi alisifika ndani na nje ya nchi ya Mgombezi. Alikuwa na jeshi lenyenguvu na watu wake walimpenda sana kwani alikuwa habagui wakumtatulia shida yake au kumsikiliza.
Mfalme Mbezi alikuwa na watoto wawili, wakwanza aliitwa Mjata na wapili aliitwa Mboni. Aliwapenda sana watoto wake, ndio waliokuwa wamebakia pekee na walimfariji sana na hata kusahau kifo cha mke wake aliyekufa miaka miwili iliyopita kutikana na ugonjwa wa kwikwi.
Sikumoja mfalme aliwaita wanae Mjata na Mboni nakuwaeleza kuwa anataraji kusafiri hivyo wachague zawadi gani waletewe kilammoja pindi baba yao atakapokuwa amerejea toka safari ya nje ya Mgommbezi. Mjata akamshukuru baba yake nakumwambia kuwa angependa aletewe Kanzu nzuri yarangi ya zambarau pamoja na kofia iliyoshonwa kwamwiba wa nungunungu na iwe ya rangi ya zambarau paoja na bakora ya shaba na viatu vya dhahabu. Mfalme Mbezi alivuta pumzi ndefu kisha akamwambia mwanae Mjata kuwa atafanya awezalo ili kuhakikishakuwa anamtimizia hitaji lake. Ikawa zamu ya Mboni kusema zawadi gani aletewe na baba yake pindi atakaporejea toka safari, Mboni akapiga magoti kwaunyenyekevu mbele ya babaye nakumwambia ''Babangu, nitafurahi sana pindi utakaponiletea LULU inayolindwa na jini kisirani katika kisiwa cha mikwingwina, baba nihilo tu hitaji langu'' Mfalme Mbezi alivuta pumzi ndefu kisha akatandikiwa farasi wake nakuondoka na walinzi 12 kuelekea Bungu kisha Lewa kutafuta masoko ya bidhaa ya nchi ya Mgombezi ili kukuza uchumi.
Safari ilichukua siku kumi na kenda na ilikuwa na mafanikio makubwa kwani walipata oda nyingi ya katani na mzigo waliokuwa wamefungasha wa katani pamoja na dhahabu vilikwisha na wakawa napesa nyingi sana. Alianza safari ya kurudi nyumbani lakini mara ghafla alikumbuka ahadi ya zawadi ambazo watoto wake walimtuma. Alinunua kanzu ya rangi ya zambarau ya Mjata pamoja na kofia iliyoshonwa na mwiba wa nungunungu na viatu vya dhahabu. Kazi ikawa kupata LULU aliyo agizwa na binti yake Mboni. Akajiapiza moyoni kuwa hatorudi nyumbani mpaka apate zawadi ya binti yake.
Mfalme alimgeukia mlinzi wake mmoja shupavu na kumwambia kuwa, amepewa jukumu kubwa sana la kuhakikisha kuwa LULU kwaajili ya binti yake inapatikana pia alimwahidi kumpandisha cheo maradufu na kumfanya tu muhimu sana katika familia ya kifalme. Mlinzi Mkwayu alijigamba kuwa atahakikisha anaipata hiyo lulu kwa heshima ya mfalme, basi mfalme alimkabidhi upanga wake wa dhahabu pamoja na chakula chepesi nakumtakia kila lakheri katika safari yake hiyo.
Mkwayu alipanda farasi wake mweusi mwenye siha njema nakupotea machoni mwamfalme kuelekea katika kisiwa cha Mikwingwina kilichopotakribani kilometa 75 toka pale walipo. Mkwayu kabla yakuondoka alimweleza mfalme angerudi na lulu ndani ya siku 2 zikizidi wajue amepatwa na mabaya. Pia alichoma shale kwenye mti nakuutemea mate yake nakusema ilihali watu wote wakiwa wanasikia maneno yale kwamba, mshale ule ukidondoka wenyewe chini toka katika mti, basi nayeye atakuwa amekumbwa na mabaya huko aendako.
Usiku wa manane ulivuma upepo mkali sana katika ile sehemu waliyokuwa wamepumzika mfalme na kundi lake mpaka mahema yalikaribia kung'ooka kutokana na upepo uliokuwa unavuma. Mara baada ya dakika takribani arobaini na tano, upepo ulikoma na hali ilibakia katika haliyake ya kawaida. Mlinzi aliyekuwa ameshika zamu usikuhuo alipo kuwa anakagua usalama, alikutana na mshale uliokuwa umewekwa na Mkwayu umedondoka chini, haraka aliwaeleza wenzake na mfalme pia alijulishwa juu ya hali ile na kugundua mojakwamoja kuwa Mkwayu amekutwa na jambo baya huko alikokuwa amekwenda. Akawaambia walinzi wake kuwa haiwezekani Lulu isispatikane na dhaihiri inaonyesha kuwa huko Mkwayu alipokwenda kunaupinzani mkubwa hivyo waondoke wote waende kuitafuta lulu kwani ingekuwa aibu kubwa sana kwa mfalme kushindwa kupeleka zawadi ya mtoto wake kipenzi Mboni.
Ilipotimia majira ya saa kumi na nusu tayari mfalme pamoja na watu wake walikuwa njiani kuelekea katika visiwa vya mikwingwina ili kumtafutia binti yake mpendwa zawadi aliyo ihiyo ihitaji ya lulu.
Ilipotimu majira ya saa saba hivi mchana mfalme paoja na watu wake walikuwa wamesha wasili ng'ambo yapili ya kivuko kuelekea katika kisiwa cha mikwingwina. Mfalme Mbezi alitoa kifaa maalumu cha kukatisha maji kilichounganishwa na nanga nzito ndogo nakufungwa ng'ambo ya kwanza kisha kufungwa katika kamba ndefu ngumu ya manila nene. Mathayo aliyekuwa mlinzi wa Mbezi alipewa jukumu la kwenda mpaka ng'ambo ya Mikwingwina na kisha kutafuta mtimkubwa afunge kwaajili ya kuvukia juu kwaajili ya mikono na kamba ya chini kwaajili ya kukanyaga kwa miguu yaani, kwakifupi kitendo cha kufunga kamba ng'ambo ya kwanza na ng'abo ya pili inaitwa NEMA. Baada ya zoezi lile kukamilika Mathayo alirudi ng'ambo ya kwanza ya mikwingwina na kumwambia Mfalme Mbezi kuwa zoezi limekamilika na hali ya kiusalama ipo madhubuti. Mfalme akaamrisha makamanda wawiliwawili wavuke kwenda kisiwani mikwingina kuleta lulu, Sufiani pamoja na Saidi walikabidhiwa vifaa vya kutendea kazi kama kisu cha almasi kwaajili ya kukatiamadini ya lulu pamoja na upanga, mkuki pamoja na mishale kwaajili ya kujihami. Saidi na Sufiani walianza safari kwa pamoja mpaka ng'ambo ya pili salama. Walipokuwa njiani kuelekea kaskazini mwa Mikwingwina waliona nyoka aina ya chatu wapatao kama 500 hivi wakawazingira na kuwameza kwa fujo

Jumapili, 28 Septemba 2014

KATEGORIA ZA KISARUFI KATIKA SARUFI YA KISWAHILI NA SINTAKSIA.



CHUO KIKUU CHA ARUSHA

KITIVO CHA FANI NA SAYANSI ZA JAMII

MUHTASARI WA SOMO LA SARUFI YA KISWAHILI NA SINTAKSIA

Msimbo wa somo:KISE 330

Jina la somo: SARUFI YA KISWAHILI NA SINTAKSIA.




IMEANDALIWA NA STEPHEN MANYAMA CHARLES UOA.2012-2015.

Uzito wa somo: Credit 3

Hadhi ya somo: Lazima

Ufafanuzi wa kozi.

Sarufi ya Kiswahili na sintaksia ni kozi inayochambua sarufi ya Kiswahili kwa kuzingatia nadharia za sintaksia kama zilivyoasisiwa na wanazuoni wa isimu. Sintaksia ni tawi la isimu linalohusu namna maneno yanavyounda virai na sentensi za Kiswahili. Sintaksia inahusu tungo za lugha ambazo zaweza kuwa ni maneno, virai, vishazi na sentensi. Japokuwa neno ni kipashio cha maumbo, linasadifu kuingia katika sintaksia ya lugha kwani lenyewe lina muundo wake unaotokana na viambajengo vinavyoliunda ambavyo ni mzizi na viambishi.

Kozi hii itachunguza nadharia kadha za sintaksia. Awali tutaanza na ubainishaji wa kategoria za maneno tukizingatia umuhimu wake katika sintaksia na muundo wa virai au sentensi. Kozi hii itazingatia zaidi nadharia za msingi za sintaksia kama vile sarufi miundo virai, sarufi zalishi, Nadharia ya ungoekaji na uambatishaji (government and binding). Katika kozi hii virai na sentensi vitachanganuliwa ili kubaini miundo yake.

Malengo ya kozi

Katika kozi hii wanafunzi wanatarajiwa kufanya yafuatayo:

a) Kuelewa maana ya sintaksia

b) Kutambua kategoria kuu na kategoria ndogo za sintaksia

c) Kueleza umuhimu wa kategoria za sintasia katika kujifunza sintaksia

d) kufahamu nadharia mbalimbali za sarufi miundo:Sarufi miundo virai, sarufi patanishi na uteuzi na nadharia X-bar

e) kuchanganua sentensi kwa mujibu wa nadharia za sarufi miundo

Maudhui ya kozi

1.0 Maana ya lugha na sarufi

Lugha ni nini?

Lugha ni mfumo wa sauti za nasibu zinazotumiwa na watu ili kupashana habari

Sarufi ni nini?

Sarufi ni mfumo wa kanuni za lugha zilizo katika ubongo wa mzawa wa lugha

ambazo humwezesha kutunga sentensi zisizo na kikomo ambazo hukubalika na wazawa wa lugha wanaoifahamu lugha hiyo barabara

2.0 Umilisi na utendi wa lugha

a) Umilisi ni uwezo wa kuzungumza lugha kwa ufasaha alio nao mtu unaotokana na yeye kuzifahamu vilivyo kanuni za kisarufi hata kumwezesha kuzalisha tungo nyingi zisizo na kikomo.

b) Utendi ni utumiaji wa lugha katika mazingira halisi ambao huweza kuathiri maana za maneno kulingana na matumizi yake au na mambo yanayomhusu mzungumzaji mwenyewe k.v. kutokuwa makini au kukosa kumbukumbu, kuongea akiwa amekasirika, kasoro za ala za sauti k.v. mapengo, kigugumizi n.k.

3.0 Tungo za Kiswahili na Vipengele vyake

Lugha ya Kiswahili ina tungo na vipengele mbalimbali kama zilivyo lugha nyingine. Tofauti yake na lugha nyingine zisizohusiana k.v. Kiingereza au Kimasai ni kwamba huhitilafiana katika uundaji wa maneno na mpangilio wa maneno katika tungo. Mathalani, wingi katika Kiingereza hudhihirika mwishoni mwa nomino ilihali katika Kiswahili na lugha dada za Kibantu huonekana mwanzoni mwa nomino. Isitoshe, kivumishi katika Kiswahili hufuata nomino, lakini katika Kiingereza hutangulia nomino. Kwa hivyo japokwa lugha zote zina maneno, virai,vishazi na sentensi, kila moja ina miundo na vipengele vya kisarufi tofauti na lugha nyingine.

4.0 Kauli za vitenzi na aina zake

Kauli ni uhusiano ulipo baina ya kiima na kitenzi (mtenda) au kiima kitenzi

na yambwa (mtenda)

Aina za kauli

Kauli ya kutenda, kutendwa, kujirejea, kutendana, kutendeka,

5.0 Sentensi na aina zake

Sentensi ni kifungu cha maneno chenye maana kamili chenye muundo wa kiima na kiarifu

a) Sentensi sahili

Sentensi sahili ni tungo yenye mana kamili inayoundwa na KN + KT, na ambayo KT ndicho muhimu katika tungo kwani chaweza kusimama peke yake.

Miundo ya Sentensi sahili:

i) Muundo wa kirai kitenzi (KT)

ii) Muundo kirai nomino na kirai kitenzi (KN+KT)

iii) Uchanganuzi wa sentensi sahili

b) Sentensi ambatani

Hii ni sentensi ambayo hundwa na vishazi huru viwili au zaidi kwa kuunganishwa na viunganishi na, lakini n.k.

Miundo ya sentensi ambatani

i) Miundo yenye vishazi sahili

ii) Miundo yenye vishazi sahili + changamani

iii) Miundo yenye vishazi changamani pekee

iv) Miundo yenye vishazi visivyokuwa na viunganishi

v) Uchanganuzi wa sentensi ambatani

c) Sentensi changamani

Hii ni sentensi yenye kuundwa na kishazi huru na kishazi tegemezi

Miundo ya sentensi changamani

i) Miundo yenye vishazi rejeshi

ii) Miundo yenye vishazi – vielezi

iii) Uchanganuzi wa sentensi changamani

6.0 Kategoria za kisarufi

Kategoria ya kisarufi ni kundi la maneno lenye sifa za kisarufi zinazofanana.

Kwa mfano, mtoto, embe, kiti, mti n.k. ni maneno ya kategoria

nomino kwa sababu yana sifa shirika. Maneno ya kategoria moja ya kisarufi yana sifa za kisemantiki, kimofolojia au kisintaksia zinazofananana ambazo ziwapo katika tungo hujaza nafasi karibu ileile.

Nomino – hutaja jina la kitu, huwa mtenda au mtendwa katika sentensi,

huweza kuwa katika umoja au wingi. Kwa mfano: mtoto – watoto, kitu – vitu, embe –maembe.

Kitenzi – huonyesha tendo au hali ya kufanyika kwa kitu. Kwa mfano: cheza, imba, kimbia.

Kivumishi – hueleza sifa ya kitajwa ambacho ni nomino. Kwa mfano: dogo, zuri

Aina nyingine za maneno ni pamoja na kielezi, kiunganishi, kihusishi n.k.

Aina za maneno hutumika kubainisha aina za virai kwani jina la kirai hutokana na kategoria ya kisarufi ya neno kuu.

7.0 Maana ya sintaksia

Sintaksia ni tawi la isimu ambalo linahusu namna maneno yanavyoungana na kuhusiana katika kirai au sentensi. Sintaksia inachunguza namna maneno yanavyojipanga katika sentensi kwa kuzingatia kanuni za sarufi ya lugha husika.

8.0 Mikabala tofauti ya Sintaksia

Uchambuzi wa muundo wa lugha umefanywa na wanasarufi wa nyakati tofauti na kuzua mikabala tofauti kuhusu muundo wa lugha kama walivyouona kwa wakati wao. Mkabala wa awali uliokuwa umejikita katika lugha kongwe kama Kilatini ulikuja kujulikana baadaye kama wa kimapokeo kwani ndio uliorithishwa kutoka kizazi hadi kizazi na kutumika kuchambua

lugha nyingine za dunia. Mkabala mwingine ni ule ulioichambua lugha kwa kuzingatia vijenzi vinavyounda sentensi na ulioasisiwa na Chomsky. Mkabala huu ulijulikana kama mkabala wa kimuundo ambao hata hivyo baadaye ulifanyiwa marekebisho zaidi na mwenyewe Chomsky na waliomfuata.

8.1 Mkabala wa Kimapokeo

Wanamapokeo walichambua sintaksia ya lugha kwa kuainisha miundo ya sintaksia iliyo katika lugha. Kwa mujibu wa wanamapokeo, virai na sentensi zimeundwa na kategoria za kisarufi yaani maneno ambayo kila moja liliainishwa na uamilifu wake kutajwa. Kwa hivyo mwanaisimu alichambua sentensi kwa:

a) kutaja kategoria za kisarufi za maneno yanayounda sentensi

b) kueleza kazi au uamilifu wa kila neno lililounda sentensi.

Kwa mfano: ‘Mama anapika chakula’.

Sentensi hii ilichambuliwa kwa kueleza:

Muundo: Sentensi hii inaundwa na maneno matatu: ‘mama’, ‘anapika’ na ‘chakula’ na kwamba kila neno lina kategoria yake

Kategoria za maneno yanayounda sentensi: ‘mama’ na chakula’ ni nomino za umoja, na ‘anapika’ ni kitenzi kilicho katika wakati uliopo.

Uamilifu wa kila neno: ‘Mama’ ni kiima, ‘anapika chakula’ ni kiarifu.

Aina ya sentensi: Sentensi hii ni kishazi. Hii ni sentensi arifu.

Aidha wanamapokeo walichambua sentensi kwa kubainisha kategoria za maneno yaani aina za maneno kwa mujibu wa maana zake, vipengele vya kimofolojia na au tendo.

Nomino ilifafanuliwa kuwa ni jina la kitu, mtu, mnyama, hali. Nomino huweza kuhesabika au kutohesabika na kwamba huwa na umoja na wingi au umoja tu au wingi tu.

Kitenzi kilifasiliwa kuwa ni neno lenye kudokeza tendo ambalo huchukua viambishi vya wakati uliopo, uliopita au ujao, mtenda ambaye huwakilisha kiima katika kitenzi , mtendwa n.k. Katika sentensi kitenzi hufuata kiima ambacho ni nomino mtenda au kufuatwa na nomino mtendwa au yambwa. Kwa hivyo sentensi ‘ Mama amelala’ ingechambuliwa hivi:

Sentensi hii ina nomino ‘mama’ ambayo ina uamilifu wa kiima cha sentensi yaani mtenda na kitenzi ‘amelala’ chenye uamilifu wa kiarifu cha sentensi. Kitenzi hiki ni sielekezi.

8.2 Mkabala wa wanamiundo kama ulivyoasisiwa na Noam Chomsky

Nadharia ya Sintaksia ambayo mwasisi wake ni Noam Chomsky imejaribu kueleza vipengele vya kisintaksia vya lugha mbalimbali ili kuonyesha jinsi lugha mahsusi zinavyopanga maneno yao ili kupata sentensi.

Lengo la Chomsky katika uchanganuzi wake wa lugha ni kuunda nadharia ya sintaksia ya jumla itakayonyesha vipengele vya kisintaksia vinavyopatikana katika kila lugha na jinsi vinavyotofautiana. Hii inafahamika kama nadharia ya sarufi ya jumla.

Lengo lingine la Chomsky ni kupinga mtazamo wa wanaisimu wa miaka 1950 (wanamapokeo) waliodai kuwa tofauti za lugha hazina ukomo, mtazamo ambao hakuuafiki kwani ulimaanisha kuwa ingebidi kila lugha iwe na nadharia yake. Alidai kuwa tofauti baina ya lugha ni ndogo na kwamba nadharia ya sarufi ya lugha ingeweza kujumuisha lugha zote isipokuwa kwa tofauti ndogondogo tu. Alibainisha kategoria za virai kuwa ni: KN, KT, KV, KE, KH, KU.

9.0 Sarufi miundo virai

Muundo ni mpangilio wa vitu vidogo vilivyowekwa pamoja na kujenga kitu

kikubwa zaidi.

Sarufi miundo virai ni mkabala wa kuchambua lugha kwa kuigawa sentensi katika virai vinayoiunda na kisha kuvichanganua zaidi hadi kufikia neno moja moja lililokiunda kirai.

Tungo huundwa na viambajengo kwa utaratibu maalumu.Tungo za lugha ni neno, kirai, kishazi na sentensi. Virai, vishazi na sentensi huundwa na maneno.

10.0. Muundo wa kirai na sentensi

Kirai, kishazi na sentensi ni vipashio vya lugha vinavyoundwa na viambajengo ambavyo ni vidogo kuliko vyenyewe. Kirai hujengwa na maneno, na kishazi na sentensi hujengwa na virai. Viambajengo vya tungo ndivyo vinavyofanya muundo wa tungo husika.

10.1 Muundo wa Kirai

Kirai ni fungu la maneno yanayohusiana kimuundo lisilokuwa na muundo wa kiima kiarifu. Maneno katika kirai humilikiwa na neno moja ambalo ndilo neno kuu. Kirai hubainishwa na kategoria ya neno kuu. Kwa mfano: KN, KT, KV, KE KH n.k.

Virai huundwa na viambajengo. Kiambajengo ni kikundi cha maneno au hata neno moja pia inayofanya kazi kama kitu kimoja. Kirai, kishazi au sentensi ni mkusanyiko wa viambajengo kadha.

Kirai ni mkusanyiko wa viambajengo vilivyojengwa kuzunguka neno kuu. Kwa mfano, KN huundwa na nomino na vivumishi vyake, kwa hivyo muundo wa kirai ni maneno yanayokiunda yakiwakilishwa na alama za kategoria za maneno hayo.

Kwa mfano: a) ‘Mtoto mdogo’.

Hiki ni Kirai Nomino (KN) kilichoundwa na N (nomino) na V (kivumishi).

Kwa hivyo KN  N+V

b) ‘analima shamba’.

Hiki ni kirai kitenzi (KT) chenye kuundwa na kitenzi (T) na kirai nomino (KN). Kwa hivyoKT  T+KN

10.2 Aina za Virai na sifa ya kila moja

a) Kirai Nomino

b) Kirai Tenzi

c) Kirai Vumishi

d) Kirai Elezi

e) Kirai Husishi

f) Kirai Unganishi

11.0 Muundo wa Vishazi na Sentensi

Kishazi ni kikundi cha maneno kilicho ndani ya sentensi chenye muundo wa

kiima na kiarifu. Kishazi kina muundo sawa na sentensi.

11.1 Aina za vishazi na miundo yake

a) Vishazi ambatani

b) Vishazi tegemezi

11.2 Sentensi na Miundo yake

Sentensi ni kikundi cha maneno chenye maana iliyo kamili. Sentensi ndicho kipashio lugha cha kimuundo ambacho ni kikubwa kuliko vipashio vingine. Vipashio vya lugha ni pamoja na: mofimu, neno, kirai, kishazi na sentensi yenyewe. Sentensi na kishazi huundwa na virai vikuu viwili: KN na KT. KT yaweza kuundwa na kitenzi na nomino, kitenzi na kielezi n.k.

Kwa hivyo S- KN + KT

Sentensi na upatanishi wa kisarufi

12.0 Sarufi geuza umbo zalishi

Nadharia geuza umbo zalishi huonyesha ujuzi alionao mzungumzaji ambao humwezesha kutunga sentensi sahihi na zisizo na kikomo. Uwezo wa mzungumzaji kutunga sentensi zisizo na ukomo unatokana na kufahamu kanuni za kutunga sentensi sahihi ambazo mzawa wa lugha anazijua kutokana na kuwa na umilisi na lugha yake. Kanuni za kutunga sentensi sahihi hubainisha sentensi sahihi na zisizo sahihi.

Kwa mujibu wa nadharia hii, sentensi ina umbo la nje ambalo ndilo linalojitokeza katika usemaji na hata inapoandikwa, na umbo la ndani ambalo huwa limefichika na hujidhihirisha katika umbo jingine wakati wa kuongea (maana).

Nadharia hii imeweza kuonyesha uhusiano wa tungo ambazo japo zilikuwa na umbo la nje tofauti, zina umbo la ndani sawa.

Kwa mfano:

a) Juma anacheza mpira

b) Mpira unachezwa na Juma

S

KN KT

T KN

Juma anacheza mpira

S

KN KT

T KU

N U KN

Mpira unachezwa na Juma

Mfanano wa tungo hizi umekitwa katika maana. Japokuwa sentensi a) inaanza na Juma, na ile b) inaanza na Mpira, mtenda na mtendwa katika sentensi zote ni yule yule.

Mchakato wa kubadili umbo la nje la sentensi a) na kuwa b) umesababisha uchopekaji wa kiunganishi ‘na’ na kiambishi tendwa ‘w’ katika kitenzi ‘cheza’.Kanuni geuzi tendwa ndiyo iliyotumika kuingiza mabadiliko haya.

Sentensi yaweza kubadilishwa kutoka umbo moja hadi jingine

Kwa mfano:

c) John anafanya mtihani na Maria anafanya mtihani

d) John na Maria wanafanya mtihani

Umbo la nje la tungo hizi ni tofauti lakini umbo la ndani ni sawa. Tungo d) imedondosha baadhi ya maneno yaliyo katika c).

Kanuni ya udondoshaji imetumika kudondosha ‘anafanya mtihani’ ambayo imerudiwa katika sentensi c).

Kanuni ya kubadilishana viambishi idadi imetumika kubadili idadi ya mtenda kutoka umoja ‘a- ya ‘anafanya’ iliyotumika kwa John na Maria kila mmoja peke yake, na kuingiza kiambishi cha wingi: ‘wa- ya ‘wanafanya’

13.0. Sarufi miundo virai zalishi

Katika sarufi miundo virai zalishi muundo wa sentensi huelezwa kwa kuchanganua vijenzi vyake ambavyo ni viambajengo. Viambajengo hivi huchanganuliwa hadi kufikia neno moja ambalo hubainishwa kwa kategoria yake ya kisarufi. Uchanganuzi huu wa sentensi huelezwa kwa kanuni ambazo huwezesha kutunga sentensi nyingi zaidi.

13.1 Kanuni za muundo virai.

a) KN  N --- mtoto

Hii ina maana kuwa KN ina N (yaani Kirai Nomino kina kiambajengo kimoja tu ambacho ni nomino). Hii yaweza pia kuelezwa hivi:

KN

N

Mtoto

Hii ina maana kuwa kirai hiki ni neno moja. ‘mtoto’

Kirai chenye viambajengo zaidi kimoja, yaani chenye maneno zaidi ya moja

huelezwa kwa kanuni:

KN N V au

KN

N V

Mtoto mzuri

Hii ina maana kuwa KN kinaundwa na maneno mawili, yaani ‘mtoto mzuri’

Vivyo hivyo kwa Kirai kitenzi (KT)

b) KT  T anakula

Hapa tunaona kuwa KT ina T yaani ina kiambajengo kimoja tu ‘anakula’. Hii inaweza kuelezwa kwa njia ya matawi pia.

KT

T

Anakula

Iwapo KT ina viambajengo viwili, muundo wake huelezwa hivi:

KT  T KN. Muundo huu unaelezeka pia kwa njia ya matawi hivi:

KT

T KN

N

anakula chakula

Vivyo hivyo kwa:

c) KV  V au KV  V E,

KV

V E

mdogo sana

d) KE  E au KE  E E

KE

E E

polepole mno

e) KH  H au KH  H KN

KH

H KN

kwa haraka

13.2 Kanuni za msingi za miundo virai

Kanuni za miundo virai hujidhihirisha katika sentensi. Sentensi ifuatayo

huchanganuliwa kwa kuzingatia kanuni za miundo virai.

‘Mama amepika chakula kingi sana

S----- KN KT

S

KN KT

KN KE

N T N V E

Dada amepika chakula kingi sana

1. S ----------- KN KT

2. KN --------- N V

3. KT --------- T KN KE

4. KE --------- E

5. T ----------- pika

6. N ----------- dada, chakula

7. V ----------- kingi

8. E -----------  sana

9. H ----------- kwa



Katika kategoria zilizokuwa ndani ya Kiswahili ni neno la kategoria gani huchagua kategoria ipi? Makala haya yatajadili maana ya kategoria, yataainisha kategoria mbalimbali za maneno kwa mujibu wa wataalamu, yatajadili kategoria gani huchagua kategoria ipi katika tungo za Kiswahili, yatabainisha sababu zinazopelekea kategoria kuchaguana na kujaribu kuunda kanuni mbalimbali na hatimaye kuhitimisha. Kategoria za maneno ni aina za maneno kadri ya uainisho wake kutegemeana na sifa za maneno husika kuwekwa katika kundi moja. Mfano Kategoria ya Nomino, Kategoria ya vitenzi, kategoria ya vivumishi. Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu (2004) maneno yameainishwa katika makundi nane. Makundi hayo ni Nomino, Kitenzi, Kivumishi, Kiwakilishi, Kielezi, Kihusishi, Kihisishi na Kiunganishi. Ambapo kategoria hizi zimepangwa kulingana na sifa za maneno yanayoingia ndani yake. Kihore na wenzake (2003) wanaainisha kategoria saba za maneno nazo ni nomino, vitenzi, vivumishi, viwakilishi, viunganishi, vielezi na viingizi. Kwa pamoja wataalam hawa wanakubaliana kuwepo kwa kategoria za maneno ingawa wanatofutiana katika idadi ya aina za kategoria.Tofauti hizi zinatokana na baadhi ya maneno yanaonekana kutoingia katika kategoria zilizoainishwa. Kwa mfano kategoria ya maneno kama kwa, la, cha, vya na wa kwa mujibu wa Kihore na Wenzake (2003) yanaonekana kuwa viunganishi lakini tukiangalia dhima yake katika lugha ni kuhusisha aina za maneno mengine ambayo ni ya kategoria tofauti au kategoria finyu tofauti. Vile vile tatizo linajitokeza pale ambapo maneno haya yanapofanya kazi tofauti tofauti katika lugha katika kigezo cha semantiki. Maneno ya lugha mfano neno na linafanya kazi kama kiunganishi na pia kama kihusishi. Hebu tuangalie mifano ifuatayo; Mifano: i) baba na mama ii) Amepigwa na Johari Katika tungo ya kwanza neno “na” limefanya kazi kama kiunganishi na katika tungo ya pili limefanya kazi ya kuhusisha kitenzi amepigwa na nomino Johari. Kwa kuliona tatizo hilo Kamusi ya Kiswahili Sanifu ikaamua kuongeza aina ya nane ya maneno yaani Kihusishi. Tatizo lingine linajitokeza katika baadhi ya maneno hususani kihisishi mara nyingine hutokea katika umbo la Kirai hususani kirai nomino, Mfano Mungu wangu! Mtume! Yesu! Maneno hayo huweza kubainishwa kama vihisishi ingawa ni nomino. Mwingiliano huu ndiyo unaoleta matatizo katika taaluma ya sintaksia, na ipo haja ya kufanya uanishaji wa aina za maneno tena au tukubaliane kuwa baadhi ya maneno ya tabia ya kughairi kanuni za lugha. Sanjari na hilo neno aina ya kitenzi kimekuwa na tabia ya kubadili maana za tungo kadri kinavyonyambulishwa. Kitenzi kinabeba dhima ya mufidi, ufanyizi, unyume, uambatani, mwao kwa uchache kwa mujibu wa Khamis (2008). Kutokana na kitenzi nomino huzalishwa kwa sababu hiyo twaweza kusema bado tunahitaji mchakato utakaotuwezesha kutafuta ufumbuzi wa mwingiliano wa aina hizi. Ingawa kuna mwingiliano huo lakini ni jambo la msingi kuangalia uhusiano wa maneno katika taaluma ya sintaksia . Katika kubaini uhusiano huo tunaangalia neno la kategoria gani huchagua kategoria nyingine, hatua ya kwanza tunaweka vikundi mbalimbali vya maneno ambavyo huashiria kuwepo kwa uhusiano wa karibu wa baadhi ya maneno. Wataalam mbalimbali wamebainisha vikundi vya maneno hayo. Habwe na Karanja (2007:154) wanaainisha maneno katika makundi matatu ambavyo ni kundi Nomino (KN), kundi tenzi (KT) na kundi husishi (KH). Chomsky na Halle (1968:08) wao wanachanganua tungo sentensi kwa kuainisha fungu Nomino (KN) na fungu Tenzi (KT). Hii ina maana kwamba wanatambua kuwepo kwa kundi na hivyo kuona kuwa maneno yanachaguana. Katika mjadala huu maneno yanawekwa katika makundi yafuatayo; Kikundi Nomino (KN), Kikundi kitenzi (KT), Kikundi husishi (KH), Kikundi vumishi (KV) na Kikundi elezi (KE). Katika ugawaji wa makundi haya neno linalotawala maneno mengine hukipatia jina kikundi hicho, mfano katika kundi nomino lifuatalo; Baba mdogo katika kikundi nomino hiki neno Baba linatawala neno mdogo, nomino baba inatawala kivumishi mdogo. Kwa kuchunguza vikundi hivyo vya maneno, tunaweza kugundua kuwa kategoria zina tabia ya kuchaguana. Jambo la kujiuliza ni kwa nini kategoria huchaguana? Kategoria huchaguana kwa sababu zifuatazo: Sababu ya mofo-sintaksia, Katika sababu hii tunazingatia mahusiano ya maumbo ya maneno yanavyopelekea kuchaguana. Msisitizo unawekwa katika upatanisho wa kisarufi unavyoruhusu kategoria anuai kuchaguana. Wazo hili pia limeelezewa na Khamisi kupitia kazi ya Steere (1870) anaeleza kuwa alijishughulisha na kupata maana tu iletwayo na umbo au sauti, hivyo ikafaa kuitwa Maelezo ya Sauti – maana. Pia Khamisi anaeleza “Mchango wa Steere tunaweza kusema kuwa wa kimofolojia na elezi bila kuwa na ufafanuzi” Mfano: Mtoto mzuri N V Kitoto kizuri N V Vitoto vizuri N V Kwa hivyo katika data hiyo hapo juu, maumbo ya maneno yamesababisha kuchaguana kwa maneno hayo. Pia katika data ifuatayo utagundua kuwa maumbo ya maneno pia yanaweza sababisha kutochaguana kwa maneno; Mtoto kizuri Kitoto mzuri Vitoto kizuri Ukichunguza data hiyo unagundua kuwa maneno hayo hayawezi kuchaguana, kwani maumbo ya maneno hayo hayaruhusu viambishi awali katika maneno yanayofuata. Khamis (2008:4), anaeleza juu ya unyambulishaji usio na mipaka na unyambulishaji wenye mipaka. Hii inaonesha kuwa ni sababu nyingine ya kategoria ya maneno kuchaguana. Pia Guthrie (1962:203) kama anavyonukuliwa na Khamis (2008:5) unyambulishaji wenye mipaka huathiri tabia ya kitenzi kisintaksia kwa kuongeza yambwa, kupunguza yambwa au kutofanya chochote kile kwenye kitenzi, anaendelea kuzungumzia aina za minyambuliko kama fanyizi, mufidi, ambatani, nafsi, tendwa, uwezo, tuamo na nyume ambayo hupelekea kitenzi kuteua kategoria za maneno. Mfano wa mnyambuliko mufidi, Neno shika kabla ya kunyumbulishwa linaweza kuchukua nomino mbili mfano baba ameshika kikombe. Lakini kitenzi shika kinaponyumbulishwa kwa kuongeza –i- tunapata shikia hivyo tunaweza kusema baba amemshikia mwalimu kikombe. Hivyo kitenzi hicho kimechukua nomino tatu. Lakini hatuwezi kusema baba ameshika mwalimu kikombe. Kwa sababu kitenzi shika hakidhibiti nomino tatu. Pia katika mnyambuliko fanyizi husababisha kitenzi kibebe Nomino. Mfano; Imb –ish-a watu, kiambishi –ish- kinafanya kitenzi imba kuchagua nomino watu. Ikifanya dhima ya kutendesha. Lakini hatuwezi kusema imbisha ng’ombe, tungo hii haina mantiki, kwani ng’ombe hawezi kuimba. Mnyambuliko wa utendwa pia unasababisha kitenzi kuteua kategoria ya maneno; Mfano, chez-w-a, fund-w-a vitenzi hivyo vinalazimisha kuteua kategoria ya nomino au kielezi. Mfano Mtoto amechezwa unyago Hapa kitenzi chezwa kinaruhusu nomino unyago, kwa sababu unyago unachezwa, lakini hatuwezi kusema mtoto amechezwa nguo, ingawa nguo ni nomino kama ilivyo unyago, lakini nomino hiyo haiwezi kuchezwa kwasababu kimaana tungo hii inakataa. Dhana ya kitenzi si elekezi hujitokeza katika kitenzi ambacho hakiruhusu kuchukua nomino nyingine. Hapa kitenzi kinawekewa hali ya utendeka inayojidhihirisha katika umbo la –k na –ik. Mfano: kikombe kimevunjika Maji yamechemka Pia sababu ya Kisemantiki, ambapo maneno huchaguana kwa kufuata mantiki ya maana inayokusudiwa. Mfano: anakunywa ugali T N Pamoja na ukweli kuwa kitenzi kunywa ni elekezi (kinaweza kubeba nomino, sababu za kisemantiki zinakataa, huwezi kunywa ugali. Kwa kuzingatia kanuni ifuatayo ya kitenzi kunywa: Kunywa (T – ele) - ------ + [___kiminika] +maji, soda, shalubati, bia Sanjari na hilo kitenzi cha lugha ya Kiswahili kina tabia ya kubeba dhana mbalimbali na kusababisha maana kutofautiana. Kwa mfano kitenzi chenye mnyambuliko mufidi kina dhima za kisemantiki zifuatazo kutokana na kuteua nomino zenye kubeba nduni tofauti tofauti kama ifuatavyo: Mfano: pik – i –a + N T + N +sababu +mahali +faida Mfano: a) pikia wali (faida) b) pikia nje (mahali) c) pikia nini? (sababu) Hivyo maneno huweza kuchaguana kutokana na sababu za mofosintaksia, kisemantiki na sababu zinazotokana na tabia mbalimbali za vitenzi. Matumizi ya maneno katika tungo yoyote ile hutegemea sana mahusiano kati ya neno na neno ili tungo hiyo ilete maana, hivyo sio tu kusema Nomino inaweza kukaa na Kitenzi, inabidi kujiuliza maswali zaidi, je kila nomino itakaa karibu na kitenzi fulani? ni muhimu kuzingatia sababu zote zinazosababisha maneno kuchaguana ili kujenga maana katika lugha.

Jumanne, 9 Septemba 2014

KIDAHIZO KATIKA KAMUSI.

Swali:-    Kidahizo ndiyo msingi wa kamusi. Fafanua kauli hii ukizingatia maumbo ya maneno yanayoweza kukaa katika nafasi ya kidahizo.


    Swali litajibiwa kwa kuligawa katika sehemu tofauti ili liweze kueleweka vizuri. Ambapo  tutaangalia maana ya kidahizo, maana ya kamusi, maelezo ya kina kuhusu kidahizo na kisha tutaangalia jinsi maumbo ya maneno yanavyoweza kukaa katika nafasi ya kidahizo.
Istlahi kidahizo imefafanuliwa na wataalamu wengi miongoni mwao ni pamoja na hawa wafuatao;
TUKI (1981) wanaafasili kidahizo kama neno linaloingizwa katika kamusi kwa chapa ilyokolezwa.
BAKIZA (2010) nao wanaeleza kuwa; kidahizo; ni neno linalochapishwa kwa hati zilizokozwa na pengine kutiwa rangi kwenye kamusi ambalo taarifa zake zinafanuliwa. Tunaweza kuwaunga mkono wataalamu hawa fasili yao kwani kidahizo huwa katika wino uliokolezwa na huingizwa katika kamusi ili kutolewa maana. Lakini kwa fsili ya jumla tunaweza kusema kuwa,
Kidahihizo ni neno linaloingizwa katika kamusi ili liweze kufafanuliwa kwa kupatiwa maelezo yanayohusu taarifa za kisarufi, maana, matumizi, etimolojia semi mbalimbali za lugha na nyingine.
Oxford (2010) wanaeleza kuwa; kamusi ni kitabu ambacho huwa kinaorodha ya maneno ya lugha fulani katika mpangilio wa alfabeti na huelezwa maana ya maneno hayo. Au kamusi ni orodha ya maneno yaliyopo katika mfumo wa eletroki kwa mfano yanaweza kuhifadhiwa katika kompyuta. Faslili hii ionekena kuwa na mashiko kwani kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia si sahihi tene kufasiri kamusi kama kitabu bila kuihusisha na elektroniki katika uhidhi wake.
Kamusi hutungwa ikiwa na malengo mbalimbali kulingana na mahitaji na matumizi ya taaluma au mtumiajia fulani. Mfano zipo kamusi za uwanja husika kama sheria, isimu, falsafa na nyingine. hivyo uteuzi wa msamiati hulingana na uwanja unaotungiwa ambapo kama ni uwanja wa jumla lazima tutakuta msamiati wenye lugha sahili au lahisi. Hivyo msamiati unaokusanywa na kuwekwa katika kamusi ili kufasiliwa ndiyo huitwa kidahizo. Vidahizo hufafanuliwa kwa kupatiwa taarifa za kina ili anayetaka taarifa hizo azipate bila utata wowote.
Katika kamusi za Kiswahili vidahizo huwa na maneno ya kawaida yanayotumika katika Nyanja mbalimbali za mawasiliano miongoni mwa wazungumzaji wa Kiswahili. Msamiati unaoingizwa katika kamusi kama vidahizo hukusanywa katika sehemu tofauti  mfano machapisho mbalimbali, kama matini magazeti na vitabu mbalimbali.
Kidahizo kimegawanyika katika sehemu mbili yaani kidahizo huru na kidahizo mfuto. Hii ni kwa mujibu wa TUKI (2000). Kidahizo kikuu katika kamusi huwa ni umbo la msingi la neno. Mfano “lim.a” “li.a” wakati kidahizo mfuto, ni kinyambuo  kisichotumika sana au neno ambatani ambalo limeingizwa ndani ya maelezo ya kidahizo kikuu. Na kusoma maelezo ya maana ya kisarufi. Iwapo halitumiki sana au halijapata kutumika lakini likatumika tu kwa siku moja hupatiwa maana ya kisarufi tu. Kinyambuo cha kitenzi ambacho kina kategoria tofauti huingizwa kama kidahizo mfuto ndani ya umbo la msingi bila maelezo ya maana na kisha huingizwa tena kama kidahizo kikuu katika herufi ya alfabeti inayohusika.
Kidahizo kama msingi wa kamusi, hupangwa kwa kufuata utaratibu wa alfabeti. Kwa kila ukurasa neno la kwanza na la mwisho katika ukurasa limechapwa sehemu ya juu ya ukurasa ili kumwongoza msomaji atambue nafasi ya neno analohitaji au analotafuta, iwapo lipo katika ukurasa anaousoma au lipo nyuma au mbele ya ukurasa unaohusika maneno ya kumuongoza msomaji humwezesha kupitia kamusi na kugundua neno unalotaka kuliko kusoma ukurasa na kila kidahizo ili kupata neno unalotafuta.
Kidahizo ni msingi wa kamusi kwa kutokana nacho ndipo tunapata maana ya maana ya neno, etimolojia yake, matumizi na matamshi yake. Kwa hiyo bila kidahizo hatuwezi kuwa na kamusi. Msamiati wote unaokusanywa huwa ni kwa ajiri ya kutolewa maana katika kamusi ili kusaidia watumiajia wa lugha Fulani au wenye kuhitaji kujua msamiati wowote kutumia kamusi. Kwa hiyo naweza kusema hakuna kidahizo hakuna kamusi. Huo ndiyo umuhimu wa kidahizo katika kamusi.
Baada ya maelezo hayo mengi sasa tuone maumbo yanayoweza kutokea katika kamusi kama kidahizo.  Maumbo hayo ni kama haya yafuatayo.
Maumbo sahili; haya ni maumbo yanayoumbwa kwa neno huru yaani lisilo na utegemezi au lisiloweza kuambishwa.
                    Kwa mfano; maneno kama
                “barua”, “nyumba”, “bakuli” na “baba”.
Maneno haya ni huru. Hivyo maumbo haya huingizwa  katika kamusi kama kidahizo.
Maumbo ambatani; haya ni maumbo ya maneno ambayo huumbwa kwa kuunganisha maneno mawili tofauti, mfano nomino na kitenzi, nomino na nomino na mengine. Katka kamusi maneno haya huchukuliwa kama neno moja lenye kuwakilisha dhana fulani. Kwa mfano maumbo haya yametoka katika kamusi ya tuki (2001).
Kipeleleza-nyanbizi nm vi- [ki-vi-] asdic.
Kipazasauti nm vi- [ki-vi-] loud speaker.
Kipashamoto nm vi- [ki-vi-] chafing-dish.
Kipimahewa nm vi- [ki-vi-] barometer
Kitanguakimbanga nm vi- [ki-vi-] anticyclone
Maneno yote haya ni mwambatano lakini katika kamusi husimama kama neno moja na siyo kuwa tunaangalia maana ya neno moja moja. Hapa nisawasawa na maneno ya nahau, misemo nayo katika kamusi huchukuliwa kama neno moja lenye kuwakilisha dhana fulani. Mfano; TUKI (2001)
Kifungua kinywa,
 kick the bucket,
tia  nanga.
Maumbo changamani, ni maumbo ya maneno yanyokuwa na uchangamani. Ni maneno ambayo hayawezi   kusimama pekee katika kamusi. Maneno haya huwa na viambishi vinavyotenga mzizi wa  neno pia maneno haya hutengwa ili kuonesha uwezo wa kunyumbuliwa au kuchukua viamshi tofauti tofauti. Mfano;

M.toto 
M.tu
Nufaik.a
Nui.a
Maneno haya huweza kunyumbuliwa na kuleta maana nyingine tofauti na maneno sahili ambayo hayawezi kunyumbuliwa. Kwa mfano neno “nui.a” linaweza kunyumbuliwa na kupata maneno mengine kama, nuilia,nuilika, nuiana nuiza.
Maumbo hulutishi, haya ni maumbo ambayo kutokea kama kidahizo katika kamusi. Maneno haya huundwa kwa kuunganisha sehemu mbili za maneno tofauti na siyo kuunganisha maneno mazima. Kwa mfano;
Telephone
Mobitel
Telefax
Maumbo ya akronimia, haya ni maumbo yanayoingizwa katika kamusi kama kidahizo. Maumbo haya huwa katika ufupisho na huwakilishwa kwa herufi kubwa ambazo kila herufi hubaeba dhba Fulani. Mfano; kutoka Oxford (2006).
ISBN International Standard Book Number
ISA Industry Standard Architecture
ISDN Integrated Services Digital Network
SAD Seasonal Affective Disorders
Akronimia hizi hutokea upande wa kidahizo kuwakilisha maana  ama dhana iliyondefu kuwa katika maneno machache.
Maumbo rejerezi, katika kidahizo kuna maumbo ya maneno ya kumfanya msomajia arejelee neno jingine ili kupata ufafanuzi zaidi, maneno yanayorejelewa katika kamusi huoneshwa kwa mshale. Mshale huu ulenga kumuonesha msomaji kulitafuta neno analooneshwa. Kwa mfano;
Pally   → PAL
Pas.try  →see also CHOUX PASTRY
Pipe  → see also PIN PIPES
Mshale huu huwekwa baada ya kuwa taarifa zote kuhusu kidahizo hicho zimetolewa, na huenda kunahitajika maaelezo ya ziada kuhusu neno hilo kwa hiyo msomaji huoneshwa neno jingine kwa mshale ili aone tena maelezo hayo.
Maumbo dondoshi, haya ni maumbo ambayo huingizwa katika kamusi kama kidahizo baada ya sehemu ya neno hili kudondoshwa. Mfano wa maumbo hayo ni kama vile; kutoka katika Oxford (2006).
Phone kutokana na neno telephone
Gram kutokana na neno telegram.
Bike  kutoka na neno bicycle
Maumbo haya fupishi tunayakuta katika kidahizo cha kamusi na hubeba maana ambayo inapatikana katika neno zima ambalo halijafupishwa.
Maumbo radidi, haya ni maumbo ya neno linalojirudia rudia katika kamusi. Neno hili hubeba dhana  moja katika kamusi. Kwa mfano maneno kama,
Uramberambe nm [u-] coconut kernel
Mzengazenga nm mi-n[u-i] carrying two things by using a pole across the soulder
Mzikoziko nm mi [u-li- ] ipecacuanha.
Mnyunginyungi.
Maneno haya hubeba dhana moja inayowakilishwa na uradidi huo.
Maumbo mengine yanayoweza kuingizwa katika kamusi kama kidahizo ni maumbo ya homonimia. Maneno haya huwa na maumbo sawa na matamshi sawa lakini maana huwa tofauti. Katika kamusi huingizwa kama vidahizo vyenye maana tofauti na maana hizo hutofautishwa kwa kupewa namba.
Mfano
Kaa1.
Kaa2,
Kaa3
Panda1,
Panada2
Panda3
Vidahizo hivyo huonekana katika kamusi kama ilivyo mifano hapo juu.

Kwa kuhitimisha, tunaweza kusema kuwa uorodheshaji wa vidahizo katika kamusi hutegemea lengo la kamusi. Mfano kama kamusi ni ya kisheria huorodhesha vidahizo vyake katika  misingi ya kiseria. Maana za msingi ndizo huorodheshwa kwanza na kufuatiwa na maana zilizozuka baadaye au maana zinazohusishwa na neno hilo. Kidahizo ni cha msingi katika kamusi kwani huonesha herufi rasimi zinazopaswa kuunda neno.

Marejeo
BAKIZA (2010) Kamusi ya Kiswahili Fasaha. Kenya: Oxford University Press.
Mdee, J. S. (2010) Nadharia na Historia ya Leksokografia. Dar es Salaam: TUKI.
Oxford (2010) Oxford Advanced Learner’s Dictionary. New York: Oxford University Press.
TUKI (2001) Kamusi ya Kiswahili-Kiingereza. Dar es Salaam: TUKI.
TUKI (2004) Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Dar es Salaam: TUKI.
TUKI (2006) English-Kiswahili Dictionary. Dar es Salaam: TUKI

MATUMIZI YA MISEMO MAGAZETINI:

 
         Misemo magazetini hutumika kwa namna tofauti. Matumizi haya ya misemo hutumiwa moja kwa moja kwenye vichwa vya habari au katika maelezo. Baadhi ya vichwa vya habari hutofautiana na mada ambazo huwa zinakuwemo  ndani ya habari.Hii ina maana kuwa misemo inayotumika huwa na maana iliyotofauti kabisa na maana inayoonekana magazetini.Misemo mingine tumeionyesha kwenye kiambatisho.  Ngoja uangalie mifano ifuatayo:
a)      Nesi  Kitete ajikaanga (Mtanzania, mei, 23,2011.)
b)      Sarakakasi za Sitta Mwakyembe CCJ (Mtanzania, Mei 9, 2011).
c)      Vigogo CCM  wakaangwa (Manzania, Mei,23,2011)  .
d)     Spika, Zitto jino kwa jino, Mkulo  apigilia msumali wa mwisho(Uhulu, Juni, 14, 2011).
e)      Ujamaa wampofusha Mukama(Rai,mei 19-25,2011).
f)       Lady Jaydee kutembea uchi live(Sani,Mei, 14,2011).
g)      Akina Ukwa waja tena (Kiu, ya jibu Juni, 23,2011).
h)      Ngeleja kitanzini(Uhuru, Juni; 6, 2011).
i)        Mashabiki Yanga wafurika kushuhudia majembe yao (Bingwa, Juni, 14, 2011).
j)        Ulimwengu ndiye muuaji (Uhuru Juni 6, 2011).
k)      Morocco yafanya mauaji (Uhuru, Juni 6, 2011).
l)        Mbowe balaa Dar (Majira, juni,6, 2011) .
m)    Mganda awasili kumvaa Mwakyembe(Bingwa Mei, 20 , 2011).
n)      Lowassa amkatia Kiwete rufaa (Mwananchi, juni, 16, 2011).
o)      UPDP kuunguruma Dar kesho (Mtanzania,Mei,25,2011).
p)      CDA yakabwa koo na kamati ya bunge(Bingwa,Mei, 20,2011).
Katika mifano hii, ni dhahili kuwa maana inayoonekana katika msemo hii sivyo ilivyo katika maelezo au habari nzima. Mfano, katika (a) siyo kwamba ‘nesi alijikaanga kiaangoni’ bali alijiweka katika mazingira magumu ya kuendelea na kazi baada yahuduma  kumzalisha mama
                                                                         8.
 na mwanae kufichwa. Pia katika (f) haimaanishi Ukwa waigizaji wa Nigeria bali kuna vijana waliojifananishwa na waigizaji hao. Katika (h) ‘majembe’ haimaanishi majembe vifaa bali anamaanisha wachezaji wapya waliosajiliwa na timu ya Yanga.Mifano mingine mingi tutaitolea maana katika sehemu inayofuatwa.
                                                                     
4.1.KWA NINI MAGAZETI HUTUMIA MISEMO:
Kihole (2004) anasema kuwa ; ‘ni kwa hali hii ya kushangaza kile kinachotajwa katika mada hiyo ama hufanya baadhi ya wasomaji kukosa hata hamu ya kufikiria kununua magazeti haya au kuwachochea watu kufanya juhudi za kuyapata magazeti hayo’. Hivyo baadhi ya magazeti hutumia misemo ili kuvuta umakini wa wasomaji. Ngoja sasa tuangalie baadhi ya misemo ambayo huweza kuvuta wasomaji.
a)      Nilitema big G kwa karanga za kuonjeshwa
b)      Ray C akimbia nchi.
c)      Ngono Big Brother sasa(Kiu ya Jibu,juni,22,2011).
d)     Nilipopiga ramri kumtafuta Mungu(Kiu ya jibu,Juni,22,2011).
e)      Lady  Jay dee kutembea uchi(Ku ya jibu,Juni,22,2011).
f)       Kituo cha kuoshea nyeti za kike Dar(Sani,Mei,11-14).
g)      Mganda awasili kumvaa Mwakyembe (Bingwa Mei,20,2011).
h)      Spika Makinda mbumbumbu anasimamia asichokijua (Rai,Juni,20,2011).
i)        Freemason na ugaidi katika kanzu ya uislamu (Mtanzania,Juni,17,2011).
j)        Wanaume kumeza vidonge vya kuzuia mimba(Uhuru, Juni, 7-14,2011).
k)      Sauti ya radi awa makamu wa Rais(Ijumaa mei, 20, 2011).
l)        Waziri, changu wateta kwa nusu saa Dom(Ijuma,Julai,15,2011).
m)    90% mastaa wauza ngono bei chee(Ijumaa, Julai,15,2011).
n)      Badra aanika chachandu zake adatisha midume(Ijumaa,Julai,15,2011).
o)      Mchumba aliyevua nguo (Dimba, Juli,17,2011).
p)      Linah sina mtu sasa niko single(Sani,juni,12,2011).
q)      Mrembo anaswa akichimba dawa hadharani(Iumaa,Julai,15,2011).
                                                            9.
Kwa kuitazama  misemo hii katika vichwa vya magazeti  tunaweza kubaini kuwa inavutia wasomaji hata kununua magazeti ili kupata taarifa iliyomo ndani ya gazeti hilo. Kutokana maoni ya Kihole (2004) anaposema kuwa ni kutokana na matumizi ya misemo hiyo wasomaji huweza kukatishwa tamaa au kufanya juhudi za kuyapata magazeti hayo, tumeshuhudia magazeti mengi yakitumia misemo hiyo ili kufanikisha
nia ya wasomaji. Mfano gazeti la sani, Ijumaa na Kiu.

1.1.KUSISITIZA JAMBO:
Katika utafiti wetu tumegundua kuwa magazeti hutumia misemo, na misemo hiyo huwa inajirudiarudia katika magazeti mengi. Misemo hii hulenga kuweka msisitizo juu ya jambo lilopita, lililopo au lijalo. Mfano misemo tuliyoitumia katika utafiti wetu baadhi inasisitiza juu ya mambo yaliyokuwepo katika kipindi hicho cha utafiti ulipofanyika. Ngoja sasa tuione baadhi ya misemo hiyo.
a)      Tibaijuka ang’aka(Mtanzania,Mei,20,2011).
-Hi ilkuwa kipindi cha mchakato wa watu kurudisha ardhi walizochukua na wananchi bila kukubaliwa na serikali.
b)      Wabunge CCM wakaangwa (Mtanzania, Mei,23,2011).
Misemo hii imesikika sana kipindi cha wabunge wanahusihwa na migogoro ya chama   ilyojulikana kama (kujivua gamba).
c)      DC walimu wa shule za kata wasiitwe Voda fasta.
d)     Kujivua gamba hakutoshi.
Katika mifano hii misemo mingine huibuka kulingana na mada iliyopo na baadae misemo hiyo haisikiki tena. Hivyo ni kutokana na msisitizo huo wasomaji huweza kuwa na ufuatilizi juu ya tukio fulani kulingana na jinsi linavyotokea mara kwa mara.


                                                                 
1.2.MAANA YA MISEMO MAGAZETINI:
 Katika utafiti huu tumegundua kuwa magazeti hutumia misemo mbalimbali yenye maana tofauti. Kulingana na nadhalia iliyotumika kuchambua utafiti huu tumeona kuwa kazi ya fasihi huwa haina maana moja hivyo maana inaweza kutokana na kazi iliyopo au kulingana mukutadha uliopo. Hivyo maana ya misemo mingine hutokana na mukutadha wa kazi iliyopo. Hivyo katika maana ya misemo  hii tuliyotoa tumezingatia jinsi misemo hii ilivyotokea magazetini.  Mfano wa ,misemo hii ni kama ifuatavyo;
a)      Kalenga aipiga tafu Vodacom miss Bagamoyo(Mtanzania,Mei, 20,2011).
-‘Kupiga tafu’       kusidia .
b)      Aahidi kuanika hadharani vielelezo walivyoshiriki(Mtanzania,Mei, 20, 2011).
                -‘Kuanika’ maana yake ni kuweka wazi.
c)      Azzani asiwe mbuzi wa kafara CCM (Rai, Mei, 19-25,2011).
-‘Kuwa mbuzi wa kafara maana yake’ asiangaliwe kama mkosaji kutokana na makosa
                    yanayofanywa na wakuu wake wa kazi.   
d)     TAKUKURU inabweka lakini haing’ati(Rai, mei, 19-25, 2011)
-‘Hii ina maana kuwa takukuru inatishia lakini haitendi.

e)      Niyonzima aotambawa jangwani(Bingwa, Mei, 20,2011).
-Kuota mbawa maana yake ni kushindwa kufikia mwafaka.

f)       Nyota wa Man U walipoanika vifaa vyao kwenye ‘pati’Bingwa, (Mei,19-25,2011).
           -Kuanika vifaa maana yake walikuusanyika na nakujumuisha wake zao. Vifaa ni
wanawake.
g)      Mshindi wa Tanzania ajishebedua ‘BBA’.(Bingwa, Mei,19-25,2011).
-Kujishebedua maana yake kujifanya hutaki kitu fulani huku unakitaka.

h)      Blatter amekalia kutikavu FIFA? (Majira,23,2011).
-Kukalia kuti kavu maana yake amejiweka katika nafasi ngumu ya kazi yake.
i)        Bimman abwaga manyanga (Majira,Mei,23,2011).
-Kubwaga manyanga maana yake kuacha kazi.
                                                           11.

j)        Harambee ya Yanga yadoda (Uhuru, Mei, 3,2011).
-Kudoda maana yake kushindwa.

k)      Wadai hukumu inanuka rushwa(Majira,Mei,23,2011).
-Kunuka rushwa ina maana kuwa kuna hali ya kutoa rushwa katika hukumu hiyo.
l)        Mwakalebela aibwaga TAKUKURU.
-‘Kuibwaga’ ina maana ya alishinda kesi iliyomkabili kuhusu TAKUKURU.
Hivyo kama tulivyoeleza kabla hatujaanza kutoa mifano hii kuwa kazi ya fasihi huwa haina maana moja, nidhahili kuwa maana nyingine katika mifano hii imetolewa kulingana na muktadha wa kazi yenyewe au taarifa ilivyo kwenye magazeti.
Waandishi wa magazeti nchini Tanzania wanatumia misemo katika magazeti, kwanza ni kwa sababu ya kutaka siko la magazeti yao,hii ni kwa mujibu wa mwafunzi mmoja mwenye namba ya usajiri (2009-04-03894). Anasema kuwa waandishi hutumia misemo katika vichwa vya habari kwa kudokezea kile kitakachokuwa ndani ya habari yenyewe.Mfano ‘endelea na habari hii ndani upate uhondo’ ‘usijinyime uhondo huu’ Hivyo misemo hii imekuwa chanzo cha waandishi kuuza kazi zao. Mfano gazeti la SaniIjumaa, Kiu.
Pia kwa muuza gazeti katika kituo cha mabasi kilichoko ubungo jijini Dar es salaam namba ya simu 0713750941)  anasema kuwa amekuwa akiuza magazeti kwa muda mrefu na kusema kuwa magazeti yanayonunuliwa saana ni yale yenye maneno yanayovutia.
hivyo tukizingatia maoni na maelezo ya watu hawa tunaweza kukubaliana nao kwani tunaona maagazeti mengi yakitumia misemo mingi.   


                                                    HITIMISHO:
        Kwa kuhitimisha tunaweza kusema kuwa misemo ni kipengele ambacho ni kipana sana kwani katika utafiti wetu tumegusia tu misemo bila kangalia dhima zake, fani na maudhui yake. Hivyo ni bora zaidi kufanyike uchunguzi mwingine ili kuweza kubaini vipengele hivyo vya fani na maudhui. Vile vile misemo mingi huanza kama misimu na ikitumiwa sana huweza kuwa na mashiko na kutumika maeneo tofauti.
                                                                       

                                                          
KIAMBATISHO.
1.      Tibaijuka ang’aka.
2.      Nesi kitete ajikaanga.
3.      Kalenga aipiga tafu Vodacom miss Bagamoyo.
4.      Sarakasi za sitta Mwakyembe CCJ.
5.      Akili kuanika hadharani vielelezo walivyoshiriki.
6.      Vigogo CCM wakaangwa.
7.      Wafumania nyavu 10 kukumbukwa.
8.      UPDP kuunguruma Dar kesho.
9.      Ujamaa wampofusha Mkama.
10.  Azzan asiwe mbuzi wa kafara.
11.  Wizara ya elimu imulikwe.
12.  Takukuru inabweka lakini haing’at.i
13.  Gamba laCCM halivuliki, ibueni mafisadi.
14.  Mganda awasili kumvaa Mwakyembe.
15.  Nyota wa Man U walipoanika vifaa vyao.
16.  Mshiriki wa Tanzania BBA ajishebedua.
17.  Mbowe balaa Dar.
18.  Bimman abwaga manyanga.
19.  Wadai hukumu inanuka rushwa.
20.  CDA yakabwa koo na kamati ya bunge.
21.  Mwakalebela aibwaga TAKUKURU.
22.  Harambee ya Yanga yadoda.
23.  DC walimu wa shule za kata wasiitwe Vodafasta
24.  Ris wa zamani wa FIFA amkingia Blatter kifua
25.  Wamer amkaanga Bin Hamman
26.  Sauti ya radi awa makamu wa Rais
27.  Kujivua gamba hakutoshi
28.  Balozi wa Tanzania UK katikati ya mkutano.
29.  CCM itambue ugumu na urefu wa gamba.
30.  Mkata  tawi Gbagbo hakumsikiliza Odinga kawasikliza mijusi
31.  Basi lakanyaga kombe la Real Madrid
32.  Ulimwengu ndiye muuaji
33.  Kauli hizi za viongozi CHADEMA mauti yetu
34.  Mateja wageuza kituo cha mabasi ‘Gesti bubu’
35.  Kiburi chamuondoa duniani
36.  Spika Zitto jino kwa jino
37.  Kujivua gamba si ndoto ya mchana
                                                                      15.
38.  Tulivyozunguka kuitafuta vaselini Kampara
39.  Mashabiki wafurika kushuhudia majembe yao.
40.  Basena akunwa na beki wa Motema pembe.
41.  Wyne Rooney apandikiza nywele.
42.  Ngeleja kitanzini.
43.  Wanaume kuanza kumeza vidonge vya kuzuia mimba.
44.  Ikulu – viongozi wa dini si Malaika.
45.  Lady Jaydee kutembea uchi live.
46.  Kituo cha kuoshea nyeti za kike Dar.
47.  Wabunge wamchefua Spika Makinda awafananisha na watu wa kariakoo.
48.  CCM mnahangaika na Lowassa CHADEMA haoooo..
49.  Pinda hajui idadi ya mawaziri wanaoishi hotelini.
50.  Freemasoni na ugaidi ndani ya kanzu yabuislamu.
51.  Julio amtolea nje nyota wa Chelsea.
52.  Jenerali mchana nyavu ageuka balozi Japan.
53.  Mjadara wa posho waitikisa nchi.
54.  Dr. Slaa pakacha na chujio hayahifadhi maji.
55.  Abebwaye hukitazama kisogo cha ambebaye.
56.  Nani mwanamke shujaa ajitokeze tumuone?
57.  CCM ikiwatimua mapacha watatu tutawapokea AFP.
58.  Spika Makinda mbumbumbu asimamia asichokijua.
59.  Lowassa amkatia Kikwete rufaa.
60.  Munge arusha mpira Masijala.
61.   Mlema sijiudhulu ng’o.
62.  Bajeti iliyotolewa na Zitto haina masilahi kwa taifa.
63.  Ngono Big Brother sasa.
64.  Aliyezama baharini kusaka mwili wa osama aibukia patupu.
65.  Nilivyopiga ramli kumtafuta Mungu.
66.  Aki na Ukwa waja tena.
67.  Nilitema big ‘G’ kwa karanga za kuonjeshwa.
68.  Ray c akimbia nchi.
69.  Waziri, changu wateta kwa nusu saa Dom.
70.  Mainda, Steve Nyerere Mhhhh!.
71.  90% Mastaa wauza ngono bei cheee.
72.  Mrembo anaswa.
73.  Badra aanika chachandu zake adatisha midume.
74.  Asha Bakari vimwana Twanga pepeta ni zaidi ya miss.
75.  Mchumba aliyevua nguo shereheni.
76.  Lina sina mtu kwa sasa niko single.
                                                                              16.
77.  Belina alizwa viatu, atangaza dau.
78.  Kalala Juniour bifu za kijinga siyo ishu.
79.  Kuolewa si kila kitu dada’ngu vuta subila.
80.  Aliyemwaga radhi hadharani aachwa kwa taraka tatu.
81.  Jenifer Aniston amwenzi mbwa wake kwa totoo!
82.  Wanaomjua waanika siri zke.
83.  Mrembo anaswa akichimba dawa hadharani.
84.  Lina sina wakumpa penzi.
85.  Mbunge CHADEMA amlipua Sitta.
86.  Lowassa alizwa na kujiudhuru kwa Rostam.
87.  Mikopo ya elimu ya juu yaitafuna wizara ya elimu.
88.  Lowassa amlilia Rostam.
89.  Rostam adaiwa kumkejeli Kikwete.
90.  Ngeleja uso kwa uso na wabunge leo.
91.  Uamuzi wa Rostam kuachia ngazi watikisa nchi.




            
                                                            
                                                           MAREJEO.
Kihole, Y.M.(2004) Maswala ya kisarufi katika magazeti ya mitaani ya kiswahili: Tanzania.
              Mtandao www.ifeas-uni-mainz.de/SwaFo/SF11%20 kihore.pdf
King’ei, K.(2000) Matumizi ya Lugha kwenye vyombo vya habari. Kenya:  Mtandao
Mgazeti, Mtanzania, Kiu ya jibu, Ijumaa, Rai, Majira, Uhuru, Nipashe, Mwananchi, Bingwa,
             Mwananchi,Sani,: ya kuanzia Mei-Julai (2011).
Mulokozi .M.M.(1996)Utangulizi  wa  Fasihi. Dar  es  salaam:Taasisi  ya  Uchunguzi wa
               Kiswahili.
Wafula. R.M. na K.  Njogu (2002) Nadharia za Uhakiki wa Fasihi. Nairobi: Jomo Kenyatta
               Publishers Ltd.
Wamitila. K.W. (2006)Uhakiki wa Fasihi:Misingi na Vipengele Vyake. Nairobi:Kenya Litho
                Ltd.
  www.landmark.edu/library/citation-guides/apa.cfm Iliyosomwa Tarehe 23 juni 2011 saa
                11:41
                                                                        14